HALI YA KIROHO YA ARDHI INAVYOHUSIKA NA KUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO

KUTAZAMA VIDEO YAKE BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


PICHA ZAKE ZOTE AKIWA MTUPU BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


MWINJILIST: LAURENT ELIAS MPOMA

LENGO YA SOMO:

Kuhakikisha ya kwamba Mafanikio yako yaliofungwa kwenye hali ya kiroho ya ardhi yanafunguliwa

Leo tuangalie jambo moja tu kufungua mafanikio yako yaliyofungwa na hali ya kiroho ya ardhi inayofanya mahali unapoishi pawe nyumba ya utumwa

Kumbukumbu 6:12

Angalia vizuri sana haya maneno Nchi ya misri, nyumba ya utumwa

Angalia haya mambo vizuri kwa kutazama mambo yafuatayo

1 Kufuatana na 2nyk 7:14 nchi maana yake ni ardhi yenye mipaka halali ya kuumiliki. Biblia ya kiingereza maneno ya mwisho inasema kuiponya nchi yako (I will heal their land)

Taifa ni tofauti na nchi linahusisha mkusanyiko ya watu hasa linapozungumza maswala la uongozi waliokubaliana, lina mlolongo wake utegemea nchi na nchi na katiba waliyo nayo.

Ukitoka kwenye taifa utakuta kabila, kabila utakuta jamaa, ndani ya taifa kuna lugha.

Nchi imegawanywa tofautitofauti na mipaka yake.

Kiblia Taifa linaweza kuwepo lakini lisiwepo kwenye nchi yake. Wana wa Israeli walikuwa Taifa lakini si kwenye nchi yao

2 Ukilinganisha mstari huu wa 2nyk 7:14 na ile Kumb 6:12 utaona ya kuwa hali ya kiroho ya ardhi inaweza ikageuza eneo kuwa nyumba ya utumwa

Kumb 6:12

Nchi maana yake=2nyk 7:14 nchi hiyo inaitwa Misri

Nchi ya Misri nyumba ya utumwa kwa hiyo ardhi imefanyika nyumba ya utumwa au ardhi ina uwezo wa kufanya eneo likawa nyumba ya utumwa

3 Utumwa wa wana wa Israeli ulikuwa ni wa kiroho lakini ulijitokeza katika maisha yao ya kila siku

Sababu 3 zinakazokusaidia kueleza jambo ili

MOJA

Shida haikuwa kazi waliyokuwa wanafanya lakini ni hali/mazingira ya kiroho ambayo walikuwa wanafanya hiyo kazi

Kut 1:11-14

Kazi walizokuwa wanafanya Misri walizifanya pia Kaanan. Walifanyishwa kazi ngumu

Sasa si kila kazi ngumu ni kazi ya utumwa. Walishughulika na chokaa, matofali na kujenga miji na mashamba

Swala si aina ya kazi ndo iliwafanya kuwa watumwa bali mazingira ya kiroho

Walipokuwa wanamlilia MUNGU hawakumlilia sababu ya kazi walizokuwa wanafanya bali sababu ya utumwa Kut 2:23

Utumwa si kazi ni hali ya kiroho/mazingira ya kiroho yanayotengeneza aina fulani yamaisha ambayo:-

Ubana fikra za watu,

Ubana maamuzi yao,

Uweka mipaka kwenye maisha yao na kwenenda kwao

Si watu wengi sana wanaweza kujua wako kwenye hali ya utumwa sababu ya kazi wanayofanya maana kazi hiyo hiyo mwingine anaomba kufanya

PILI

Walishindwa kujitoa

Kama ingekuwa ni swala la kazi kwanini wasiache?

Kila siku walalamika kazi ngumu kazi ngumu kwanini usiandike barua ya kuacha? Utafute iliyo nyepesi?

Unapokuwa mtumwa kwenye mazingira ya nyumba ni tofauti nay ale ya gerezani

Yule aliyekwenye nyumba inamchukua mda mrefu sana kujua kama ni mtumwa

Kama MUNGU asingewatangazia kwamba wako utumwani wasingejua.

Walipokuwa wanalia MUNGU awaondolee uchungu wa ule utumwa MUNGU akaondoa utumwa maana huo ndio uliosababisha uchungu ndani yao

TATU

MUNGU aliwatoa kwa nguvu

Kumb 7:8

Swala alikuwa kazi bali ni ile hali ya mazingira ya kiroho iliyowafunga kwenye utumwa



4 Waishio ndani ya nyumba wanatambuliwa kiroho kwa kuangalia jina la mmliki wa nyumba hiyo

Esta 8:1-2

Soma ile Esta 7:10

Amani hayupo, nyumba yake kapewa Esta

Katika ulimwengu wa roho nyumba zinatazamwa tofauti na tunavyotazama, angalia na Modekai naye akapewa pete ya Amani na Esta akamweka Modekai juu ya mlango wake amani

Kumb 6:12

Nchi ya Misri nyumba ya utumwa weka misri haijalishi uko nchi gani kama wewe ni Mmisri uko duniani unatambulikana kama mtu wanyumba ya misri au nchi ya misri kuna alama inayokutambulisha

Nyumba ya Israeli na nchi ya Israeli, wana kitambulisho katika ulimwengu wa roho kinachofanana

Amani alikufa na aliyepewa mamlaka juu ya nyumba yake alipewa Esta haijalishi walikaa kikao cha kuchagua msimamizi

Modekai alipewa mamlaka kwenye lango la nyumba ya amani, haijalishi hawako nyumbani wakati huo lakini wako na alama waliuwawa wote

Ukiwa na alama kwa ajili ya uangamifu utapata shida sana. Kama nyumba ya baba yako inamilikiwa na adui utapata shida sana

Math 12:29

Nani anayemiliki nyumba na uzao wako?

Uwezi kuwafungua waliofungwa kabla ya kushughulika na Yule aliye juu yao

5 MUNGU aliwatoa wana wa Israeli toka kwenye nyumba ya utumwa kupitia kwenye mlango wa nyumba ya utumwa

Kut 12:13-23

Alitumia kitu gani?… Jibu ni DAMU YA AGANO

Hakuwapitishia dirishani bali mlangoni lakini ilikuwa lazima DAMU YA AGANO itumike kuwatoa

Nchi ya Misri kipindi kile yote ilikuwa chini ya mazingira ya utumwa iliitwa nyumba ya utumwa na MUNGU alikwenda kuwafuta uzao wa Ibrahimu, Isaka na Yacoko sababu ya kiapo alichowaapia kwamba kuwatoa wana wa Israeli utumwani (walikuwa na alama) hakwenda kumfungulia kila mtu atoke

Mafanikio yao na kukua kwao kulikuwa kumefichwa na kukamatwa na mazingira ya ardhi ya Misri na walikuwa hawajui

Angalia ardhi ya nyumbani kwenu ama mahali ulipo kama ina mtawala anayetumia ardhi hiyo kama nyumba ya utumwa kuwa na uhakika utapata shida sana kutoka

Mfano nyumba ina vijana wana akili sana wana uwezo wa kufanya biashara, ana uwezo wa kufundisha na kufanya kazi lakini wako nyumbani na wale wajirani hawana hata shule lakini wako kazini.

Wakati mwingine unafikiri ni sawasawa sababu yuko kwako au nyumbani ujajua kuwa ardhi imegeuza nyumba yako kuwa nyumba ya utumwa

Kama baba yako alisimama na MUNGU mahali akaweka agano usifiriki shetani atakuachia kirahisirahisi katika mambo yako ama kuamua kwako.

Utashangaa kwako tu mambo hayaendi lakini kwa wengine yanaenda…hii yote ni yale mazingira ya kiroho yakibadilishwa na mambo yote yanabadilika

Ujawahi kuona mtu anahama kutoka kwenye nyumba ya kupanga kwenda kwenye nyumba yake gafla mambo yake yanasimama kiroho hata kiuchumi?

MUNGU aliwapitishia wana wa Israeli langoni ili kujua kuwa walikuwa kwenye nyumba.

Wengi wamefungwa:-

Kufikiri kwao

Kutokupata msaada mahalipopote pale

Wasipate kazi

Wakae tu nyumbani

Kitu cha imani wakifikiri wako kiroho. Hawafanyi kazi na ni watumishi wanatakuishi maisha fulani ya kiutumishi hivi, hawafanyi biashara wala kazi yoyote, wengine wameacha masomo yao

YESU anasema nyumbani mwa BABA yake, na pia anasema kanisa ni nyumba yake kwa hiyo, alama ya kiroho ya kanisa inategemea jina la kanisa.

Kama unasali kanisani hujui jina la mchungaji wako basi ujue alama yako ya kiunganiko chini ya mchungaji imepotea

Ardhi ni kama kompyuta kubwa ukikanyaga ardhi inafahamu na kama haikufaamu upeleke taarifa kwenye system yake kujua background yako na ndiyo maana ukikataliwa mjini hata mashambani utakataliwa na ukibarikiwa mjini na mashambani umebarikiwa

MAOMBI

<NGUVU YA MUNGU KWANZA>

 >>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

 ENDELEA  SIKU YA PILI  

KUSUDI LA SOMO:

Kuhakikisha ya kwamba Mafanikio yako yaliofungwa kwenye hali ya kiroho ya ardhi yanafunguliwa

Kumb 6:12, 2Nyk 7:14

Pitia somo la jana ili kujua tulipotioka nay ale mambo ya msingi 5 juu ya kufungua mafanikio yako yaliyofungwa na hali ya kiroho ya ardhi inayofanya mahali unapoishi pawe nyumba ya utumwa

Kumbuka jambo la msingi utumwa wa wana wa Isareli haukuwa sababu ya kazi walizokuwa wanafanya bali ni kwa ajili ya hali ya kiroho ya mazingira ya kazi walizokuwa wanafanya

Walimlilia MUNGU juu ya uchungu moyoni mwao wakati wanafanya kazi wala si kwa sababu ya kazi kuwa ngumu

Leo tuangalie NAMNA YA KUJIONDOA KWENYE MADHARA YA LANGO YA ARDHI YA NYUMBA UNAYOISHI INAPOMILIKIWA KIROHO YA NGUVU ZA SHETANI

Ni jambo pana na jipya kwa watu wengi neema ya MUNGU na iwe juu yako kuweza kuona na kufahamu jambo hili maana kujua na kufunguliwa katika jambo hili utafunguliwa katika mambo mengi sana

Esta 8:1-2, 13-14

Mwz 22:17

Math 12:29

Kut 12:12-23

Tuangalie vipengele vichache vya jambo hili ili iwe rahisi kuelewa

1 Ardhi na nyumba iliyojengwa juu yake vina uhusiano wa kiroho

Unasema unajuaje…..?

Kufuatana na Kumb 6:12 MUNGU amelinganisha nchi na nyumba kwa hiyo ardhi ile ambayo ina mipaka halali inauhusuano wa kiroho na nyumba inayojengwa

2 Mlango wa nyumba una uhusiano na mlango wa ardhi

Kwanini? sababu kama ardhi ina uhusiano wa kiroho na nyumba basi na milango yao ina mahusiano

3 Ukigusa mlango wa ardhi kiroho unagusa pia mlango wa nyumba kiroho

Matendo 16:26

Tetemeko lile halikuwa la kawaida lile la kuangusha nyumba bali lilikuwa lile la kushughulika na ardhi ambayo juu yake gereza lilikuwa lipo

Sababu walikuwa wapo gerezani kwa jinsi ya mwili isingekuwa rahisi wao kutoka maana hawakufungwa kimwili bali kesi yao mpaka kufungwa kwao ilikuwa kiroho

Ndiyo maana MUNGU alileta tetemeko akatikisa misingi ya gereza na Biblia inasema milango ya gereza ikafunguka haisemi ikavunjwa na vifungo walivyokuwa wamefungwa vikaachia

Yule askari alipoona milango iko wazi alitaka kujiua maana alijua wametoroka lakini walimwambia asijiue akawakaribisha kwake akawanawisha miguu na kuwatayarishia chakula na baada ya hapo walirudi gerezani

Kulipokucha asubuhi wale makadhi waliowafunga walitoa order ya wakina Paulo kuachiliwa.

Nini nataka uone hapa gereza halikuvunjwa wala kuwa na nyufa hata moja kutoka kwenye lile tetemeko

MUNGU hakuwa na shida na gereza la nje bali alikuwa na shida na gereza la kiroho ambalo kwa jinsi ya nje watu wanaona kama vile kuta tu na linaweza kuwa sehemu yoyote ile

MUNGU alikuwa anashughulika na ardhi  ili kushughulika na nyumba iliyo juu ya ardhi akafungua milango ya ardhi ili kufungua milango ya gereza iliyoko juu yake

Kama nyumba yako ni ya utumwa imezungukwa na mazingira ya utumwa usiangaike kuombea nyumba bila kuombea ardhi ya nyumba hiyo maana mlango wa ardhi una uhusiano na mlango wa nyumba yako

Vita ya ardhi si vita ya kumshirikisha kila mtu maana ina mapamabano yake mabaya kama ujajipanga

Kama huna NENO la kutosha ndani yako MUNGU akikusemesha uwezi kusikia maana kusikia huja kwa NENO la KRISTO maana waweza kushughulika na ardhi MUNGU akikwambia shughulikia mlango la ardhi

Wakina paulo walienda kuhubiri wakatengeneza mahali pa kusali bila kucheck na kushughulikia nani anamiliki lango la ardhi/nani ni mmiliki wa lile eneo

Waulize watu wa nyumba ya amani maana kiroho nyumba yake ilikabidhiwa Esta na Modekai sasa haijalishi kikao cha milathi kimeamua nini maana wamiliki ndio wanaoamua na kutoa ruhusa hali ya kiroho na hali ya maisha ya nyumba hiyo inaendaje

Unaanzisha kanisa/fellowship mahali badala ya kuangalia na kucheck nani ameshikiria lango la roho nyingine inayopingana na kitu unachofanya na ambaye ameshikiria lango la ardhi ambalo pia ndilo limeshirikia lango la nyumba ya sehemu hyo na msingi wa kiroho unayotumia kusali sasa kama vifungo hivi vimefungwa kwenye ardhi na vikaja kuonenakana mpaka kwa nje usipojua namna ya kuvifungua kwenye ardhi uwezi kufunguka

Angalia habari ya kina paulo kama waliendele na maombi kikundi cha cha ibada kikavurugika wakafungwa jera hata baada ya kutolewa gerezani walifukuzwa kutoka nje ya mji sababu walianzisha huduma mjini bila kusimamia malango ya ardhi ya mji

Matendo 16:39-40

Walipotoka gerezani walienda kwa Lidya na kukutana na ndugu/wapendwa tu na wale wapendwa waliwafariji tu hawakuwa wa msaada nao wakaenda zao

Ndiyo maana chunga sana watu wanaokushabikia huduma wakati hawajui vita unayopitia, chunga sana watu wanakusumizia front line wakati hawajua kupigana sababu ukifungwa gerezani watakufariji na kukupa pole na kusema tunakuombea na wakati hawajui hata wanachoomba

Mji ule ulikuwa na wapendwa lakini hawakuweza kuwasaidia kina Paulo sababu inategemea ni nani aliyeshirikia lango la ardhi kiroho la mji ule.

Maana walioshirikilia kama hawaitaki huduma kuwa na uhakika itafungwa na watu kuamia kwenye huduma ama kanisa jingine hata kama wapendwa wapo na usije fikiri watakusaidia watakufariji tu

Vikundi vingi sana vya maombi watu hawajui ni kwanini gafla vimechanua na gafla vimekufa sababu ni moja tu ulianzisha kikundi cha maombi bila kushughulikia lango la ardhi ambalo Modekai ndiye aliyeshikiria lango hilo na kama uko kinyume naye kuwa na uhakika kikundi hicho kitafungwa kabisa

Ndiyo maana unaweza kukuta makanisa mengine yanapata shida eneo hilo lakini nyumba nyingine hazipati hiyo shida ama kanisa moja linapata shida na jingine walaa sasa ni mambo mawili au moja lina operate kwa viwango vya juu sana au siyo tishio

Ndiyo maana watu wengi wanapata shida kwenye nyumba zao Biblia inaita nyumba za kitumwa na wako kwao.

Umewahi kufikiri kwa mfano hicho kiwanja ulichonunua ni nani anamiliki lango la hicho kiwanja katika ulimwengu wa roho?

Nani amepewa kumiliki ardhi uliyojenga? Wengine alipewa marehemu sasa ukichanganya jambo hili kiroho kuwa na uhakika kama usipojua namna ya kutengeneza kisiwa cha ardhi ya kwako utapata shida sana kuvuka na vita yake si nyepesi

4Kama vile nyumba ilivyo na mlango zaidi ya mmoja vile vile na ardhi ina milango zaidi ya mmoja inayoweza kutumika kumfunga mtu

Isay 26:1-2

Nchi ili kurikaribisha taifa, taifa lazima lipite kwenye lango.

Anapozungumzia lango kwenye nchi anazungumzia lango la kwenye ardhi linaloruhusu watu kupitia, kuingia na kutoka

Matendo 16:26-27, 24

.milango… Biblia haituambaii milango ilikuwa mingapi mlinzi alipoamka alikuta milango yote imefunguliwa na funguo anazo yeye.

5Kila lango la kiroho katika ardhi au nyumba lina walinzi wa kiroho

Matendo 12:6,10

Kuliwa na walinzi kwa ajili ya petro na kulikuwa na walinzi kwa ajili ya mlango/nyumba

Kuna mapepo unapewa wewe ukitoka nyumbani unakuwa nayo na kuna yale yamepewa kulinda ardhi ya nyumba yako hayatoki.

Alipofika kwa wapendwa waliokuwa wanaomba aligonga mlango (maana yake wakikupa kibali na kukufungulia ingia) malaika alazimishi wapendwa kufungua, wakati huku pengine malaika alimpitisha na milango kufunguka yenyewe. Swala ni kwanini hawakumfungulia? maana yuke dada hakufungua mlango baadaye walikuja wakamfungulia

Ardhi lile lilikuwa na malango 4, walipita lindo la kwanza na la pili hata mlango wa chuma na wa kuingilia mjini na mpaka kwa wale wapendwa waliokuwa wanamwombea kuna watu amabo wamefungulia lakini wako gerezani.

Fikiri Petro kama malaika alipomtokea angemwambi avae nguo na viatu kisha akapotea maana yake nini yuko huru keshavaa nguo na viatu lakini yuko gerezani kafungwa hana uhuru tena

Ndiyo maana tuna watu wengi sana tunawaombea na inapofika kwenye kufunguliwa kwako tunafunga mlango tunatamani kuwaomba kwenye chumba cha maombi lakini kuwafungulia hatufanyi hivyo.

Wengi tunawaombea halafu tukikutana nao tunakumbuka na kuona lile tatizo bado kwako hata kama wamebadilika kwa hiyo tunajikuta bado hatujawafungulia gafla wanarudi gerezani

6Omba kwa imani na kwa juhudi hadi aliyefungwa apite milango yote iliyomkwamisha

Matendo 12:5

Waamuzi 5:8

Kati ya eneo la uwanja la mapambano la MUNGU ni langoni

Petro ililazimika avuke geti 4, mbili ndani ya gereza, moja ndani ya mji na nyingine kwa waliokuwa wanamwombea hivyo MUNGU akikupa eneo la kuwavusha watu na kukupa namna ya kuomba omba mpaka uwavushe geti zote

Wakati mwingine unapohitaji msaada wa vita unahitaji watu ambao wanajua kupigana uhitaji msaada wa pole hata kama ni pole bali hawata nyamaza mpaka umetoka

MUNGU atakupa mamlaka ya kukanyaga na kukika malangoni na kuachilia DAMU YA YESU hapo maana hii ni ahadi ya MUNGU kwa Ibrahimu

<NGUVU YA MUNGU KWANZA>
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>


ENDELEA  SIKU YA TATU  


SOMO: HALI YA KIROHO YA ARDHI INAVYOHUSIKA NA KUFUNGWA AU KUFUNGULIWA KWA MAFANIKIO YAKO

LENGO YA SOMO:

Kuhakikisha ya kwamba Mafanikio yako yaliofungwa kwenye hali ya kiroho ya ardhi yanafunguliwa

Kumb 6:12, 2Nyk 7:14

SUMMARY YA SIKU 2

>>Pitia somo la siku ya kwanza na siku ya pili ili kujua tulipotoka maana kuna yale mambo ya msingi 5 juu ya kufungua mafanikio yako yaliyofungwa na hali ya kiroho ya ardhi inayofanya mahali unapoishi pawe nyumba ya utumwa siku ya kwanza na vipengele 6 vya namna ya kujiondoa kwenye madhara ya lango ya ardhi ya nyumba unayoishi inapomilikiwa kiroho ya nguvu za shetani kwa siku ya pili

>>Somo hili halifundishwi kama ile kawaida ila kila siku MUNGU anampa kitu kipya ili yule atakayesikiliza kwa siku hiyo atapata jibu lake

==>Si watu wengi pia wanalipokea kwa haraka sana mioyoni mwao somo hili na kwa sababu hiyo ROHO MTAKATIFU anarirudia na kurirudia ili lizidi kujengeka ndani yetu

Leo tuangalie KUFUNGULIWA TOKA KWENYE KIAPO KILICHOIFUNGA NAFSI YAKO NA HALI YA KIROHO YA ARDHI

Na katika kulitazama jambo tuangalie mambo kadhaa ambayo MUNGU ameachilia ndani ya kichwa cha Mtumishi ili yamkini yatufikishe mahali pa kuweza kuingia kwenye maombi na wale ambao kuna viapo vimewafunga wapate kufunguliwa

1Njia mojawapo inayounganisha mafanikio yako kimaisha na hali ya kiroho ya ardhi ni maagano

Mwz 9:13

2Nyk 7:14

Anazungumzia juu ya kuiponya nchi yao na kumbuka nchi ni ardhi lenye umiliki halali na ina mipaka kabisa. Biblia ya kiengereza imewaka wazi kabisa inazungumzia juu ya ardhi

Sasa tazama kitu ambacho MUNGU alifanya wakati Nuhu ametoka kwenye safina wako watu wachache waliojulikana kama wapo na wanyama na ndege, ukisoma ile sura ya 8 na 9 na alipozungumza nao kwa habari za agano

..Anasema ni ishara ya agano kati yangu na nchi na hasemi ni ishara ya agano kati yangu na wewe bali ni ishara ya agano kati yangu na ardhi

2Ishara ya agano hilo juu ya ardhi husika kazi yake ni hizi zifuatazo:

MOJA (i)

Kazi kubwa mojawapo ni kukumbusha kuwepo kwa agano

Mwz 9:13-16

Tazama maneno haya….nami nitalikumbuka agano langu lililoko kati yangu na ninyi…..

Kukumbusha kwa watu wote waliohusika na maagano, kiswahili kinakosa lugha iliyo nyepesi sana juu ya neno agano maana tukisema ni mapatano halitoshi au mapatano ya kimkataba linasogea kidogo maana agano ni pana kidogo

Jambo ambalo watu wengi hawafahamu Agano haliwezi kuwa Agano isipokuwa kuna kitu cha kiroho kati yake, kunaweza kuwa na mapatano lakini hakuna kitu cha kiroho kati yake

MBILI (ii)

Kukumbusha kuwepo kwa kiapo kwa sababu ishara ni alama ya uhaminifu kwenye kiapo husika

Yosh 2:11-13-19

Rahabu alipokuwa amegundua ukombozi wake umekaribia, kivipi ni kwa imani kama Waebrania isemavyo, kwa hiyo hakuangamia pamoja na waovu wengine sababu aliwakaribisha wale wa pelelezi kwa furaha, kwa shukrani na kwa imani

Swali la msingi kwanini MUNGU asiwapitishe pembeni ya mji wa Yeriko kwa safari yao ya kwenda Kaanani? Maana mji ule uliangamizwa wote na watu wakao humo isipokuwa Rahabu na familia yake na hata wakati wanaondoka Joshua aliachilia laana ili asiwepo mtu wa kujenga hapo

Fahamu ili kilichomfanya MUNGU aende Yeriko ni Rahabu peke yake hakuna kitu kingine chochote kilimpeleka kule maana Rahabu alikuwa na destiny, alikuwa na kitu katika maisha yake na shetani alifikiri akiachilia uasherati ndani yake na kumfunga katika ardhi ya mji wa yeriko hakuna atakaye mkumbuka. Ukitizama utaona tokea pale MUNGU alimwamisha na kumwingiza katika familia ya wayahudi yeye pamoja na familia yake na kumjengea maisha yake ya baadaye

Mji waYeriko ulifungwa wote kwa jinsi ya kiroho si ya mwili na ndiyo maana ilifunguliwa kwa jinsi ya kiroho. Gharama zote za kuuzunguka mji ule siku zote 7 kama angeulizwa angejibu ni Rahabu ndiyo maana walinyamazishwa

Kuna kitu MUNGU anaweka katika maisha yako na shetani anajaribu kukuzamisha kabisa, haijalishi mahali ulipo, haijalishi shetani amekufunguka kwa namna gani kama ni katika uasherati ama wizi au shida ili kusudi ile ndoto MUNGU aliyoweka ndani yako isije kuchipua SIKIA NENO LA BWANA MUNGU ATAKUFUATILIA NDANI YA YERIKO NA ATAKUTOA NA SI TU KUKUTOA YERIKO NA ATAKUTOA KATIKA UASHERATI atakuweka katikati ya watu amabo kila mtu atashangaa umetokea wapi na hawataacha kusema IMANI yake imemtoa pale na kumfikisha hapa na kusema yuko MUNGU ambaye anaweza kushughulika na ukahaba

Ilichukua jeshi lote la Israeli kumtoa mtu mmoja

“Ndiyo maana saa nyingine ninaposimama kwenye madhabahu huwa sijaribiwi kufikiri na wingi wa watu nafikiria kuangalia mtu mmooja ambaye MUNGU amemkusudia”

Rahabu aliwaapisha kwa kusema ninawaapisha kwa BWANA, maana yake ninawafunga kwa MUNGU wenu alafu akasema wampe alama ya uhaminifu, wakasema tusije tukaingia hatia ya kiapo ulichotuapisha…funga kamba hii, wale wapelelezi walikuwa wanatembea na kamba nyekundu ni kamba waliyokuwa wanatembea nayo ili ijulikane ni watu wa agano.

TATU (iii)

Kukumbusha masharti yaliyoambatanishwa na kiapo

Hakuna kiapo kisichokuwa na masharti ili kuonyesha hakuna agano lisilokuwa na masharti na ni masharti ya kisheria na kihalali ile roho iliyowaunganisha kwenye agano kazi yake ni kufuatilia masharti

Ndiyo maana alipowaapisha kwa BWANA walimpa masharti:

Uruhusiwi kusema

Hakikisha ndugu zako unaowataka waje aje

Hawaruhusiwi kutoka nje

3Kiapo cha agano kinabeba wahusika wakufuatiliwa

Yosh 2:12-13

Rahabu wakati anazungumza na wale wapelezi hata kuingia kwenye kiapo ndugu zake hawakuwepo lakini aliingiza jina la baba, mama yake na ndugu zake na listi ya vitu walivyokuwa navyo kwa hiyo kila kilichitajwa hakikurusiwa kuwa nje ya nyumba

Kuna watu ndani yamioyo yao MUNGU amewabebesha familia, wengine kampuni, wengine kanisa unamwona yuko peke yale lakini hayuko peke yake ndani yake amebeba majina ya watu na vitu vyao na kila mahali anawakumbuka kwamba anao.

Kumbuka habari ya yule tajiri aliwabeba ndugu zake aliokuwa anawabeba kwenye pesa na alijua watapita na kuja njia hii hii wale ndugu watano akataka wapelekewe taarifa mapema

Joshua alipewa watu wa kusafiri nao na watu wote wale urithi wao ulikuwa kwa Joshua

Watu wa namna hiyo katika ulimwengu wa roho wana alama zao ambazo zinafuatailiwa kila wakati na unapoingizwa kwenye kiapo haijalishi kwamba umekubali ama hujakubali swala ni kwamba aliyekuingiza kwenye kiapo ana sauti gani juu yako..kupitia kwenye kizazi, uhalali wa kukaa mahali pamoja

Kama mwenye nyumba ameapa kwa mungu wake juu ya ardhi ya hapo kwake ambayo na wewe unakaa maana yake amekuingiza kwenye kiapo

Ndiyo maana vipao vya maagano vinasumbua sana maana vinafunga watu hata kama hawajui kama wamefungwa

4Kiapo kinafungamanisha nafsi ya mtu na alichojiapiza

Hes 30:2 (Mahusiano ya kiroho kati ya baba na binti yake)-Daka hiyo ilikuwa aja ya Mtumishi akafundishwa na MUNGU

Kwa hiyo kiapo ni kifungo na kiapo kinafunga nafsi na kitu ambacho mtu ajiapiza nacho

Rahabu alipowaambia niapie kwa BWANA alikuwa anafunga nafsi za wale wapelelezi kwa kitu watakacho kisema, walijua kabisa huyu anazungumza kitu cha kiagano

Math 5:33-36

YESU alizuia viapo mahali ambapo havitakiwi kuwepo, kuna vitu alivitaja kwa maskudi kabisa:-

Usiape kwa kichwa chako

Usiape kwa mji wa Yerusalem

Usiape kwa mbingu na

Usiape kwa mji

Usiape kwa ardhi

YESU kwa lugha nyingine alikuwa anatufundisha kuwa waangalifu katika kuapa maana kuapa ni kuifunga nafsi yako na ardhi na roho iliyoko mahali pale inabana hayo maneno uliyotamka mahali hapo

5Ishara ya agano inafanya wahusika wafuatiliwe katika ulimwengu wa roho kujua ikiwa masharti ya kiapo yanazingatiwa

Ukisoma habari za MUNGU na agano lake la ibeahimu, isaka na yakobo utakuta anasema …kile kiapo nilichowaapia baba zako…MUNGU anamwambia mussa sijakufuata kwa ajili yako ila jina lako kwenye kiapo, nifuatilie toka ukiwa tumboni, nicheck utavyoishi na kula saa ikifika nijifunue kwako, nataka kucheck kama unafuata masharti

Wewe unaweza kusahau juu ya masharti ya kiapo lakini MUNGU hawezi kusahau

Miungu inaingia mikataba katika ardhi kwamba ikufanikishe ama isikufanikishe katika ardhi kwa nini sababu kwenye ardhi ndiko kulikowekwa siri ya mafanikio ya hapa duniani.

Ulimwengu mwingine wowote hauna udongo kasoro ardhini na mbegu zote za kiroho ziliwekwa ardhini kwa sabu Sura ya kwanza inasema kila kilichoumbwa kilikuwa ni neno na neno ni mbegu na sura ya pili kila kilichochipuka kilichipuka kutoka kwenye udongo kwa hiyo lile neno lilikuwa mbegu lilivyotamkwa MUNGU akaliweka kwenye udongo kwa hiyo udongo una mbegu za kiroho

Siri ya mavuzo yako iko kwenye ardhi, siri ya hali ya hewa iko kwenye ardhi na hii ni ishara ya agano MUNGU aliyoweka na Nuhu kwamba katika vitu alivyowekeana naye na ardhi ipo na kama ipo kuwa na uhakika na mbingu yake ipo maana utegemea na kufanya kazi pamoja

6Badala ya kukimbilia kuvunja agano badilisha na tangua kwanza kiapo ili kuliondoka jina lako na nafsi yako kwenye kifungo

Hes 30:2,10-15

Usipotangua kiapo yote yaliyosemwa kwenye kiapo yatatokea

Rahabu aliwaapisha kwa BWANA hakulijua agano likoje lakini alijiingiza kwa njia ya kiapo na kuvunja lile agano ilikuwa kutengua kile kiapo kwamba watu wale/ndugu zake wasikae ndani ya ile nyumba/ ndani ya lile agano.

Sasa kiapo kile hakitawafunga hata kama agano lipo

Shida watu wengi sana wanakimbilia kuvunja agano wasilolijua limefungwaje na limefungiwa wapi na vitu gani vimehusika kwenye agano.

Usijaribu kumkwamua mwingine wakati wewe umekwama toka wewe kwanza



Joshua aliwaambia watu chagueni hivi leo ila mimi na nyumba yangu tutamtumikia MUNGU wakasema nasi tutamtumia huyo MUNGU akawaambia kwanza ondoeni alama za miungu yenu kwanza

Ukifunga nafsi kwa kiapo usipotangua kila ulichokisema kitatokea na kinaweza kukusumbua miaka na miaka. Unatangua kwa kutumia DAMU YA YESU maana ni DAMU ya AGANO na ni DAMU BORA kuliko damu zozote zile

7Miguu yako ni lango rahisi la kutumia kuifunga nafsi yako na ardhi katika kiapo cha kiroho

Zab 56:6

Zab 57:6

Shetani anatumia nyayo kushika nafsi yako kwa hiyo anaotea nyayo zako. Shetani amekuwekea nyavu kwenye miguu lakini usikii nyavu unasikia moyoni mwako kukata tama, kila ukiganyaga usogei mpaka umeacha kutembea

Sasa unaweza kujua kwanini Rahabu alipokuwa anataka kutolewa kule ilibidi wazunguke kwa miguu siku zote zile, sababu miguu ya watu wa MUNGU inaweza kuachilia nguvu za MUNGU inapokanyaga mahali

Walipokuwa wanazunguka walikuwa wanatafuta misingi ya ile kuta zile hazikuwa kuta zimejengwa kawaida bali zilikuwa kuta za kiroho, sababu ile ardhi ilikuwa na misingi ya kiroho 7 na ule wa 7 ulifungwa mara 7. Kile kitu na kila mahali kulianguka chini kasoro nyumba ya rahabu misingi mingine yote ilibomoka

Kuokoka kwako na kupona kwako si sababu ya matendo yako bali ALAMA YA DAMU YA YESU moyoni mwako

<NGUVU YA MUNGU KWANZA>
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>



KWA NAFASI ZA KAZI POPOTE TANZANIA, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
[3.00 MB]VIDEO YA ALIKIBA AKIBANDUANA NA JOKATE, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



0 coment�rios: