UJUMBE: VIFUNGO VYA MWILINI

KUTAZAMA VIDEO YAKE BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


PICHA ZAKE ZOTE AKIWA MTUPU BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


Utangulizi:
Mungu anawapenda sana wanadamu na Biblia inasema wazi kuhusu hili katika kitabu cha Maombolezo 3:31; Ni raha yake kuona hatuna matatizo na tunaishi kwa amani. Mungu hakumuumba mwanadamu ateseke bali alimuumba afanikiwe akiwa duniani na kuishi kwa furaha.
Wakati huohuo, shetani kwa asili hapendi mtu aliyeumbwa na Mungu afanikiwe na ndio maana katika Luka 3:16 inasema, “…ambaye shetani amemfunga miaka kumi na minane…” (Matendo 10:38; 2Wathesalonike 2:18-19) kwa maandiko hayo tunaweza kujua kuwa shetani anaweza kufunga, kuzuia, kupinga na kushindana na mtu. Kwa asili shetani ni mshindani na furaha yake ni kuwatesa wanadamu ambao wanapendwa na Mungu. Yeye hufanya hivi ili kuumiza moyo wa Mungu kupitia wanadamu walioumbwa na Mungu.

SHETANI ANAWEZA KUMFUNGA MTU:
Kama tulivyoona kuwa shetani anapenda kuwatesa wanadamu na ili kutimiza lengo lake njia mojawapo anayotumia ni kuwafunga watu. Na tunapotaja vifungo, tunakuwa tunazungumzia vifungo vya aina kuu tatu, yaani, Vifungo vya mwilini, Vifungo vya rohoni na vifungo vya nafsini kwasababu mtu ni roho inayokaa ndani ya nyumba iitwayo mwili. Katika hatua hii ya kwanza tunaanza kuangalia kwa undani kuhusu vifungo vya mwilini:-

Mwili ni nini?
Hatuwezi kujua namna mwili unavyoweza kufungwa bila kujua asili ya mwili wa binadamu. Tuanze kwa kuangalia andiko hili Mwanzo 2:7 “BWANA Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya ardhi…” kumbe asili ya mwili wa mwanadamu ni mavumbi au udongo. Na ndio maana katika Isaya 64:8 Biblia inasema, “… sisi tu udongo nawe ni mfinyanzi wetu…” nabii Isaya ambaye aliwahi kumuona Mungu lakini alijua ukweli huu kuwa mwili ni mavumbi (Ayubu 7:21, 34:15). Kumbe pamoja na kuwa umevaa vizuri au umeupamba mwili vizuri lakini asili yake ni udongo na katika ulimwengu wa roho huonekana kuwa ni udongo kabisa. Kwa ufupi mwili wa mwanadamu ni udongo na mtu anapokufa mwili huirudia nchi (Mhubiri 12:7) yaani mavumbi.

Ndio maana hata watu wanapooana ni miili ndio ambayo inakuwa imeoana na si roho kwasababu mbinguni hakuna kuoa wala kuoana kule ni katika roho. Kwa kujua kuwa mwili ni udongo basi namna ambayo unaweza kuutendea udongo wa kawaida ndivyo vilevile waweza kuutendea mwili wa binadamu. Udongo wa ardhini waweza kuoteshwa mimea na kuchimbwa, vilevile na mwili wa binadamu waweza kufanyiwa hivyo.

TOFAUTI KATI YA MWILI NA UDONGO WA KAWAIDA:

Kuna mambo mawili makuu yanayosababisha mwili wa binadamu uwe tofauti na udongo wa kawaida.

1. Mwili uliwahi kushikwa na mikono ya Mungu maana hakuna kitu kilichowahi kushikwa na Mungu na kikabaki kama kilivyo.

2. Ndani ya mwili wa mwanadamu kuna roho ambayo huuisha mwili na kuupa uhai. Kwasababu hizo mwili wa mwanadamu hutofautina na udongo wa kawaida.

MWILI WA MWANADAMU UNAWEZA KUPANDIWA VITU:
Biblia iko wazi kuwa Mungu wa mbinguni anaweza kupanda, (Mwanzo 2:8); kumbe Mungu ambaye ni roho (Yohana 4:24) anaweza kupanda katika ardhi kabisa vivyo hivyo shetani naye ni roho naye ana uwezo wa kupanda katika mwili ambao kwa asili ni udongo. Hapa ndipo lile andiko la “KILA PANDO AMBALO BABA WA MBINGUNI HAKULIPANDA LITANG’OLEWA” linapoleta maana; Mapando ambayo hayajapandwa na Baba wa mbinguni ni lazima yatakuwa yamepandwa na shetani. Ndio maana ya mfano wa Yesu katika Mathayo 13:25 “lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.” Huyo ambaye Yesu anamwita adui ni shetani mwenyewe. Kumbe unapolala au kujisahau shetani huja na kupanda magugu, hili jambo linatendeka katika ulimwengu wa roho. Ni muhimu kujua siri hii kwamba kama vile udongo unavyopandwa vivyohivyo shetani naye anao uwezo wa kupanda juu ya mwili wa mwanadamu.

Unaweza kumsikia mtu analalamika kuwa mwili unachoma lakini kumbe katika ulimwengu wa roho mtu huyo amechomwa mkuki au kisu. Kufikia hapa sasa twaweza kujua kwanini Mungu alikataza kupanda mbegu mbili za tofauti katika shamba moja (Mambo ya Walawi 19:19). Mungu alisema hivi akitufundisha kuwa mahali ambapo Mungu amepanda shetani hatakiwi kupanda mahali pale. Mtu anaweza kuhisi vitu vinatembea mwilini kumbe amepandiwa wanyama wanaotembea katika mwili wake.

PEPO ANAWEZA KUJIGEUZA NA KUWA CHOCHOTE:
Tulijifunza kuhusu sheria mbili za rohoni, hapo tuliona uwezo wa pepo wachafu kujigeuza na kuwa kitu kingine yaani kuvaa sura mbali mbali ili kutimiza kazi zao. Jambo hili twaweza kuliona katika (1Wafalme 22:19-23) huyu pepo kwa asili hakuwa wa uongo lakini aliweza akaenda na akawa pepo wa uongo. Yule pepo akaingia katika vinywa vya manabii wa Mfalme Ahabu na kuwafanya wamtabirie uongo. Kwa maana hiyo tunaona uwezekano wa pepo mchafu kujigeuza na kuwa kitu chochote ili kutimiza lengo alilokusudia.

Sasa twaweza jua kuwa mapando tuliyokuwa tunayazungumzia ni pepo wachafu ambao hujigeuza na kuwa kile kitu na hivi ndivyo vinavyoitwa “Vifungo vya mwilini”. Wakati mwingine pepo anaweza kujigeuza na kuwa kinywa cha mtu, kama pepo wa katika (1wafalme 22:19-23) alivyofanya. Hivyo; unaweza kumuona mtu anatukana matusi ya ajabu bila hata aibu, kumbe pepo kajigeuza na kuwa kinywa chake. Pepo anaweza kuwa uso wa simba, unamkuta baba mwenye nyumba mkali kwa watoto na mkewe kumbe ni uso wa simba. Kwahiyo; pepo wanaweza kujigeuza maumbo mbalimbali kama nyani, simba, paka hata bundi ili mradi kuharibu hatma ya mtu. Mnamkuta dada aolewi kumbe uso wake umefunikwa kwa sura ya simba, kila mwanaume anayetaka kumchumbia haoni sura nzuri bali anaona simba. Na ndio maana kuna baadhi ya wadada watumia muda mwingi kujipodoa lakini bado hawapendezi kwa kuwa uso sio wa kwake.

KUNG’OA KILA KILICHOPANDWA KATIKA MWILI WAKO:
Imeandikwa kila pando asilolipanda Baba wa mbinguni litang’olewa, hivyo Mungu ametupa mamlaka ya kung’oa kila pando la kishetani yaliyopandwa katika mwili. Miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu hivyo shetani hatakiwi kugusa sehemu yoyote ya mwili wako.

Tumia mamlaka yako kung’oa kila pando ambalo shetani amepanda katika maisha yako mapando ya magonjwa, homa zisizoisha, ukimwi, mwasho wa mwili na matatizo mbalimbali. Jina la Yesu lina mamlaka yote dhidi ya kazi zote za shetani katika maisha yako.

Sehemu ya Pili.

Utangulizi:
Shetani hajabadilika na silaha zake ni zilezile; na jambo kubwa linaloshangaza watu ni kwamba silaha za shetani ni zilezile lakini bado zinatenda kazi kwenye maisha ya watu. Moja ya kifungo kinachosumbua watu ni kifungo cha tabia.

Mara nyingi kupata urafiki au uhusiano ni rahisi lakini ili uweze kuendelea kuwa karibu na watu hao unatakiwa uwe na tabia nzuri. Hivyo shetani anaweza kukuacha usonge mbele na kazi ya Mungu lakini akakuzuia kupitia vifungo vya tabia. Kwasababu hii Roho Mtakatifu ametaka leo tujifunze kuhusu vifungo vya tabia:

KIPAWA NA TABIA YA MTU:
Kuna vitu kadhaa vya kuangalia kama mtu wa Mungu unayehitaji kufanikiwa, cha kwanza ni kipawa na pili ni tabia ya mtu.

Mithali 18:16 “zawadi ya mtu humpatia nafasi, humleta mbele ya watu wakuu; ” hili neno zawadi kwenye Biblia ya kingereza linaitwa “GIFT” au kwa Kiswahili kipawa. Sasa basi kipawa cha mtu chaweza kumfikisha mbele za watu wakubwa na kujulikana. Mfano mtu anaweza kuwa na kipawa cha uwimbaji lakini anakaa kijijini na umaskini, ila kile kipawa chake kikionekana kinaweza kumleta mtu huyo mjini hii ndio maana ya sehemu ya kwanza ya andiko hilo. Kwasababu hiyo kila mtu aliyepo duniani amepewa kipawa na Mungu ambacho kwa hicho anaweza kufika kwenye hatua ya juu zaidi.

Sasa basi kipawa cha mtu humleta mtu kwenye mafanikio yake, tatizo linakuja pale mtu anapokuwa na kipawa lakini tabia yake si nzuri. Hivyo tabia ndio ambayo inakubakiza katika sehemu uliyopo. Mtu anaweza kuwa na macho ya rohoni au upako lakini kama tabia yake ni mbaya hakuna mtu atakayetamani kuwa karibu naye. Ili Mungu akutumie kwa kiwango cha juu ni muhimu kuanza kwa kubadili tabia yako.

TABIA ZA KIMUNGU NA TABIA ZA ASILI:
Biblia imeainisha tabia za aina mbili, yaani tabia ya Kimungu na tabia ya kiasili au ya mwilini. Katika 1Wakoritho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.” 1Wakorintho 3:1 kuna tabia za rohoni na tabia za mwilini. Hivyo anachosema Mtume Paulo ni kwamba unapoongea na watu inabidi ujue ama mtu huyo ana tabia za rohoni au za mwilini. Mfano mtu anaweza kuwa mwimbaji mzuri lakini ana tabia ya uongo; Mtu mwingine anaweza kuwa na kipawa kitakachomfanya apate mchumba; lakini kama tabia yake ni mbaya ama uongo, au umbeya au uzinzi inaweza kumfanya kuachwa na mchumba wake sio kwasababu hapendwi bali kwasababu ya tabia. Tabia ya Kimungu ni tabia njema na nzuri lakini tabia ya kibinadamu ni tabia mbaya aliyonayo mtu.

Shetani akitaka kuharibu kipawa cha mtu anaanzia kwenye tabia yake; kwa maana hiyo tabia ya kibanadamu au ya mwilini ndio hiyohiyo Biblia inaiita tabia ya kishetani. Ukisoma katika Yakobo 3:15 “Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.” Unaona kumbe tabia mbaya ya kinadamu ndio hiyo inaitwa tabia ya kishetani. Mhubiri 10:1 “Mainzi mafu huvundisha marhamu ya mwuza marashi; Kadhalika upumbavu haba ni mzito kuliko hekima na heshima.” Hili ni neno la hekima la Mfalme Suleimani kusema mainzi wanaweza kuharibu marhamu nzuri; ikimaanisha unaweza kupata mpenyo katika maisha lakini tabia mbaya inaweza kukupeleka mbali kabisa na upenyo wako.

Ndio maana waweza kumkuta mtu ni mwombaji au anatenda miujiza lakini tabia yake ikawa mbaya kwasababu ya asili. Jambo hili ndlo linalosabisha watu wengine kusema “kama ulokole ndio huu sitaki kuokoka” kumbe mtu huyo aliwahi kumuona mtu ambaye ameokoka na ananena au anaombea watu lakini ni mwongo au mzinzi. Katika Biblia, Samson alikuwa mnadhiri wa Mungu na alikuwa amepakwa mafuta tangu tumboni mwa mamaye. Japokuwa alikuwa mpakwa mafuta lakini alikuwa na tabia mbaya ya kutaka wasichana wa kifilisti ambao Mungu alikataza tangu mwanzo. Hii ni sawa na mtu kung’ang’ania kufungwa nira na mtu asiyeamini. Kwa njia hii Samson akakutana na Delila ambaye lengo lake halikuwa upendo bali ni kumharibia kipawa chake kwa kuijua siri yake. Vivyohivyo shetani amewaangamiza watu wa Mungu wengi kwa kuwafanya waoe au kuolewa na watu wasiomjua Kristo na matokeo yake kile kipawa cha Kimungu kilichokuwa ndani yao kinashindwa kuonekana tena.

KUBADILI TABIA:
Tabia mbaya ya mtu huondoka kwa kuamua mwenyewe, hata kama mchungaji akuombee mara zote kama tabia yako ni mbaya kwa asili inakulazimu kuamua kuibadili mwenyewe. Ni kweli tabia yako inaweza kuwa imeshakupotezea kibali kwa watu au imeshakupotezea upenyo katika maisha lakini ukiamua kuanza upya na BWANA na kuacha zile tabia mbaya Mungu wetu ni wa nafasi ya pili. Mungu wetu anatoa nafasi ya pili biblia inasema, “usifarahi ee adui yangu niangukapo mimi nitasimama tena”


Leo naongea na watu ambao walikuwa waombaji leo hawaombi tena, walimuhofu Mungu lakini leo hawana hofu, walikuwa watakatifu lakini leo ni waovu wakubwa Mungu anayo nafasi ya pili kwaajili yako. Amua kutubu na kuacha dhambi na tabia hiyo mbaya; Mungu atakuwezesha tena kama alivyomwezesha Samson kuwaangamiza wafilisti wote. Hivyo uamuzi wa kwanza ni kuamua mwenyewe kuacha tabia hiyo.
KWA NAFASI ZA KAZI POPOTE TANZANIA, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
[3.00 MB]VIDEO YA ALIKIBA AKIBANDUANA NA JOKATE, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



1 comment:

  1. IFAHAMU MIZIMU NA MAJINI NA UNDANI WAKE KATIKA KUOMBA LOLOTE MALI,UTAJIRI, UPONYAJI N.K......

    DOKTA MDIRO whatsp/call +255 742162843

    ANGALIZO HUSIJARIBU JAMBO ULIZA KWA MAELEKEZO

    Omba lolotee kwa njiaa ya mizimu mungu atatenda asema DOKTA MDIRO,

    Kuna watu wakisikia neno mzimu wanatimkaa mbio lakini wakisikia neno mtakatifu wanabarikiwa na wakati ni kitu kilekile kasoro jina tu.

    Daktari wa kiafrika anaitwa mganga wa kienyeji na wa kigeni ni Mtaalamu au mwanasayansi.

    Ibada takatifu zinaitwa Kusali na za lienyeji zinaitwa matambiko amka wacha kulala.

    watakatifu wa kiafrika wanaitwa mizimu, Mzimu nii binadamu yeyote yule aloachaa mwili na ANAISHIII na mungu karibu, kwaiyo sisi sote nii mizimu watarajiwa, unapomfananisha Mzimu na shetaani nikukataa ukuu wa afrikaa, wazungu Mzimu uloishiii vizuri dunian wanauita mtakatifu sisi mizimu iloishi vizuri na VIBAYA duniani tunaayaita mashetani.

    Ndiomaana ktk orodha ya watakatifu karibu wote wazungu, waafrika wa kuwahesabu, @highlight

    WAZUNGU KWENDA MAKABURINI WANAITA HIJJA , SISI KWENDA MAKABURINI TUNAITA MATANDIKO, HATA MZIMU WA NYERERE UMECHUKUWA MUDA KWELI KUFANYWA MTAKATIFU KWASABABU HAKUWA MZUGU.
    🤫DOKTA MDIRO ANASEMA MIZIMU INAFAIDA KUBWA KTK MAISHA YA MUWAFRIKA, KUIKATAA NI KUKUBALI BALAAA NA KUKUBALI NI CHAZO CHA BARAKA.
    NA MAISHA MEMA APA DUNIANI,
    😒 Mikosi, manyanyaso balaa, na gundu ulizonazo haziwezi kuondoka mpk ukutane na mizimu yenu .
    Dokta MDIRO ANAKUAMBIA MIZIMU YA BIBI YAKO NA BABU YAKO INAA MAJIBU YA MATATIZO YAKO.

    ReplyDelete