KANUNI ZA KUTEKA MIJI KWA AJILI YA BWANA,

KUTAZAMA VIDEO YAKE BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


PICHA ZAKE ZOTE AKIWA MTUPU BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



UTANGULIZI
                               Ndugu mpendwa napenda kukusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo.Pia ninapenda kukukaribisha katika kujifunza somo hili.Somo hili lina umuhimu mkubwa sana katika nyakati/majira       tuliyopo sasa.Kama kichwa cha somo kinavyoonyesha,somo hili ni somo ambalo naamini litakwenda kuleta mapinduzi ya kiroho katika jamii,familia na kanisa kwa ujumla.Nakushauri ulisome somo hili kwa mtiririko ili uweze kupata maarifa mapya na vitu vipya kutoka kwa Roho Mtakatifu.Lengo la kwanza la somo hili ni kukuandaa kama mwanajeshi wa Bwana,kwa ajili ya kuteka miji iliyo chini ya shetani na kuirejeza kwenye ufalme wa Mungu Baba.Sasa unaweza ukawa unajiuliza,swali hili;kwamba kwa nini mimi ndio niteke miji hiyo?kwanini Mungu mwenyewe asifanye kazi hiyo?Jibu ni kwamba Mungu huwa anafanya kazi pamoja nasi kwa ajili ya kutupatia mema[Rumi.8:28],Na mema hayawezi kuja kama miji tunayoishi itaendelea kuwa chini ya ufalme wa giza.Kwa nini tuteke miji wakati,aliyeumba miji yote ni Mungu  na wala sio shetani? 
                               Dhambi ya Adamu na Eva pale eden ilipelekea dunia yote kuwa chini ya shetani(yaani shetani akawa ndio mungu wa dunia hii)[2kor.4:4] badala ya mwanadamu. Kwa hiyo asilimia kubwa ya miji tunayoishi inamilikiwa na adui(shetani).Na ndio maana kazi ya Mungu inapigwa vita kwa kiasi kikubwa.Sasa lengo la pili la somo hili ni kukuwekea(impart knowledge) ufahamu utakaokusaidia kuirejeza miji hiyo mikononi mwako,kama mwakilishi wa ufalme wa Mungu.Kutokana na miji mingi kuwa chini ya shetani,matukio mengi ya kutisha yamekuwa yakitokea kila siku,mfano vifo vya ajabu,ajali za barabarani,mauaji ya albino nk.
                            Sasa shetani amekuwa akipofusha watu ili watu wasijue kuwa yeye(shetani) ndiye anayehusika katika matukio hayo yasiyo na hata chembe ya huruma[Mungu ni mwenye huruma] hawezi amuru maalbino wauae,ajali za watu kufa kama vile kuku kwa mkupuo.Ndugu mpendwa shetani ni mjanja na biblia inasema kwenye kitabu cha ufunuo kuwa anajua wakati uliobaki ni mchache..kwa hiyo anachofanya ni kuhakikisha anav
                  Ni muda mrefu sana nimekuwa nikisikia matukio mengi ya kutisha na ya  ajabu yakitokea katika jamii tunazoishi; hasahasa matukio ya ajali za barabarani, ukatili , watu kujinyonga na kunywa sumu nk.Na mara nyingi nimekuwa nikisikia watu wengi wakisema yote hayo ni mapenzi ya Mungu(yaani Mungu ndio amesababisha) na muda mwingine hata watumishi wa Mungu wengi wakati wa mazishi nimewasikia na wewe umewasikia wakisema “Bwana ametoa na Bwana ametwaa;jina la Bwana libarikiwe”
                             Kwa upande wangu nimekuwa nikipata shida kidogo juu ya misemo hii  ya mazishi, na Je ni kweli Bwana ndiye anayetwaa hao watu wote? mfano mlevi,ajali nk.Maana muda mwingine unakuta wala Mungu hahusiki hata kidogo katika matukio hayo, bali aiza mtu amejisababishia mwenyewe au kuna mkono wa shetani umehusika!.Si kwamba nasema Mungu hahusiki kwa asilimia zote,hapana!.Bali ukikuta Mungu amehusika basi mtu huyo amekuwa mgumu sana na amekuwa akiharibu kazi ya Mungu mfano,Herode[Matendo.12:22-23] au Mungu amependa kumpumzisha mtu huyo kwasababu ya umri[1Fal.1:1,1nyak.29:28 .
                            Kumbuka kuwa si mapenzi ya Mungu mtu afe katika       dhambi[Eze.18:23; 33:11], pia si mapenzi ya Mungu ufe kabla ya wakati ambao yeye amekusudia uishi hapa duniani ambao ni miaka 120[Mwanzo.6:3] kama ukiishi vizuri na Bwana hiki ni kiwango cha chini tu unaweza ukaishi zaidi ya hapo mfano ibrahimu aliishi miaka 140,Ayubu 140.Sasa kama ndio hivyo kwa nini uondoke kabla ya hapo.
                             Sio hivyo tu bali kwa wewe mtumishi wa Mungu uwepo wako hapa duniani ni wa muhimu sana,Yesu alimwomba Baba wa mbinguni ili asitutoe ulimwenguni [Yoh.17:15] , maana yake kuna kazi unatakiwa ufanye,na endapo utaonekana huifanyi na wala humzalii Mungu matunda basi ndio unakatwa[Math.3:11,7:19; Luka.13:6-9](sasa hii ni kwa ajili ya wale tu ya waliokoka).ni kweli kufa ni faida kwa mtu aliyeokoka,hilo nakubaliana nalo asilimia zote,lakini pia kuishi ni kristo na kwafaa sana kubaki kwa ajili ya kristo na ili kuendelea kuziremba taji zetu za kule mbinguni(kumbuka kuwa utalipwa kwa ajili ya kazi unayofanya hapa Duniani,utavalishwa taji,kama ukienda huko na hakuna matunda yoyote uliyomzalia Mungu basi usitarajie kitu.
                               Unajua utakuwaje?Embu fikiria unahitimu kidato cha 4/6 au chuo alafu siku hiyo wenzako wote wanapewa zawadi na kuvalishwa taji, alafu wewe peke yako tu ,ndio huna mtu wa kukuvalisha taji wala kukupa zawadi,unafikiri utajisikiaje?lazima ujisikie vibaya.Ndivyo itakavyokuwa unavyong’ang’ania kufa ukisema ni faida wakati hamna chochote ulichokifanya hapa duniani kwa ajili ya Mungu[Luka.12:47-48].
                                Ujue hii inakuhusu wewe ndugu uliyeokoka na lengo langu hapa ni kuona unabadilisha mawazo uliyonayo na maombi ambayo umekuwa ukimwomba Mungu ili akuondoe duniani.Kumbuka kuwa Mungu anakuhitaji ili uendelee kuwepo hapa duniani kwa aijli ya kazi yake[Yoh.17:15].Wewe ukifa shetani anafurahia kwa sababu upinzani unapungua.Hivyo badilisha hayo mawazo ya kutaka kuondoka(kufa) bali umwombe Mungu akuongezee siku za kuishi angalau na wewe ujitengenezee taji yako kule mbinguni[Ufunuo.2,3].
                            Sasa kwa watu ambao hawajaokoka Mungu anasema anachukia kufa kwao katika dhambi,na kwasababu hiyo basi inamanisha kuwa Mungu hahusiki katika vifo vingi vya watu wanaokufa kabla ya wakati uliokusudiwa.Na ukijaribu kuchunguza kwa undani zaidi utakuta asilmia kubwa ya ajali na vifo vinavyotokea nyakati za leo, wala Mungu hahusiki na kama anahusika naweza nikasema kuwa ni kwa asilimia chache sana( 25%) tu tena hiki ni kiwango kikubwa sana.Embu fikiria  vifo vya maalibino,watoto wachanga,vijana wadogo,Ajali za kila siku barabarani na watu kujinyonga na kunywa sumu je haya yote utasema Mungu anahusika?
                            Sasa usishtuke maana lengo la somo hili sio kukuogopesha bali somo hili lengo lake kubwa ni kufuta mawazo hasi(potofu) uliyojengewa na watu kuhusu masuala hayo na upate ufahamu mpya(chanya) ili uweze kuchukua hatua ambazo Mungu anataka wewe uzichukue ili angalau wewe uweze fikisha siku za Bwana.
                             NB:Kuna watu ambao mmekuwa na mawazo potofu,eti kwamba ukifundisha mafundisho kama haya una mtukuza shetani sana kwasababu yeye ndiye anatajwa mara nyingi.Nani kakudanganya kuwa unapomtaja mtu kwa ubaya,kwa lengo la kufichua maovu yake,ni kwamba unamsifia?.Siri ya vita vyote sikuzote ni kumsoma adui yako na kumsoma adui yako haimaanishi unamtukuza.Ndugu kama na wew ulikuwa na mawazo kama haya uyaondoe,maana hayatoki kwa Mungu bali kwa shetani ; kwa lengo la kukufanya usizijue hila zake na ili aendelee kukutawala na kutawala mji unaoishi.
                             Kanuni ya kusoma somo hili ni kwamba kabla haujaendelea na somo hili nakusihi ufanye maombi kwanza umuombe Roho mtakatifu akupe kiu ya kujifunza somo hili na nguvu ya kulitendea kazi [soma Mt.7:24-27; 13:18-23] maana somo hili lina upinzani sana.mpaka nimeweza kuliandaa somo hili ni kwa neema ya Mungu tu na kama sio neema hiyo basi sasa hivi usingekuwa na nakala hii.Hivyo anza kwa maombi,haribu na uvunje kila roho zilizotumwa na mwovu ili kukuzuia usipate kitu katika somo hili.Pia uwe na biblia yako karibu.Somo hili limegawanyika katika sehemu kuu tano (5); sehemu ya kwanza ,ya pili ,ya tatu,nne,tano na hitimisho.

                                 SEHEMU YA KWANZA:KUJITAMBUA NA KUTAMBUA
                               Somo hili limekuja wakati muafaka ambao wewe kama mtu wa Mungu unatakiwa ujitambue wewe ni nani,unapambana nanani(adui)? ;na ni nini unatakiwa kufanya katika nyakati hizi za mwisho.
                             Tunaposema kujitambua inamaanisha kuwa wewe mtu wa Mungu unatakiwa kujitambua kuwa wewe ni nani mbele za Mungu na nini unatakiwa kufanya.Na tunaposema kutambua maana yake unapaswa kujua adui yako ni nani?,na ni majira gani uliyoko?
                             Na nianze kwa kusema kwamba shida kubwa iliyoko katikati ya wana wa Mungu(waliookoka) ni kutokujua majira waliyoko na hata kama wanajua wanashindwa kutambua ninini wanachotakiwa kufanya kwenye majira hayo[Efeso.5:15-21].Wapendwa wengi nyakati za leo wamejikita zaidi kwenye kuombea masuala ya kwao na ya madhehebu ya kwao.Wamesahau kuwa nini Yesu aliwaagiza(The great commission) [Mathayo.24:14]..Kumbuka kuwa Yesu alisema kwamba ; “Basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi…na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi..”[Mathayo.28:19-20].
                             Lakini wapendwa wengi swala hili hawana mpango nalo ,badala yake wamegeuka na kuwa kama wanasiasa ambao badala ya kuwatetea  wananchi waliowachagua,wananza kutetea vyama vyao;na ndivyo walivyo watumishi na wapendwa wengi wa leo.badala ya kumtetea Yesu aliyewatuma wanaanza kutetea madhehebu ya yao.Hii yote ni kutokujitambua na kutokutambua mapenzi ya Bwana wao[Luka.12:47-48].
                               Biblia inasema katika kitabu cha [Ufunuo.12:12b].“Ole wa nchi    na bahari! kwa maana yule ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi ,akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.”Biblia inaweka wazi kuwa shetani yeye anajua majira aliyoko na anayatumia vizuri…Kanisa la leo limesahau na hata kama halijasahau basi limeacha wajibu wake na kazi ambayo Mungu alikusudia kanisa lifanye(The great commission)[Mathayo.24:14].
                             Kila kanisa(madhehebu) leo hii, limejiwekea vipao mbele vyake katika mambo yao.Lakini masuala ya Mungu wameyaweka pembeni.Kanisa la leo halina muda wa kutafuta mapenzi ya Mungu.Ukikuta mipango wanayopanga ni ya kwao binafsi na hata ukikuta mahubiri wanayoyafundisha ni ya kusengenya kanisa lingine,wakifikiri kuwa wanapatia kumbe wanakosea w.Kanisa la mitume halikuwa na tabia hizi za leo.
                              Na kwa sababu hiyo tunahitaji matenge wanasahau kuwa Yesu alisema; “……na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi..”[Mathayo.28:19-20] ikiwemo upedo[Yoh.13:34-35],kupenda jirani na Adui yako[Matthayo.5:43-48].Kanisa la leo linahitaji matengenezo(reformation) mapya kama yale aliyoyafanya mtumishi wa Mungu Martin Luther.Kanisa la leo halina umoja,halina upendo, halina unyenyekevu ,wala uvumilivu na kusamehana nk.Zaidi sana ubinafsi na kusengenyana ndio kumejaa makanisani Kwakweli kanisa linapaswa kutubu na kurudi kwenye kusudi ambalo Mungu alikusudia kanisa lifanye.
                               Sasa unaweza ukaanza kufikiria kuwa ninalalama bure hapana! Ila nakufundisha kitu ambacho kipo kwenye biblia.Wala  sio nimebuni.sasa tufuatane nikupitishe kwenye maandiko ili upate kujua nini ,Mungu alikusudia kwa ajili ya kanisa;alafu linganisha na jinsi kanisa la leo linavyoishi.Sasa tuanzie mwanzo kabisa wa nini ambacho Mungu alikuwa anakusudia kwa ajili ya kanisa:-
                               Kitabu cha [mwanzo.1:26-28] kinaonyesha mwanzo wa uumbaji wa Mungu wa kumuumba mwanadamu.Mungu anasema ″Na tufanye mtu kwa mfano wetu ;na kwa sura yetu ;wakatawale samaki wa baharini na ndege wa angani ;na wanyama ;na nchi yote pia;na kila chenye   kutambaa kitambaacho juu ya nchi……″

                       Lengo  kubwa la Mungu kuumba Dunia ni kwa ajili ya mwanadamu na ndio maana aliweka kila kitu cha kumsaidia na cha kumfaa mwanadamu katika maisha yake ;kabla hajaumbwa aliwekewa hewa –oksjeni;maji;miti;mifugo;mimea n.k.Vyote hivi ni kwa ajili ya mwanadamu.
                               Na baada ya Bwana Mungu kumuumba mwanadamu alimkabidhi utawala na umiliki wa Dunia hii.Alipewa kumiliki dunia na vyote vilivyomo ndani yake- [Mwanzo1: 27-28].“Mungu akawabarikia……na kuitiisha ;mkatawale……na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi ″.Neno ninalotaka ulione hapo kwenye mistari hiyo ni “kutiisha na kutawala dunia”
                             Wakati huohuo ndani ya Dunia pia alikuwemo shetan, kwa sababu tayari alishahasi kule mbinguni na akatupwa Duniani.soma-[Isaya.14:12-15,Eze.28:11-19].       
                       [Ufunuo. 12:10.]“………kwa maana ametupwa chini mshitaki      wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wet,u mchana na usiku ″.
                             Mungu alipomuumba mwanadamu alimpa nafasi moja ya heshima na kubwa sana –na nafasi hiyo ni ya umiliki wa Dunia hii-Na kwa ujumla hakuna malaika yeyote aliyewahi kupewa nafasi kama aliyopewa mwanadamu,hata shetani enzi za uhai wake (kule mbinguni) hakuwahi kupata nafasi kama hiyo, japo aliitamani sana na ndio maana alifanya uhasi akifikiri kuwa angepata sehemu ya kumiliki, na yeye awe kama Mungu.
                              Katika ranking(ngazi) ya ufalme wa Mungu hapa duniani, mwanadamu alipewa nafasi ya pili-yaani baada ya Mungu alifuata mwanadamu;alafu malaika na mwisho ni shetani na mapepo yake .      

                                       
KWA NAFASI ZA KAZI POPOTE TANZANIA, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
[3.00 MB]VIDEO YA ALIKIBA AKIBANDUANA NA JOKATE, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



0 coment�rios: