VITA VYA KIROHO NA KUOMBA

KUTAZAMA VIDEO YAKE BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


PICHA ZAKE ZOTE AKIWA MTUPU BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


Paulo anafundisha: ‘Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.’ (Waefeso 6:10-12).

Kwa hiyo, ndugu, tufanyaje? Tuombe dhidi ya ‘falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.’? Hapana! Hiyo siyo shauri la Paulo! Kwa kweli. HAMNA mahali mmoja katika Biblia ambapo tunasoma kwamba hata muumini mmoja katika maombi yake anaomba juu ya shetani, falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Hata Danieli hakuomba juu ya mapepo mabaya katika ulimwengu wa roho. Aliomba kwa ajili ya kazi ya Mungu na watu wa Mungu tu! (Soma Danieli 10. Yule aliyeongea na Danieli alimjulisha kuhusu vita vya pekee juu ya mkuu wa ufalme wa Uajemi na kuhusu msaada wa Mikaeli, lakini Danieli mwenyewe hakuwa ameomba juu ya mambo haya wala hakutaja mambo haya katika maombi yake!)

Kwa kweli Bwana Yesu alitoa pepo na watumishi wake wanaweza kufanya hivyo. Hiyo ni jambo lingine kabisa! Lakini hamna mstari mmoja katika Biblia unaofundisha tuombe dhidi ya ‘falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’ na hamna mfano mmoja wa muumini aliyefanya hivyo. Sasa fundisho la mtume Paulo ni nini juu ya ‘kushindana kwetu’? Anasema:

‘KWA SABABU HIYO twaeni SILAHA zote za Mungu…’ Kwa nini? Je, ili tupate kuomba dhidi ya ‘falme na mamlala? Hapana! Paulo anaendelea kueleza, ili ‘mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. Basi SIMAMENI, hali mmejifunga KWELI viunoni, na KUVAA DIRII YA HAKI kifuani,na KUFUNGIWA MIGUU utayari tupatao kwa Injili ya amani;zaidi ya yote MKIITWAA NGAO YA IMANI, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.Tena ipokeeni CHAPEO YA WOKOVU, na UPANGA WA ROHO ambao ni neno la Mungu.’ Mafundisho ya Paulo juu ya ‘vita vya kiroho’ inahusu mwenendo wetu wa kiroho, yaani, jinsi ya kusimama katika haki na imani! Kama Yakobo pia anafundisha, ‘Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.’ (Yak.4:7). Pia na kama Paulo anafundisha kwenye 2 Wakor.10:3-5, ‘Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;’ Unaona? Vita vyo kiroho kwa msingi vinahusu ‘kuangusha’ mawazo ambayo shetani anataka kuchochea moyoni mwetu yajiinuayo juu ya elimu ya Mungu! Kupinga hayo, Paulo anasema ‘silaha za vita vyetu zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome’. Silaha hizo zinazingatia, ‘ngao ya imani’ na ‘upanga wa Roho’.

Tukisimama imara kwa imani katika Bwana ndipo tunaweza kuomba. Je, tuombe dhidi ya falme na mamlaka nkd? Hapana! Paulo anafundisha kwa wazi, ‘kudumu katika kuwaombea watakatifu wote…’. Basi, anafundisha tusimame imara katika Bwana ili tuweze kuomba kwa ajili ya WATAKATIFU wote – yaani, kwa waumini wote katika Kristo – na kwa ajili ya kazi ya Mungu.

Je, ni Paulo tu anayetufundisha tuwaombeeni watakatifu wote? Hapana.

Yesu aliomba, “Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako.” Kumbe! Mzigo wa Bwana Yesu katika maombi yake ulikuwa (na unaendelea kuwa) kwa ajili ya watu wake, kwa ajili ya watakatifu! Alisema kwa wazi, “siombei ulimwenguni”. Je, Bwana Yesu aliwaombea wengine? Ndiyo. “Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao (Yoh. 17:9,20,21). Aliwaombea waumini na wao watakaoamini! Je, katika maombi yetu, tunaongozwa na Neno la Mungu, na Roho Mtakatifu?

“Kadhalika… Roho mwenyewe HUTUOMBEA kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa HUWAOMBEA WATAKATIFU kama apendavyo Mungu.” (Warumi 8:26,27).

Kumbe! Roho Mtakatifu alituongoza kuwaombea watakatifu, yaani, waumini, watu wa Mungu.

Na Yesu, kama kuhani mkuu, anaendelea kutuombea kama imeandikwa,

“…tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu…Naye,… kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili AWAOMBEE.” (Waebr.4:14; 7:25). Tena imeandikwa, “Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye ANAYETUOMBEA.” (Warumi 8:34).

Na sisi, katika maombi yetu na katika ‘vita vya kiroho’, je, tunaelekezwa kuombe kwa ajili ya nini au nani? Neno la Mungu husema kwa wazi, “kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika KUWAOMBEA WATAKATIFU WOTE.”(Waefeso 6:18).

Tunapaswa kuwaombea wataktifu wote katika Roho. Je, mtume Paulo aliomba kwa ajili ya watakatifu? Ndiyo. “Twamshukuru Mungu, Baba yake Bwana wetu Yesu Kristo, SIKU ZOTE TUKIWAOMBEA…Kwa sababu hiyo sisi nasi, … HATUACHI kufanya maombi na dua KWA AJILI YENU, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni.” (Wakol.1:3, 9).

Ni wazi tunaweza na tunapaswa kuomba kwa ajili ya mambo mengine, kwa mfano:

“Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka…” Kwa nini? Paulo anatujulisha, “tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.” (1 Tim.2:1,2).

Paulo aliwaombea ndugu zake kwa jinsi ya mwili, yaani, Wayahudi, ili waokolewe, “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.” (Warumi 10:1). Ni wazi tunaweza kuwaombea wengine ili waokolewe.

Ni vema kuomba kwa ajili ya kazi ya Mungu na kwa ajili ya watumishi Wake,

“Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu.” (2Wathes.3:1)

“Mkituombea na sisi pia, kwamba Mungu atufungulie mlango kwa lile neno lake, tuinene siri ya Kristo.” (Wakol.4:3)


Yesu anawaombea waumini. Roho Mtakatifu anawaombea waumini. Paulo aliwaombea waumini sikuzote. Na sisi tumeambiwa kuwaombea watakatifu kila wakati katika Roho. Kwa ujumla, haya ni mafundisho hasa ya Agano Jipya na yanawakilisha mzigo wa maombi ya watakatifu. Pamoja na hayo tunafundishwa kuomba kwa ajili ya kazi ya Mungu na watumishi Wake pia ili wengine waokolewe.
KWA NAFASI ZA KAZI POPOTE TANZANIA, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
[3.00 MB]VIDEO YA ALIKIBA AKIBANDUANA NA JOKATE, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



0 coment�rios: