Mungu Ni Nani?
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
![Mwanamke akisali kwa Mungu](https://assetsnffrgf-a.akamaihd.net/assets/m/1102012184/univ/art/1102012184_univ_cnt_3_md.jpg)
1. Kwa nini tumwabudu Mungu?
Mungu wa kweli ndiye Muumba wa vitu vyote. Hana mwanzo wala mwisho.
(Zaburi 90:2) Yeye ndiye Chanzo cha habari njema inayopatikana katika Biblia.
(1 Timotheo 1:11) Kwa kuwa Mungu ndiye aliyetuumba, tunapaswa kumwabudu yeye
peke yake.—Soma Ufunuo 4:11.
2. Mungu yukoje?
Hakuna mwanadamu ambaye amewahi kumwona Mungu kwa kuwa yeye ni Roho.
Mungu hana mwili wa nyama na damu kama viumbe wanaoishi hapa duniani. (Yohana
1:18; 4:24) Hata hivyo, tunaweza kutambua utu wa Mungu kupitia vitu alivyoumba.
Kwa mfano, matunda na maua ya aina mbalimbali yanafunua upendo na hekima ya
Mungu. Ukubwa wa ulimwengu unafunua nguvu za Mungu.—Soma Waroma 1:20.
Tunaweza kujifunza mengi zaidi kuhusu utu wa Mungu kwa kuisoma
Biblia. Kwa mfano, Biblia inatueleza mambo ambayo Mungu anapenda na
anayochukia, na jinsi anavyoshughulika na watu katika hali mbalimbali.—Soma
Zaburi 103:7-10.
3. Je, Mungu ana jina?
Jina la Mungu, Yehova, katika lugha mbalimbali
Yesu alisema: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.”
(Mathayo 6:9) Ingawa Mungu ana majina mengi ya cheo, ana jina moja tu.
Linatamkwa kwa njia tofauti katika kila lugha. Katika Kiswahili kwa kawaida
jina hilo linatamkwa “Yehova.” Lakini watu fulani wanalitamka “Yahweh.”—Soma
Zaburi 83:18.
Jina la Mungu limeondolewa katika Biblia nyingi na mahali pake
kuchukuliwa na majina ya cheo Bwana au Mungu.
Lakini Biblia ilipoandikwa, jina la Mungu lilipatikana mara 7,000 hivi.
Yesu alifanya jina la Mungu lijulikane alipokuwa akiwafundisha watu kuhusu
Mungu.—Soma Yohana 17:26.
4. Je, Yehova anatujali?
Baba na mama wakimhangaikia mtoto wao ambaye ni mgonjwa
Kama baba huyu mwenye upendo, Mungu anatenda kwa njia itakayotuletea
manufaa ya kudumu
Kwa kuwa tunateseka sana leo, je, hilo linamaanisha kwamba Yehova ni
Mungu asiyetujali? Watu fulani wanadai kuwa Mungu anatuacha tuteseke ili
atujaribu. Lakini hilo si kweli.—Soma Yakobo 1:13.
Mungu amempa mwanadamu uhuru wa kufanya maamuzi. Tunathamini sana
uhuru tulio nao wa kuchagua kumtumikia Mungu. (Yoshua 24:15) Hata hivyo, watu
wengi wamechagua kuwafanyia wengine mambo mabaya, ndiyo maana kuna mateso
mengi. Yehova anaumia anapoona ukosefu huo wa haki.—Soma Mwanzo 6:5, 6.
Yehova ni Mungu anayetujali. Anataka tufurahie maisha. Hivi
karibuni, ataondoa mateso na wale wanaoyasababisha. Kwa sasa, ana sababu nzuri
ya kuwaruhusu wanadamu wateseke kwa muda fulani. Tutajifunza kuhusu sababu hiyo
katika Somo la 8.—Soma 2 Petro 2:9; 3:7, 13.
5. Tunaweza jinsi gani kumkaribia Mungu?
Mwanamke akisali kwa Mungu
Yehova anatualika tumkaribie kupitia sala. Anapendezwa nasi tukiwa
mtu mmojammoja. (Zaburi 65:2; 145:18) Yuko tayari kutusamehe. Anatambua
jitihada zetu za kumpendeza, hata ingawa nyakati nyingine tunakosea. Kwa hiyo,
licha ya kutokamilika kwetu, kwa kweli tunaweza kufurahia urafiki wa karibu
pamoja na Mungu.—Soma Zaburi 103:12-14; Yakobo 4:8.
Kwa kuwa Yehova ametupa uhai, tunapaswa kumpenda kuliko
tunavyompenda mtu mwingine yeyote. (Marko 12:30) Kadiri unavyoonyesha upendo
wako kwa Mungu kwa kujifunza mengi kumhusu na kufanya yale anayotaka, ndivyo
utakavyomkaribia zaidi.—Soma 1 Timotheo 2:4; 1 Yohana 5:3.
Inayotangulia
Inayofuata
Pata Kujua Mengi Zaidi
HABARI NJEMA KUTOKA KWA MUNGU!
Je, Mungu Ana Jina?
Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile, Mweza-Yote, Muumba, na
Bwana. Lakini jina la kibinafsi la Mungu limetumiwa mara 7,000 hivi katika
Biblia.
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼
Ooh ubarikiwe sanaaaaa mtumishi wa MUNGU nimebarikiwa sana
ReplyDelete