SOMO: KUTEMBEA NA MUNGU

KUTAZAMA VIDEO YAKE BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


PICHA ZAKE ZOTE AKIWA MTUPU BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



VITU VYA KUZINGATIA UNAPOAMUA KUTEMBEA NA MUNGU

Mwanzo 5:21-24
1. Mwisho wa maisha yako ni wa muhimu sana kuliko mwanzo wako.

"Mwanzo wako ni kiashiria cha mwisho wako lakini mwisho wako hutuonesha/hudhihirisha hatima yako"

Biblia inatoa hesabu ya idadi ya siku zote alizoishi Henoko kuwa ni miaka mia tatu na sitini na mitano (365), lakini inasema katika miaka hiyo Henoko alitembea na Mungu miaka mia tatu (300). Maana yake miaka sitini na mitano (65) Henoko alikuwa akitembea kwenye njia yake mwenyewe. Biblia inaweka wazi kabisa kuwa Henoko alianza kutembea na Mungu baada ya kumzaa Methusela na utakumbuka kuwa Methusela alizaliwa Henoko akiwa na miaka sitini na mitano (65). 

”Enock alipomzaa Methusela akiwa na umri wa miaka 65 aliamua kutembea na Mungu kwa imani katika muda wa miaka 300. Hii ikiwa na maana kuwa maisha ya Enoko kabla ya kufanya uamuzi wa kukubaliana na Mungu kutembea pamoja katika kila hatua ya maisha yake, alitembea katika njia zake mwenyewe au katika mwelekeo aliodhania mwenyewe kuwa ulimfaa, ni mpaka pale alipoamua kwenda na Mungu katika mwelekeo anaotaka Mungu.

2.kutembea na Mungu kunahusisha uamuzi na utayari.

Mungu hawezi kutembea na mtu ikiwa mtu huyo hayupo tayari kutembea na Mungu. Ni kwa yule ambaye anatafuta kwa bidii kutembea na Mungu ndiye atakaye weza kutembea na Mungu. Kwa lugha rahisi naweza kusema ni mpaka utakapogundua umuhimu na uhitaji wa kutembea na Mungu kwenye maisha yako na kuchukua hatua ya kutafuta ndipo ufahamu huo utakusukuma kwenye hatua ya kuanza kutafuta kutembea na Mungu. Waebrania 11:6 Waebrania 11:6 inasema "6 Na pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu kwa maana kila mtu anayemjia ni lazima aamini kuwa yupo na kwamba yeye huwapa tuzo wale wanaomtafuta kwa bidii.

Wakristo wengi wanaona kuwa wanaweza kwenda mwendo wa maisha yao bila uwepo wa Mungu kwenye kila kitu ambacho kinazunguka maisha yao. Kutokujua au kuona umuhimu wa jambo hilo, kumesababisha wengi kwenda uelekeo wowote wanaoutaka kwenye maisha yao kwasababu kukosekana kwa Mungu kwenye hatua za maisha ya mwanadamu humfanya mtu kuwa huru kwenda uelekeo wowote lakini kuwepo kwa Mungu katika matembezi yako hukupa nidhamu inayokusaidia kwenda kwa uelekeo ambao Mungu anataka uende nae. Hii ni kwasababu "Kujua unapokwenda hukusaidia kutokwenda katika mwelekeo usiotakiwa kwenda"

3. kutembea na Mungu kunahusisha kuishi tofauti na tamaduni zilizokinyume na maadili ya ufalme wa Mungu

Kutembea na Mungu kwenye maisha yetu kunahusisha kuishi katika mila, desturi na tamaduni za ufalme wa Mungu uliekubali kutembea pamoja nae ili ikusaidie kwenda pamoja nae.Kwa lugha rahisi naweza kusema "kutembea na Mungu kunahusisha kuishi kinyume na tamaduni zilizokinyume na maadili ya ufalme wa Mungu"uliekubaliana nae kwenda pamoja katika safari yenu.
Enoko kutembea na Mungu katika wakati wake kulihitaji uamuzi mgumu na utayari wa moyo kwasababu wakati alioishi, jamii iliyomzunguka, maadili ya watu katika jamii yake yalikuwa yameharibika sana. Aliamua kuishi kwa mujibu wa kanuni na mila za ufalme wa Mbinguni ambazo zilitofautiana sana na kupingana na tamaduni za jamii aliyokuwa akiishi wakati huo.

Mungu alipoumba ulimwengu huu alikuwa amekusudia ulimwengu huu utawaliwe kwa kanuni, Mila na desturi za mbinguni. Hii ni kwasababu dunia ni ulikuwa ni mwendelezo wa kiutawala wa serikali ya mbinguni. Ni muhimu kufahamu wakati wa ukoloni kuwa ni serikali za kifalme tu ndio zilikuwa zinamiliki makoloni ambapo koloni lilihesabiwa kuwa ni mwendeleo wa eneo lakini ambalo liko mbali na serikali inayotawala koloni hilo.

4.Kutembea na Mungu kunahusisha kwenda na Mungu katika kila hatua unayopiga katika maisha yako.

Kutembea na Mungu kunahusisha makubalino katika uhusiano wako na Mungu. Amos 3:3 inasema " Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja wasipokuwa wamepatana? "
Kutembea uhusisha hatua moja kwenda nyingine na uhusisha kwenda katika uelekeo mmoja, hatua kwa hatua. Biblia haisemi kuwa Enoko na Mungu walitembea kwa miaka 30 kisha Enoko akatembea mwenyewe kisha alipofikisha miaka 80 akaanza tena kutembea na Mungu, Hapana! Mwendo wao ulikuwa ni wa kila siku kwa miaka 300.

Kutembea kwa Enoko na Mungu kulikuwa na maana hii ni kumfanya Mungu kuwa ni sehemu ya maamuzi yako, sehemu ya mawazo yako, ni sehemu ya kalenda (ratiba yako), ni sehemu ya muda wako, ni sehemu ya mahusiano yako. Kila hatua unayochukua kila siku kwenye maisha yako, Mungu anakuwa sehemu muhimu, hakuna unachokifanya bila yeye kuhusika 


5.Kutembea na Mungu kunahusisha Imani.
Enock aliweza kutembea na Mungu kwa njia ya Imani sio kwa kuona. Inawezekana labda alipata nafasi ya kusikia habari kuhusu Mungu na akaamua kuamini kuhusu Mungu huyo. Miaka 300 aliweza kuwa na uhakika na Mungu ambaye hajawahi kumuona kwa macho lakini akaamini kuhusu Mungu huyo. Katika wakati alioishi Enoko hapakuwa na Bliblia kama ilivyo kwetu leo, hata amri sheria alizotoa Mungu kupitia Musa zilikuwa bado hazijatolewa, hapakuwa na mashujaa wa imani kama akina Ibrahimu, Daniel na wengine wengi ambao tunasoma habari zao leo na zinatusaidia kuinua viwango vya imani mioyo mwetu kuhusu Mungu. 

Waebrania 11:6 inasema"
Wakati alizoishi Enoko inawezekana kutembea kwake na Mungu kwa maana ya kumshirikisha Mungu katika kila eneo la maisha yake ilionekana ni kama kupoteza muda au kuwa mshamba, lakini mwisho wa matembezi yao Mungu alimpa thawabu ya uaminifu wake katika matembezi yao ya miaka 300 kwakua haikuwa jambo rahisi.

6.Kutembea na Mungu kunahusisha mazungumzo kati yako na Mungu.
Watu wawili wanapokuwa wanatembea ni lazima mazungumzo yanajitokeza katikati yao, kila mmoja anazungumza na mwenzake na kushirikiana mawazo au mipango waliyonayo. Ndio maana Biblia inasema 1Wathesalonike5:16 inasema"Ombeni bila kukoma"

Haiwezekani kutenganisha Neno la Mungu,maombi na mtu alieamua kutembea na Mungu. Maombi na kusoma Neno la Mungu ni njia pekee ambayo hudumisha/uhimarisha mazungumzo kati yetu na Mungu. Kwa maombi unapata nafasi ya kumueleza Mungu na kwa Neno lake Mungu anazungumza na wewe. Ikiwa watu wawili wanatembea safari ndefu bila mazungumzo(conversation), huona safari yao kuwa ni ndefu, ngumu na yenye kuchosha sana, lakini wanapozungumza hujikuta safari yao imekuwa fupi Licha ya kuwa ilikuwa na uchovu mwingi, ni tofauti na mtu anaetembea Peke yake.
Hiki ndicho kitu kinachotokea mtu anapokuwa anazungumza na Mungu kwa njia ya maombi na kumsikiliza Mungu katika Neno lake katika safari ya maisha tunayoishi, kwa kadiri tatizo alilonalo mtu anavyoliona kubwa, kila wakati anapozungumza na Mungu kwa njia ya maombi, hujikuta anaona tatizo alilonalo sio zito au kubwa kama alivyokuwa akifikiri. 

7 . kutembea na Mungu kunahitaji kuwa na picha kamili ya wapi unapoelekea.

"Kujua unapokwenda hukusaidia kutokwenda katika mwelekeo usiotakiwa kwenda "
Neno la Mungu hutusaidia kufahamu zaidi kuhusu njia tunayoiendea, ni muhimu kwa mtu anaetembea na Mungu kufahamu na kuliishi neno la Mungu. Kulifahamu Neno ni jambo jingine na kuliishi neno ni hatua nyingine. Wakristo wengine wana fahamu Neno ila wameshindwa kuliishi Neno kama linavyoelekeza, hivyo inapoteza ile maana ya Kulifahamu Neno, ni sawa na mwanafunzi aliyepelekwa shule kuelimika halafu tunamleta kwenye elimu ya vitendo anashindwa ku apply ujuzi, maarifa na ufahamu alionao maana kunakuwa hakuna tofauti na ambaye hakwenda shule kujifunza ulichojifunza.

Yuda 1:14-15 inasema " Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu (mwandishi hakutaka wasomaji wachanganyikiwe maana kulikuwa na Henoko wawili katika familia ya mzee Adamu Mwanzo 4:17, hivyo mwandishi alitaka wasomaji waelewe kuwa alikuwa hazungumzi Henoko huyo mtoto wa Kaini bali nazungumzia Henoko baba yake Methusela kwasababu watu wanaweza kuwa na majina yanayofanana lakini wasiwe na tabia zinazoendana au kufanana.tofauti yao ilikuwa hivi; Henoko mtoto wa Kaini alifahamika na watu kwasababu baba yake alijenga mji na kuuita Henoko lakini Henoko huyu baba yake Methusela hakufahamika sana na watu lakini alifahamika sana na Mungu mbinguni. Swali ni unataka nani kulijua jina lako?), mwandishi wa kitabu cha Yuda anaendelea kusema Henoko huyo baba wa Methusela...alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu, ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake." 

8.Namna unavyoishi inaamua namna unavyoondoka (How you live will determine how you leave).

Paulo katika 2Timotheo 4:6-8 inasema “6Kwa maana mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. 7Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, imani nimeilinda

mungu akubariki
ukihitaji maombi
piga 0763652896, 0782859946, 0714890889

KWA NAFASI ZA KAZI POPOTE TANZANIA, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
[3.00 MB]VIDEO YA ALIKIBA AKIBANDUANA NA JOKATE, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



1 comment:

  1. Mungu akubariki sana Mtumishi wa Mungu kwa somo zuri.

    Binafsi Nimeongeza ufahamu kupitia somo hili hasa kwa habari ya Henoko

    ReplyDelete