Kwa nini tuombe?
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
Kwa mkristo,
maombi ni kama kupumua. Ni rahisi kufanya kuliko kutofanya. Tunaomba kwa ajili
ya sababu mbalimbali. Kwa sababu moja maombi ni njia ya kumtumikia mungu (luka
2:36-38) na kumtii. Tunaomba kwa sababu mungu anatuamuru kuomba (wafilipi
4:6-7). Maombi yamedhihirishwa kwetu na yesu pamoja na kanisa la kwanza (mariko
1:35; matendo ya mitume 1: 14; 3:1; 4: 23-31; 6:4; 13:1-3). Kama yesu
aliehesabu kuwa maombi ni kitu cha maana, pia nasi lazima. Kama aliitajika
kuomba ili asalie katika mapenzi ya baba yake, je tunahitajika kuomba kiazi
gani?
Sababu
nyingine ya kuomba ni kuwa mungu anataka maombi yawe njia kupata suluhisho lake
kwa hali zetu. Tunaomba tukijiandaa kufanya maamuzi muimu (luka 6:12-13);
ilitushinde vizuizi vya shetani (mathayo 17:14-21); kukusanya wafanyi kazi kwa
sababu ya mavuno ya kiroho (luka 10: 2); kupata nguvu ili tuyashinde majaribu
(mathayo 26:41); na kupata njia ya kuwatia wengine nguvu kiroho (waefeso
6:18-19).
Tunakuja kwa
mungu katika mahitaji yetu kamili, na tuko na ahadi ya mungu kwamba maombi yetu
si ya bure, hata kama hatupati chenye tunauliza (mathayo 6:6; warumi 8:26-27).
Ameahidi kuwa tunapouliza vitu ambavyo viko katika mapenzi yake, atatupa
chochote tuitizacho (1 yohana 5: 14-15). Wakati mwingine anakawisha majibu yake
kulingana na hekima yake kwa manufaa yetu. Katika hali hii tunastahili kuwa
makini na kudumu katika maombi (mathayo 7:7; luka 18:1-8). Maombi yasionekane
kama njia zetu za kumfanya mungu kutenda mapenzi yetu duniani, bali iwe ni njia
ya mungu kutenda mapenzi yake duniani. Hekima ya mungu inapita hekima yetu.
Kwa hali
ambazo hatuwezi jua mapenzi ya mungu kamili, maombi ni njia ya kutambua mapenzi
yake. Ikiwa mwanamke myunani aliyekuwa na binti aliyepagagwa na mapepo
angeponywa (mariko 7:26-30). Ikiwa kibofu nche ya yeriko angemwita kristo kwa
sauti, angebaki kibofu (luka 18: 35-43). Mungu amesema kuwa kila mara tunaenda
bila kwa sababu hatuulizi (yakobo 4:2). Kwa njia nyingine maombi ni kama
kushiriki injili na watu. Hatujui ni nani ataitikia ujumbe wa injili hadi pale
tunapoishiriki. Kwa njia hiyo hiyo, hatuwezi kuyaona matunda ya maombi
yakijibiwa hadi tuombe.
Ukusefu wa
maombi yaonyesha ukosefu wa imani na ukosefu wa imani katika neno la mungu.
Tunaomba ili tuonyeshe imani yetu kwa mungu, kuwa atatenda vile ameahidi katika
neno lake na kubariki maisha yetu utele zaidi ya vile tumeuliza na kutumainia
(waefeso 3:20). Maombi ni njia ya kuona kazi ya mungu katika maisha ya wengine.
Kwa sababu ni njia yetu ya “kujitupa ndani” ya nguvu za mungu, ni njia yetu ya
kumshinda shetani na jeshi lake ambalo hatuna nguvu za kulishinda sisi wenyewe.
Kwa hivyo mungu anatupata kila mara mbele ya kiti chake cha enzi, kwa vile tuko
nakuani mkuu mbinguni anayeweza jua yote amboyo tunayapitia (waebrania
4:15-16). Tuko na ahadi yake kuwa maombi ya mwenye haki yatatenda mengi (yakobo
5:16-18). Na mungu atukuze jina lake katika maisha yetu tunapomwamini na kukuja
kwake kila mara katika maombi.
AINA ZA
MAOMBI YA KUFUNGA
Tunapofunga
na kuomba tunayatafuta mapenzi ya mungu katika jambo fulani. Bwana yesu
alitufundisha kuomba na akasema tuombapo tuombe ya kwamba “mapenzi ya mungu
yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni” #mathayo 6:10. Kwa hyo kusudi la
kufunga na kuomba ni kuyatimiza mapenzi ya mungu hapa duniani kama huko
mbinguni! Kuyatimiza mapenzi katika hayo tunayoutafuta uso wa mungu.
Kufunga na
kuomba hakumfanyi mungu ayabadilishe mapenzi yake. Hatufungi kuwaonyesha
wanadamu ya kwamba sisi ni wa kiroho sana. Kwamba labda twamjua mungu sana.
Hapana. Tunayatafuta mapenzi ya mungu maishani mwetu. Haijalishi umeokoka miaka
mingi ilopita au hivi karibuni.
Tukumbuke
maneno ambayo mungu aliyasema ktk 2nyak 7:14 “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa
jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia
zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya
nchi yao”
kwa kufunga
na kuomba tunamruhusu roho mtakatifu azihuishe nafsi zetu na kutufanya tuweze
kusikia sauti ya mungu na kumtii katika maisha yetu.
KWA UJUMLA
TUNAFUNGA ILI:
• kuna watu
wanafunga kwa sababu za kimwili kabisa. Kwamba miili yao imefika wakati inawapa
shida. Matamanio ya mwili yameshindwa kuwasiliana vizuri na roho. Kuna nyakati
tamaa za mwili zinakuwa kubwa na hivyo kwa kufunga na kuomba waweza kuutiisha
mwili huu. Kwa vijana hasa, vyakula na vinywaji tunavyokula vinaleta shida
wakati mwingine ndani ya mwili. Kwa kufunga unautiisha mwili na kuzinyamazisha
tamaa hizo. Wengine wanafunga kwa ajili ya kuyatiisha mawazo. Bwana yesu
akasema mawazo ndiyo yamtiayo mtu unajisi. Kabla mtu hajafanya uasi fulani
huanza kujichafua katika mawazo yake. Ndani ya mawazo yake ataua, atamtukana mtu,
atazini, ataiba yani atafanya kila lililo baya kabla hajalifanya katika
ulimwengu wa kimwili. Rafiki yangu mmoja akasema ikiwa mwanadamu anaweza
kupangilia mipango mbali mbali miovu hadi akaitimiza kwa nn asiweze kufanya
hivyo hivyo kwa ajili ya mungu? Kwa hyo wakati mwingine mtu anafunga kuyatiisha
mawazo machafu ndani yake. Mawazo machafu hututia unajisi! Ndo maana mtume
paulo akasema “basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase
nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika
kumcha mungu” 2kor 7:1
• lakini
kiroho tunafunga ili kuweka mahusiano yetu na mungu vizuri rohoni. Ezra 8:21-23
“ndipo
nikaamuru kufunga, hapo penye mto ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za
mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa
ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote.
AINA YA
MIFUNGO:
1. MFUNGO
KAMILI
katika
mfungo huu hakuna kula kabisa chakula kigumu bali waweza kunywa maji au
kimiminika chochote cha kukusupport.
Siku ngapi
waweza kufunga mfungo wa aina hii unategemea na neema na malengo yako katika
mfungo huo. Wengine huenda siku moja, mbili, tatu, wiki, n.k n.k
2. MFUNGO
NUSU
mfungo nusu
huanzia saa 12 asbh hadi saa 9 mchana au kuanzia jua linapoibuka hadi
linapozama. Mfungo ambao madhehebu mengine wamewazoeza waumini wao kuufanya.
Wengine wameweza kuufanya kila ijumaa. Madhehebu ambayo yamewazoesha watu wao
kufunga angalau kila wiki mara moja wameweza kuwa na mafanikio makubwa sana
katika kuzifungua nira na vifungo mbali mbali
3. MFUNGO WA
DANIEL
daniel
alifunga mifungo miwili ya aina yake;
• katika
sura ya i daniel alifunga alikula mboga mboga tu (yaweza kuwa alikula mboga
mboga na juisi fulani fulani)
• katika
sura ya 10 daniel alifunga kwa siku 21 kwa kutokula chakula kitamu, wala nyama
wala divai haikuingia kinywani mwake”
MAOMBI
KWAAJILI YA WAGONJWA.
Bwana yesu
ninakushukuru kwaajili ya majira na muda huu ambao umenipa kibali kwaajili ya
kuombea wagonjwa. Nakushukuru sana mungu wetu kwani wewe ni mwuumbaji wetu.
Mungu ulituumba kwa mfano wako na kwa sura yako. Nakushukuru mungu. Asante kwa
mamlaka ambayo umetupati wanao kwa damu yako takatifu iliyomwagika msalabani.
Asante kwani ulisema tutaweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya. Asante
mungu kwani wewe si mwanadamu hata useme uongo.nakuja kwako muda huu kwa
unyenyekevu mkuu nikiomba toba kwaajili ya wagonjwa wote. Natubu kwaajili yao
bila kujali kuwa magonjwa waliyonayo ni matokeo ya dhambi ipi. Haijalishi iwe
ni matokeo ya zinaa,kukiuka kanuni za uumbaji,uchafu,uchawi,uganga au
ushirikina natubu mungu wangu. Najua wewe ni mungu wa rehema naam utatusamehe.
Natubu kwakutokuamini kwetu naomba utusamehe mungu wetu. Umesema nami ktk neno
lako la zaburi 103:3 kuwa akusamehe maovu yako yote,akuponye magonjwa yako
yote.ndivyo hivyo mungu leo tenda kwa wagonjwa wote. Haijalishi ni ugonjwa gani
mtumishi wako anasumbuliw,haijalishi taarifa ya daktari inasemaje juu ya
ugonjwa wake,haijalishi wauguzi wake wamemtishaje na wala haisumbui kuwa dawa
zake hazipo duniani kote lakini ninachojua kuwa upo wewe yesu usiyeshindwa
jambo. Ktk jina la yesu kristo naachilia uponyaji wa mama yule,baba yule,kijana
yule,mtoto yule na wana wa kike kwa wa kiume.pokea uponyaji ktk jina la yesu
kristo. Naharibu makao yote ya shetani ndani yako ktk jina la yesu. Nang'oa
kila pando lisilotokana na mungu ndani yako sasa ktk jina la yesu kristo.
Nafuta maneno yote machafu yaliyosemwa kinyume nawe naam napanda maneno ya
kristo ndani yako sasa. Sikia hii ripor ya daktari imesema una ukimwi nami kwa
mamlaka ya yesu kristo naifuta riport hiyo naninatangaza riport ya yesu kuwa
huna ukimwi tena ktk jina la yesu kristo. Daktari kakuandikia kuwa poor
prognosis yaani unakufa nami leo nakuandikia ktk jina la yesu kuwa huta kufa
bali utaishi na utasimulia ukuu wa mungu. Ktk jina la yesu natangaza uponyaji
kwa kila mgonjwa au ndugu wa mgonjwa aliyesoma sala hii kwa imani. Umekuwa
mzima ktk jina la yesu kristo mwana wa mungu. Amina..
Kama una
mgonjwa hajiwezi au yupo mbali nawe basi soma sala hii kwa imani kisha
ukimaliza mpigie mwambie anywe au anyweshwe maji kidogo kwenye glass na mara
atapokea uponyaji ktk jina la yesu. Na wale wenye virusi vya ukimwi baada ya
sala hii wakae siku saba alafu wakapime virusi naam wataona mungu atakavyo
washangaza. Mrudishie mungu sifa na utukufu kwani yeye ndiye afanyaye
NAMNA YA
KUMWITA,KWENDA NA KUMUOMBA MUNGU ILI AKUSIKILIZE.
.yeremia
29:12 “nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza”.
Watu wengi
wamekuwa wakitamani maombi wanayoyapeleka mbele za mungu kusikilizwa.watu
wanaomba kila aina ya maombi inayowezakana maadam mungu asikie na kuwaokoa
kutoka kwenye shida waliyonayo au kuwapa haja za mioyo sawasawa na uhitaji wao.
Wapo
wanaoomba na wanaona majibu yao yanajibiwa lakini pia lipo kundi jingine kubwa
ambalo wanaona kama vile mungu amenyamaza,amewaacha,hawasikii, au wanajiona
kama vile mungu amewakataa na kuziona ahadi za mungu kwamba si za kweli na
mbaya zaidi wengine wamefika mahali pa kumwacha mungu kwa sababu ya kushindwa
kuvumilia majibu kutoka kwa mungu na hivyo kutafuta njia mbadala za kutatua
matatizo yao.wapo walioomba kuhusu watoto,ndoa zao,afya
zao,ajira,biashara,elimu zao nk. Walipoona katika fahamu zao mungu hajibu basi
wakaamua kwenda kwa waganga wa kienyeji,wachawi na kwa miungu mingine kutafuta
msaada huko.
Sasa ili
mungu aweze kusikiliza au kujibu maombi yako huenda kuna mambo mengi ya msingi
ambayo mwombaji anapaswa kuyajua na kuyatendea kazi.sasa baada ya kuona maombi
mengi ninayoomba na pia ambayo wana wa mungu pia wanaomba hayajibiwi ili
nilazimu nimuombe mungu anifundishe vizuri kuhusu hili neno.
Hivyo hayo
ninayoenda kukushirikisha ni sehemu ya yale ambayo mungu amekua akifundisha
naamini na wewe yatakusaidia maana nimeona yakinisaidia binafsi pamoja na wale
ambao mungu amenipa kuwafundisha kwa njia nyingine.
Lengo la
ujumbe huu ni kukupa maarifa yatakayokusaidia kuomba maombi ambayo wewe
mwenyewe.pindi unapoomba utakua na uhakika mungu anakusikiliza kwa wakati huo.zaidi ujumbe huu umekusudia kukufundisha
namna unavyoweza ukapeleka maombi mbele za mungu.
Siku moja
nikiwa chuoni mwaka wa kwanza majira ya tisa jioni,nilikua nikipandisha ngazi
kuelekea chumbani kwangu ambacho kilikua ghorofa ya tatu juu kabisa.wakati
naanza kupandisha zile ngazi nikasikia mtu ananiuliza ndani yangu je hivi mungu
huwa anaitwaje?anaendwaje?anatafutajwe?anakaribiwaje? Nilipofika chumbani
nikaanza kutafakari haya maswali na baadae ndipo nikapata hii mistari katika
yeremia 29:12-13 inayosema “nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami
nitawasikiliza. nanyi mtanifuata na kuniona,mtakaponifuata kwa moyo wenu
wote.”Baada ya kuisoma vizuri ndio nikagundua karibu maswali yale yote yalitoka
hapa.
Mungu
anasema nanyi mtaniita, sasa na mimi nikuulize swali, hivi umeshawahi kujiuliza
mungu tunamwitajemwitaje? Tunamwendeaje? Na tunamtafutaje. Usiishie kusema
mungu ameseam nikaribieni nami nitawakaribia, umneshawahi kujiuliza anaposema
tumkaribie yeye yuko wapi? Na pia tunamkaribia kwa namna gani? Sasa hayo ndio
maswali yaliokuwa yakinijia.
Picha ambayo
mungu alitaka niipate kwenye zile ngazi ni hii, nifikirie kwamba kile chumba
kule juu ndiko aliko yeye yaani mbinguni. Sasa baada ya kufikiria hivyo ndio
niwaze na nijiulize amesema nimuite nimwendee nimtafute n.k sasa hivi ndio
ninamwitaje, ninamwendeaje na ninamtafutaje? Nilipozidi kutafakari hiyo mistari
roho mtakatifu akanifundisha yafuatayo:
Kwanza
alinionyesha makosa matatu ambayo watoto wake mara nyingi tumekuwa tukiyafanya
wakati wa maombi. Na ningependa na wewe uyajue kwa maana itakusaidia ili bado
unayafanya basi usiyafanye tena.
KOSA LA
KWANZA, KUOMBA KINYUME AU NJE YA MAPENZI YA MUNGU.
1 yohana
5:14 inasema na huu ndio ujasiri tulionao kwake ,ya kuwa,tukiomba kitu sawa na
mapenzi yake atusikia” moja ya tafsiri za kiingereza inasema “we are certain
that god will hear our prayers when we ask for what pleases him” kosa kubwa
ambalo tumekuwa tukilifanya mara nyingi ni kuomba vitu au mambo ambayo ni
kinyume na mapenzi ya mungu.
Anaposema
sawasawa na mapenzi ya mungu maana yake ni lazima ujue kwanza nini ni mtazamo
au mawazo ya mungu juu ya hilo unalotaka kuliombea.maombi ni kuzungumza au
kusemezana na mungu kwa kumwambia yale ambayo amesema kwenye neno lake kuhusu
haja zako wewe.
Kwa lugha
nyingine usiombe kitu ambacho hujui nini mawazo ya mungu juu ya hicho kitu.
Mawazo ya mungu juu ya kila haja ujyonayo yako ndani ya neno lake .hivyo ni
lazima neno la mungu likae kwa wingi ndani yako ili unapoomba uombe kulingana
na ahadi zake na pia sawa na kile alichokisema.
Zaidi pia
wengi wanapotaka kuomba huenda kuhusu ndoa,kanisa,ajira,watoto ,biashara nk
huwa wanomba kimazaoea. Maana yake ni hii wengi wamezoea ninpoombea ndoa
nitaombea amani,upendo ,furaha nk sasa sina maana hayo maombi hayafai ila
ninachotaka ukipate ni hiki hoja unazozipeleka mbinguni hakikisha umefunuliwa
na mungu mwenyewe.maana yake mungu ndiye akupe mambo ya kuombea kuhusu nchi
,ndoa,biashara yako nk.
KOSA LA
PILI:, KUKOSA UTULIVU NA USKIVU WA ROHONI WAKATI WA MAOMBI NA BAADA YA MAOMBI.
Sikiliza
mungu anayo mambo mengi ya kukuambia wewe kuliko yaje wewe uliyonayo wewe
kumweleza yeye. Chungu hakiwezi kumwambia mfinyanzi kwamba ulinumba kwa kazi
hii tu, bali mfmyazi ndiye mwenye mengi kuhusu kile chungu.
Ndio maana
yesu anasema si ninyi mlionichagua mimi bali ni mimi niliyewachagua njnyi
(yohana 15:16),sasa watu wengi sana wana bidii nzuri ya maombi wanaweza wakakaa
hata masaa matatu mfululizo na hata zaidi wanamuomba mungu tu.
Katika mda
huu wote wao ndio wanaojieleza na mara wanapomaliza ni kusema ameni na
kuondoka.hii ni picha ya mtoto anayekuja kwako kama mzazi anasema baba/mama naomba
hela ya daftari, nauli na ya kula shuleni, pia naomba uninunulie suruali nk.
Sasa kabla wewe hujamjibu yeye ameshafungua mlango na kuondoka.sasa kibiblia
ndiko kunaitwa kukosa utulivu na usikivu wa rohoni mbele za mungu.
Mara zote
unapoomba jifunze kuwa na wakati wa kutulia kusikiliza mungu naye anasema
nini.kwenye utulivu ndiko mungu anakosema sio kwenye kelele maana anjua hamwezi
kusikilizana.soma isamwel 3:1-10 utaelewa ninachokisema hapa.mungu alisema na
samweli alipotulia.
KOSA LA
TATU, KUMUOMBA MUNGU WAKATI TAYARI UMESHAJITAFUTIAJIBU LA SHIDA ULIYO NAYO.
Hili ni kosa
jingine kubwa ambalo wana wa mungu wamekuwa wakilifanya. Wengi wana mahitaji
mbalimbali.wapo watu wengi ambao kweli wanaomba kwa kumaanisha mbele za mungu
na wengine hata kufunga kwa masaa mengi lakini tatizo lao katika fahamu zao
wameshafanya uamuzi wa nini watafanya baada ya maombi yao.sasa hata mungu
akikushirikisha mawazo yake si rahisi ukamwelewa kwa sababu tayari kwenye nafsi
na ufahamu wako kuna jibu na biblia inasema aonavyo mtu katika nafsi yake
ndivyo alivyo.
Sambamba na
hilo, kosa linalofanana na hili ni wale watu wanaomwomba mungu afanye kama vile
wao waonavyo kataka nafsi zao. Yaani wanamtaka mungu akubaliane na mawazo yao
na njia zao juu ya shida au haja walizo nazo wao wenyewe.
Na jambo
hili tunalielewa vizuri tunaposoma katika kitabu cha luka 9:12 -17 .habari za
wanafunzi wa yesu pindi njaa ilipokuwa ikiwauma watu wakati yesu anaendelea na
mkutano. Wao walimwambia bwana waage watu wakajijinunulie chakula vijijini na
mashambani, wao walidhani hili ndilo jibu la njaa ya watu. Hawakufikiri kwamba
sio wote wenye pesa za kununua chakula, kuwaaga watu kungemaanisha yesu aache
kufundisha nk. Sasa jibu la njaa ya wale watu halikuwa kama wanafunzi
walivyowaza na walivyotaka bali jibu lilikuwa kwa yesu kufanya muujiza wa
kubariki mikate mitano na samaki wawili vitosheleze watu wote 5000.
Sasa baada
ya kuwa tumeona hayo makosa makubwa matatu tuangalie mungu anaposema nanyi
mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza ana maana gani?.
Katika
mstari huu kuna mambo makubwa matatu yamezungumziwa.
MOJA NI
MTANIITA,MBIII MTAKWENDA NA KUNIOMBA, TATU NI NAMI NITAWASIKILIZA.
JAMBO LA
KWANZA NI ,MTANIITA.
Ukisoma
kitabu cha yeremia 33:3 anasema “niite,nami nitakuitikia ,nami nitakuonyesha mambo
makubwa,magumu usiyoyajua. Mungu ansema utakapomwita yeye atafanya mambo
mawili.moja atakuitikia na mbili atakuoyesha mambo makubwa,magumu usiyoyajua.
Maana yake
ni hii, kukuonyesha mambo makubwa,magumu usiyoyajua ni kukufunulia mambo ambayo
ulikuwa huyajui katika lile ulilomuita.hivyo basi kumuita mungu ni kumuomba au
kumtaka mungu akufunulie mambo makubwa na magumu usiyoyajua kuhusu shida au
hitaji au haja uliyonayo mbele zake.mfano unamuita mungu akufunulie ndoa yako
jinsi ilivyo, nini kinaendelea usichokijua, nini ukiombee, nini hakijakaa
sawasawa kwenye hiyo ndoa k.
hivyo basi unapotaka kuomba juu ya jambo
lolote lile ni vizuri kwanza ukamuita mungu juu ya hilo jambo.maana yake muombe
mungu akupe picha kamili ya hilo unalotaka kuliombea,akufunulie jinsi lilivyo
ili ujue uanzie wapi kuomba.,kama ni ndoa,nchi,mke au mme mtarajiwa,huduma yako
nk.
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼


0 coment�rios: