MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 5)
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
Mambo ya
kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu tunapokuwa katika maombi.
(1)
hatupaswi kuwa na mashaka yoyote!
Maandiko
yanasema katika yakobo 1:5-7,
“…ila naombe
kwa imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye mashaka ni kama wimbi la bahari la
bahari lililochukuliwa na upepo,na kuleperushwa huku na huku. Maana mtu kama
yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa bwana.”
Hayo ndiyo
maandiko! Hata kama tunaomba masaa 100 mfululizo, hata kama tunaomba kwa
viwango vya vinavyoonekana vya juu sanaa kibinadamu, lazima maombi yetu yawe
ndani ya kanuni, lazima tuombe pasipokuwa na mashaka tena mashaka yoyote! Hayo
ndio maandiko hakuna njia ya mkato; kama tunamuomba mungu lakini tuna mashaka
moyoni au vinywani hilo ni tatizo linalopelekea kutopokea majibu yetu ya
maombi! Kwa nini nasema mtu anaweza akawa na mashaka moyoni. Mtu mwingine
anaweza akaonekana ana imani katika mazungumzo yake, hasa pale anapokutana na
watu , lakini ndani ya moyo wake kumejaa mashaka, na mashaka hayo mungu huyaona
pale mtu anapokuwa peke yake katika fikra au pale mambo yanapokwenda kinyume na
alivyotarajia kutokana na maombi yake! Akizungumza na watu ni kama amejaa
imani! Lakini moyoni kumejaa mashaka makubwa! Mashaka ni ile hali ya wasiwasi
ya kutokuamini. “hivi kweli mungu inawezekana kweli? Itakuwa kweli? Mungu
ananisikia kweli?” N.k.
Hayo yote ni
mashaka na kwa mashaka hayo kamwe hatutaweza kupokea majibu yetu ya maombi!
Kamwe! Tukiruhusu mashaka hata kama ni kidogo tunaambiwa waziwazi, “maana mtu
kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kutoka kwa bwana.” Yaani, hata ile
kudhani, kutegemea, kufikiri, isiwepo. Mashaka ni adui mkubwa sana
anayeshindana na majibu ya maombi yetu yasitufikie.
Wakati
mwingine mashaka yanakuwepo baada ya kuomba kitu muda mrefu na kutoona majibu
ya maombi! Wakati mwingine inatokana na kuona mambo yanakuwa mabaya zaidi
kuliko mwanzo! Au uzito wa jambo pia linaweza kuchangia kukaribisha mashaka na
hata shetani pia anahusika lakini anapitia maeneo hayo hayo!
Ili tuone
majibu ya maombi yetu yakiwa dhahiri, hatupaswi kuruhusu mashaka yoyote hata
kidogo! Tukishaomba tu! Mawazo yetu yanapaswa kufikiri sawasawa na majibu ya
maombi yetu, kusema kwetu kuendana na majibu yetu ya maombi kwa imani, inaweza
kuwa sio rahisi kuishi hivyo haiwezi kuwa rahisi hata kidogo! Na hakuna mbadala
wake lazima mashaka yasiwepo ili tupokee majibu yetu ya maombi! Tunamuomba
mungu kwa sababu sisi hatuwezi, tumeshindwa ndio maana tunaomba! Kama mtu
unawashwa mgongoni utamwomba mungu “niwezeshe kujikuna?” La! Tutajikuna kwa
sababu jambo hilo liko ndani ya uwezo wetu!
Tunapomuomba
mungu maana yake sisi hatuwezi, tumeshindwa! Rahisi kufikiri nguvu za mungu
hazipo; rahisi kufikiri ukimwomba mungu basi majibu yanachukua muda mrefu!
Hatupaswi kuyaruhusu mawazo hayo kufanya kazi ndani yetu kamwe! Sisi
tunachotakiwa kuamini mungu yupo na anajibu maombi na hakuna gumu la kumshinda!
Mashaka yanapokuwa yanakuja kwa njia zozote zile, iwe kupitia watu kwa maneno
yao; n.k. Hatupaswi kuyaruhusu kwa sababu, tukiruhusu mashaka maandiko yanasema
tusitarajie kupokea kitu kutoka kwa bwana!
Kuna wakati
yesu alikuwa anatembea juu ya bahari! Na petro akaomba atembee au apewe uwezo
na yesu wa kutembea juu ya bahari! Yesu akayajibu maombi yake na akamwambia
petro atembee…lakini petro aliporuhusu mashaka baada ya kuuona upepo, akazama
mbele ya yesu! Yesu akamuokoa kwa kumshika mkono sio kwa kumuombea bali
alimshika mkono na akamwambia! (mathayo 14:26-31.31):
“mara yesu
akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, ‘ewe mwenye imani haba, mbona
uliona shaka?’”
Unaona hapa!
Petro anazama mbele ya yesu kwa sababu aliruhusu mashaka, na sisi sio kama
tukimuomba mungu kitu fulani basi kinakuwa mtelemko! Inaweza ikatokea upepo
mkali kwenye biashara zetu kwa viwango vya kuporomosha kabisa mitaji yetu! N.k.
hatutakiwi kuwa na mashaka katika hali yoyote! Tusimamie matokeo tusiangalie
mazingira tuliyonayo kwa sasa, tukiwa na mashaka tutazama tu hata kama yesu
yupo ndani mwetu!
Wakati wote
tunapomuomba mungu, tuombe bila mashaka yoyote yale! Mungu yupo na nguvu zake
zipo vilevile! Hata mimi nikikufanyia maombi na ukaanza kuona matokeo, yaani,
unatembea juu ya bahari kama petro! Lolote likitokea kama upepo likiwa na lengo
la kubadilisha hilo, hupaswi kuwa na mashaka unapaswa kuendelea kuamini! La
sivyo utazama kama petro na kuupoteza muujiza wako! Kama petro alizama mbele ya
yesu kwa sababu ya kuruhusu mashaka! Sembuse mwanadamu anayeitwa….. .
Yakobo
1:5-6,
“…ila naombe
kwa imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye mashaka ni kama wimbi la bahari la
bahari lililochukuliwa na upepo, na kuleperushwa huku na huku. Maana mtu kama
yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa bwana.”
Tumwombe
mungu atuongezee imani atupilie mbali mashaka yaliyomo ndani mwetu na atupe
kuyashinda kila yanapoinuka. Hata kama maombi yetu yatachukua muda mrefu bila
kuona majibu yake, bado hatupaswi kuruhusu mashaka, tena mashaka yoyote yale.
MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO ( 6)
Mambo ya
kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu, tunapokuwa katika maombi.
(2) kuomba
vibaya ili tuvitumie kwa tamaa zetu!
Tunaweza
tukawa kweli tunaomba, tunaomba ili tupate kazi fulani, tunaomba mungu atutumie
tukiombea watu wapone na mungu akutane na haja zao! Mwingine anaomba apate
nyumba nzuri, mwingine gari, honda, n.k. Yote haya ni mema, lakini kama mtu
anaomba moyoni kumejaa nia nyingine (kama uchoyo au kiburi), moyoni anasema au
anawaza kwamba, “nikipata gari ninalolitaka, watu watanikoma.” “nikipata pesa
hee! Watanitambua”, n.k.
Mwingine ni
kipofu tangu kuzaliwa anamuomba mungu lakini moyoni anawaza au anasema,
“sijawahi kuona mwanamke tangu kuzaliwa kwangu, nikiona sijui itakuwaje
watanikoma, maana naishia kusikia tu na kuhisi” unaona! Mtu anaomba lakini
moyoni mwake anawaza nikikipata nitakutumia hivi au vile, matumzi yenyewe ni
nje ya mpango wa mungu. Ndugu yangu hapo tutaomba na kuombewa lakini kamwe
hatuwezi kupokea majibu ya maombi! Tunataka mtoto lakini hatujaoa/hatujaolewa
wala hatutaki kusikia habari za kuoa au kuolewa!
Mwingine
anataka mungu amtumie lakini moyoni mwake kumejaa mashindano ya dhahiri,
anawaza kumzidi yule, mwingine anataka sifa tu! Mwingine anawaza utajiri kwamba
nitakuwa napata sadaka nyingi za watu n.k. Maandiko yanasema katika yakobo 4:3,
“hata
mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.”
Unaona
maandiko hayo? Kama tunamuomba mungu tukiwa na hali hiyo! Kamwe hatuwezi
kupokea majibu ya maombi. Ni kupoteza muda tu! Na mwisho wa siku tunaona kama
mungu hayupo; mungu yupo na anajibu maombi! Tatizo lipo kwetu tu! Tunaomba ili
tukipata tuvitumie vibaya! Kama tunataka kumuona mungu lazima tuzingatie
tunaomba ili tuvitumiaje? Nje ya mpango wa mungu! Tuko watu wengi tunaomba na
kufikia wakati tunafunga! Lakini tunaomba ili tuvitumiaje hivyo tunavyovitaka
kwa njia ipi?
“hata
mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.”
Yakobo 4:3.
Kuomba
tunaomba kweli! Lakini hatupati kwa sababu tunaomba vibaya ili tuvitumie kwa
tamaa zetu! Tangu wakati huu tuhakikishe nia zetu zinakuwa safi mbele za mungu
ili tuyaone majibu yetu ya maombi na nguvu ya maombi! Maombi yana kanuni zake
na ikiwa mtu anataka kumuomba mungu na kumuona mungu dhahiri akijidhihirisha
kwake binafsi hatuna budi kuzingatia yote tunayopaswa kuyazingatia.
Lolote
tunaloliomba lazima tangu moyoni huko ambako mungu anaanza nako kwa kumuangalia
mtu anataka hili ili iwe nini? Mwingine anatumia pesa kunyanyasa watu, mungu
huwa hamuinui mtu ambaye ana visasi, yaani mungu akinipa hivi fulani atanikoma!
Kila anachofanya mungu ni kwa utukufu wake tu sio kwa utukufu wa mtu yeyote.
MAISHA YA
MAOMBI KWA MKRISTO (7)
Mambo ya
kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu, tunapokuwa katika maombi.
(3)
hatupaswi kukata tamaa na kuachia maombi njiani baada ya kuona tunaomba muda
mrefu bila kuyaona majibu yetu ya maombi kwa dhahiri!
Hakuna
sehemu ngumu inayotushinda watu wengi kama hii! Watu wengi tunataka tukishaomba
tu; basi tupokee majibu yetu ya maombi muda huo huo! Mungu hafanyi kazi hivyo
ndugu yangu! Mungu ni wa utaratibu sana! Tunapomuomba mungu tunatakiwa kuamini
kwamba imekuwa. (matha 7:7).
Hilo ndilo
la kuliamini na kulishikilia wakati wote, haijalishi majibu yetu ya maombi
tutayaona lini, sisi tuamini kwamba mungu ametenda huku tunaendele kumwomba
mungu mpaka liwe dhahiri lile tunaloliomba. Mungu aliumba mbingu na nchi kwa
muda wa siku 6, (mwa 1:1). Unafikiri kwa uwezo wa mungu! Kwa nini hakutumia
siku moja tu kufanya kila kitu? Je! Hakuwa na uwezo huo? Uwezo upo mkubwa tena
sana – mungu ni wa utaratibu sana, ana nguvu ana uwezo lakini ni wa utaratibu
mno! Mnoooo! Mbona basi wewe na mimi tunakata tamaa mapema hivyo na kuacha
kuendelea kuomba! Tunaona mungu hatusikii ni kama anawasikia wengine! Ni kama
ana watu wake maalumu na sio sisi? Hatupaswi kuwaza hivyo hata kidogo, na
tusiyape nafasi mawazo hayo! Tunapaswa kuendelea kung’ang’ania mbele za bwana
mpaka tuone majibu yetu ya maombi yawe dhahiri. Maandiko yanasema katika luka
18:1,
“akaawambia
mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba mungu sikuzote, wala wasikate tamaa”.
Hayo ni
maandiko! Mungu anatambua kwamba! Mtu anaweza akaomba jambo na likachukua muda
mrefu na mpaka mtu anafikia mahali kukata tamaa na kuacha kuomba, ndio maana
inatajwa hapo “wala wasikate tamaa”.
Uwezekano wa
kuchelewa kuyaona majibu yetu ya maombi unawekwa wazi na bwana mwenyewe, lakini
hatupaswi kukata tamaa! Marufuku kukata tamaa, usikate tamaa! Endelea kuomba,
usiachie njiani hata kidogo! Usiwaze “ooh! Labda kuna makosa nimeyafanya, labda
nimefanya dhambi.” Kwani ukifanya dhambi hujui? Maandiko yanasema! 1 petro 5:6,
“basi nyenyekeeni chini ya mkono wa mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati
wake”. Kumbe kuna wakati wa mungu! Wakati wa mungu ni mzuri ndugu kuliko wakati
wetu sisi! Mungu ndio anajua wakati mzuri wa kukupa jibu lako la maombi! Usione
unakawia, wakati wako ndio unakawia, lakini wakati wa mungu ni bora saaana!
Mungu anajua wakati gani ukipata kazi utakuwa mzuri kuliko wakati fulani; mungu
ndio anajua wakati gani ukipata mtoto utakuwa mzuri zaidi! Wewe unataka mtoto
sasa lakini mungu akiangalia anona sasa sio salama! Unataka mungu akutumie
kwenye hili au lile n.k. Sisi tuendelee kumlilia bwana! Kupokea ni lazima! Kukata
tamaa ni marufuku! Hatupaswi kukata tamaa kamwe! Tuyashinde mawazo ya
kutukatisha tamaa! Mungu yupo na anajibu maombi.
MAISHA YA MAOMBI KWA MAOMBI KWA MKRISTO (PART
8)
Mambo ya
kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu,tunapokuwa katika maombi.
(4) Tunapaswa
kuwa na imani kwamba mungu yupo na anatusikia na anajibu maombi!
Ndugu yangu,
hata kama tutaomba na kujigalagaza na kulia kwa uchungu mpaka kutoka makamasi!
Lakini kama hatuna imani ni buuure, bure!
IMANI NI
NINI? Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana na mambo
yasiyoonekana, waebrania 11:11. Hiyo ndio imani! Tunaomba tunatarajia kupokea,
sasa imani ni kuwa na uhakika kwamba! Hiki ninachikiomba kinakwenda kuwa
sawasawa na nilivyoomba! Imani huwa haingalii mtu wala huwa haijilinganishi na
mtu yeyote! Imani inaangalia uwezo wa mungu tu na neno lake basi! Imani
haingalii mazingira n.k. Imani inaweza kukufanya wewe kuwa wa kwanza kukipata
hicho unachokiomba! Maandiko yanasema,
“lakini
pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye mungu lazima
aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” (waebrania
11:6).
Tunatakiwa
kuwa hivyo tunapokuwa tunamuomba mungu, tusiombe ili mradi tu, tusiombe ili
kutimiza wajibu tu, tusiombe kwa desturi na mazoea! Kwa kufanya hivyo
tutadangayika kwamba hakuna nguvu yeyote katika maombi, kumbe ni uongo wa
ibilisi tu. Tunapaswa kumuamini mungu tunapokuwa tunaomba! Na imani pasipo
matendo imekufa! Baada ya maombi lazima uonyeshe matendo na sio unalala tu na
kupigapiga soga na watu! Lazima ufanye matendo kama ni kazi tafuta kazi n.k.
Kutokuwa na
imani ni dhambi vilevile! Ndugu yangu inawezekana umekuwa una muomba mungu kwa
muda mrefu lakini huna imani! Yesu alikutana na vipofu,angalia hapa! “yesu
alipokuwa akipita kutoka huko,vipofu wawili wakimfuata wakipaza sauti. Yesu
akawaambia, ‘mnaamini kwamba naweza kufanya hili?’ wakamwambia, ‘naam bwana.’
ndipo alipowagusa macho yao yakafumbuka.” Mathayo 9:27-30.
Unaona hapo?
Baada ya kusema wanaamini ndipo yesu alipowajibu majibu yao kwa kuwafumbua
macho yao! Na hakuwafumbua macho kabla ya kujibu kwamba anaweza! Kabla ya
kuionyesha imani yao! Na sisi mungu anatuuliza kila tunapomuomba! Je! Tunaamini
kwamba anaweza kufanya hilo au hayo tunayomuomba? Kila tunapoomba swali
linakuja katika ulimwengu wa roho kwako binafsi, “je! Unaamnini naweza kufanya
hili?”
Imani ni
lazima tunapokuwa katika maombi!
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼

0 coment�rios: