MAISHA YA MAOMBIKWA MKRISTO (PART 4)
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
MAISHA YA
MAOMBIKWA MKRISTO (PART 4)
(d) maombi
yanatupa nguvu ya kutoingia majaribuni!
Yesu
aliwawaambia wanafunzi wake maneno haya kwa uzito sana baada ya kuona wanafunzi
hawana maisha ya maombi! Walikuwa wanafikiri jukumu la kuomba ni la yesu tu!
Kama sisi tunavyofikiri sasa, kwamba jukumu la kuomba ni la watu fulani tu, na
si la kwetu! Kila mahali ambapo yesu alikuwa anaomba wanafunzi wake ambao leo
tunawatambua kama mitume! Walikuwa hawana maisha ya maombi. Angalia hapa luka
9:28-32,
“baada ya
maneno hayo yapata saa nane, akawatwaa petro na yohana na yakobo, akapanda
mlimani ili kuomba (hilo ndio lilikuwa lengo lakini angalia matokeo yake).ikawa
katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka….”. (hapa yesu anaomba peke yake
wale aliopanda nao walishamwacha walikuwa na usingizi). Petro na wale waliokuwa
pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi:lakini walipokwisha amka…”
Inaonyesha
wazi walikuwa wamelala wakati yesu anaomba! Walikuwa wanaona shida kuomba kama
sisi tunavyoona shida! Lakini tatizo lilikuwa linajirudia tena na tena kwa
wanafunzi mpaka ikabidi yesu awaambie madhara ya kutokuwa na maisha ya maombi!
Hapa lilikuwa tukio jingine sio lile la mlimani! Mathayo 26:40-41,
“akawajia
wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia petro, je! Hamkuweza kukesha
nami hata saa moja?.kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni.”
Sio toeni
sadaka ili msiingie majaribuni, sio hubirini sana ili msiingie majaribuni, hapa
yanatajwa maombi pekee. Kinyume chake hatutaweza kukabiliana na majaribu,
tutashindwa bila shaka. Maombi ndio yananifanya mimi na wewe kutoingia
majaribuni, majaribu yamejaa kila kona katika dunia ya leo, lakini tutawezaje
kuyashinda kama hatuna maisha ya maombi? Hatutaweza kamwe! Kamwe! Yesu
akishasema amesema! Mtu yeyote ambaye hana maisha ya maombi ana maisha ya
kuingia majaribuni! Mtu ambaye kuomba anaona shida; mtu huyo haina haja ya
kupeleleza maisha yake. Jibu lake linajulikana ni mtu wa kuingia majaribuni na
matokeo yake anajikuta anaishi maisha ya unafiki! Anaonekana anahubiri na
kufundisha, anaoneka anapost vitu vya kutia moyo, anaonekana anaombea watu,
lakini maisha yake ni ya kujilaumu wakati wote hana uwezo wa kushinda majaribu.
Ndugu yangu hata kama sisi tunajiita mtume nabii hata kama! Hata kama
tunajulikana vipi kiuimbaji na kukubalika katika nyimbo za injili, sifa na
kuabudu, kama hatuna maisha ya maombi majaribu yakija lazima tutaingia
majaribuni! Hatutaweza kushinda hata siku moja! Leo tunaweza tukajipiga piga
vifua kama petro,na kusema, “mimi nimuache yesu”. Ukisalimiwa “mambo”, unajibu
“mambo kwa yesu”. Misimamo hiyo kama huna maisha ya maombi lazima siku moja
utaingia majaribuni tu! Misimamo bila maombi! Hakuna matokeo ya ushindi.
Namkumbuka binti
mmoja ambaye alikuwa ameokoka! Binti huyu tulikuwa tunaishi naye jirani! Binti
alikuwa na misimamo ya hatari sana! Ilikuwa tukimsalimia “mambo?”. Aanajibu
“mambo kwa yesu.” Alikuwa hajibu kwa mizaha! Alikuwa hataki mchezo mchezo
ukizingatia pia kwao pesa zipo na wakati huo yupo kidato cha tatu! Mimi wakati
huo nilikuwa mbali na ufalme wa mungu! Misimamo ya binti huyu haikudumu kwa
sababu hakuwa na maisha ya maombi! Akaangukia kwa muuza mitumba na uwokovu
akauacha! Akakataa shule wakati huo tayari ameshaanguka tayari; wakati hilo
halijaisha vizuri mimba ikaingia akamwacha yesu! Misimamo bila maisha ya maombi
ninakuambia waziwazi wewe binti ambaye unajulikana shuleni kwako unaposoma,
chuoni kwako au kazini kwako, bila maisha ya maombi unaweza kujikuta unaanguka
mahali usipoptarajia.
Yesu
alimwambia petro waziwazi katika mathayo 26:34-35, “…yesu akamwambia, ‘amin,
nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Petro
akamwambia, ‘ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe.’”
Petro
anajigamba wakati hana maisha ya maombi; muda wa maombi yeye anasinzia, na
ndivyo ilivyokuwa, alimkana yesu kwa kiapo na alisema mathayo 26:69-74, “ndipo
alipoanza kulaani na kuapa na kusema, simjui mtu huyu.” Unaona, anasema “mtu
huyu.” Wakati petro alikuwa ananyenyekea
kwa bwana! Alikuwa anamuita yesu bwana! Lakini hapa anasema “mtu huyu “. Ndivyo
ilivyowatokea wengine ambao walipuuza maombi, leo ukiwaona utashangaa!
Unajiuliza huyu si alikuwa moto wa kuhubiri, kuomba, kutoa, kuimba n.k.!
Peleleza maisha yake kabla, utakuja gundua alikuwa hana maisha ya maombi! Na
ndivyo itakavyotokea kwetu kama hatutakuwa na maisha ya maombi, ninakuambia
wazi kabisa utashindwa tu!
Ndugu yangu
omba! Omba! Omba! Ndani ya maombi ndio kuna nguvu ya kutuwezesha kushinda
ushawishi huu uliotanda kila kona katika dunia, kila siku inafunguliwa mitandao
mipya ya kuturahisishia kufanya mambo mema na hapohapo ya kuturahishia kuingia
majaribuni! Tutawezaje kushinda vishawishi kama hatuna maisha ya maombi?
Tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki na mwisho ya siku tutamwita yesu “mtu ”
badala ya “bwana” kama ilivyotokea kwa petro! Tusipoomba kuingia majaribuni sio
jambo la kutafuta! Mtu yeyote ambaye hana maisha ya maombi, mtu huyo hawezi
kujizuia katika majaribu, kama sivyo yesu tunamfanya yesu kuwa ni muongo, na
kamwe yesu hawezi kuwa muongo!
Nb: maombi
ni kwa faida yetu wenyewe, tukiacha kuomba kwa sababu zozote kumkana yesu kuko
karibu! Omba! Omba! Omba!
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼

0 coment�rios: