MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 2)
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
Kwa nini
tunazuiwa kuomba? Pamoja na sababu nyingine zinaonekana kama ni za msingi!
Angalia hii!
(b) maombi
yanaweza kubadili maamuzi ya mungu aliyoyapanga kwa taifa au kwa mtu n.k.
Hii
tunaipata kwa nabii isaya! Tusome maandiko haya kwa makini saaana! Isaya 38:1
“siku hizo hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na isaya nabii, mwana
wa amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, ‘bwana asema hivi, tengeneza mambo ya
nyumba yako; maana utakufa,wala hutapona’.”
Ni ujumbe
kutoka kwa nabii! Mungu mwenyewe hapo anasema kwamba “utakufa”, hebu jaribu
kufikiri! Ingekuwa wewe mungu anakwambia hivyo ungefanyaje? Lakini mfalme huyu
alijua hata kama mungu amesema, bado ninaweza kubadili maamuzi yake kwa sasa
kwa njia ya maombi! Alichokifanya mfalme ni hiki! Isaya 38:2 “basi hezekia
akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba bwana..hezekia akalia sana sana.”
Hezekia alijua na aliamini kwamba maombi yanaweza kubadili maamuzi ya mungu
kabisa! Baada ya maombi hayo angalia kilichotokea. Isaya 38:4, “ikawa, neno la
bwana likamjia isaya, kusema, enenda ukamwambie hezekia, ‘mimi nimeyasikia
maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako…”. Hapo kuna
vitu viwili mungu aliviangalia wakati hezekia anaomba,
(1) kuomba
kwa imani. “ikawa, neno la bwana likamjia isaya, kusema, ‘enenda ukamwambie
hezekia, mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako.” (isaya 38:4).
(2) machozi
yaliyoambata na kuomba, japokuwa wako watu huwa wanasema walokole wanalialia,
tunalia ili mungu ayapokee maombi yetu, sisi hatulii kama hao waliliao mapenzi
usiku na mchana!
Maombi hapa
yaligeuza maamuzi ya mungu, nafikiri sasa unaweza kuelewa kwa nini tunazuiwa
kuomba. Ndugu kama unaomba; hata kama ni nani alitamka kitu gani kwako, au
katika ukoo wako kwa kulaani laana zozote zile, unakuta familia nyingine hakuna
maendeleo yoyote yale pamoja na bidii zote za kufanya kazi na kusoma! Hakuna
kuoa wala kuolewa n.k. Maombi yana uwezo wa kubadilisha laana na kuwa baraka na
kufumua fumua kila vitu vibaya vinavyohusika kutukandamiza na kutudidimiza
katika maeneo fulani fulani. Hata kama bosi alisema nitakusimamisha kazi,
maombi yanaweza kubadili maamuzi ya bosi! Kama maombi yaliweza kugeuza maamuzi
ya mungu sembuse bosi ? Sembuse rais wa nchi?
Twende
kwenye mfano wa pili uone maombi ambavyo yanakitu cha kipekee.
Hapa sasa
tunaona ibrahimu ambavyo alikuwa anawashawishi malaika waliotumwa na mungu kwa
ajili ya kuiangamiza sodoma na gomora. Mwanzo18:32. “je! Utaharibu mwenye haki
pamoja na mwovu? Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu wala
hutaacha mji.hasha usifanye hivyo,…bwana akasema, nikiona katika sodoma wenye haki
hamsini mjini, nitapaacha kwa ajili yao.”
Ibrahimu
aliendelea kusema na wale malaika mpaka akafikia hesabu ya watu 10! Na ibrahimu
akaishia hapo, kama ibrahimu angeendelea kusihi bila shaka maangamizo
yasingetokea. (mwa 18:30-32). Zaidi sana walichokifanya malaika ni kumuondoa
lutu na mkewe na wanawe ambao inaonyesha hawakufika 10 kama wangekuwa 10
wasingetolewa ili mji uangamizwe kwa sababu ibra alifanya maombi na yakajibiwa
kwamba kwa idadi ya watu 10 tu na kama hao 10 wangekuwepo sodoma na gomora isingeangamizwa,
wangeachwa na mungu angetumia njia nyingine! Maana alisema kama wamgekuwa 10
asingeuangamiza mji.
Maombi ni ni
kumshawishi mungu kufanya yale ambayo wewe unataka ambayo yatakuwa ndani ya
mpango wake. Kama maombi yanaweza kubadilisha maamuzi ya mungu; sembuse
kubadilisha maaumuzi ya mtu? Ndio maana sijatoka kuzungumzia mifano ya maamuzi
ya wanadamu yalivyobadilishwa baada ya maombi, nimezungumzia upande wa mungu
ili uone maombi ambavyo yana nguvu! Kuna kitu gani umetamkiwa? Kuna kitu gani
unakitaka? Muombe mungu kwa imani!
MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 3)
(c) kuwaacha
watu na kwenda kuomba!
Hili ni
tendo la ajabu sana ambalo yesu alilifanya! Lilikuwa ni fundisho kwetu! Hebu
jaribu kufikiri; kwa jinsi yesu ambavyo ana kila kitu, lakini pamoja na yesu na
kuwa na kila kitu, lakini alijua pasipo maombi yote aliyokuwa nayo haiwezekani!
Yesu mwenyewe alikuwa anajua hapa bila maombi hamna kitu! Alifikia mahali
anawaacha makutano halafu anakwenda kuomba. Luka 5:12-16. Hebu tusome mstari wa
16.
“lakini yeye
alikuwa akijiepua,akaenda mahali pasipokuwa na watu,akaomba.”
Hapo yesu
anawakimbia makutano na kuelekea zake kwenye maombi, japokuwa ni ngumu sana kwa
baadhi ya watu kuwaacha watu na kwenda kwa kuomba katika mazingira kama haya ya
yesu, kwao ni utukufu. Ikiwa yesu alifanya hivyo, sisi tunapaswa kufanya hivyo
na kuzidi kulingana na maisha yetu na dunia ya leo, lakini leo mtu anasema hana
muda wa kuomba, eti kazi zinambana, na kwa sababu nyingine zinazofanana na
hizo, lakini bado mtu huyohuyo ambaye anasema hana muda wa kuomba huyo huyo
unaweza kumuona katika makundi ya watu au marafiki akiongea muda mrefu, lakini
hao hao wanaosema hawana muda wa kuomba ni watu hodari sana kwa kuchat, hana
muda wa kuomba lakini ana muda wa kuchat na watu kwa njia ya whatsapp, muda
wote anafanya kazi huku yuko whats app! Hana muda wa kuomba lakini ana muda wa
kuongea na watu kwenye simu masaa na masaa, hana mua wa kuomba lakini
anaangalia movie masaa na masaa; hana muda wa kuomba lakini ana muda wa
kuangalia mpira …ninaweza kusema huyu hana muda wa kuongea na mungu lakini ana
muda wa kuongea na watu! Kwa sababu maombi ndiyo kuongea na mungu.
Kuongea na
watu si vibaya; si vibaya kuchat na watu kwa njia mbalimbali za mitandao,
lakini ni mbaya kama tuna muda wa kufanya hivyo lakini hatuna muda wa kuomba!
Ni mbaya sana! Sana ! Inatakiwa ifikie mahali tunaongea na watu lakini ukifika
muda fulani tunajiepua na kwenda mahali kusikokuwa na watu au mahali ambapo
tutaweza kuomba bila buguza! Hapa yesu hakwenda kanisani! Maombi tunaomba
popote pale kama mazingira hayaturuhusu kwenda kanisani, tukipata nafasi tu
kidogo tu; tunaomba hata kimoyomoyo! Kuomba sio lazima iwe kanisani.
Bila maombi
tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki! Maisha ya uhitaji wa kupitiliza na
kujikuta kwenye madeni wakati wote, ukiondoa maombi hata unahubiri kila siku
lazima iko siku utaanguka tu! Lazima! Tuache mambo ya kukaa kaa na watu na
kuongeaongea muda mwingi tunaumalizia kwa watu. Tena wakati mwingine mambo
mengine hayana hata maana, tunaopoteza kuongea na watu ambao hata tukienda
kulala hata hawajui yanayotusibu katika usingizi wetu. Hawana sifa ya kuongea
na sisi kabla ya kuongea na mungu wetu! Kama yesu aliomba mwenye huduma kubwa
kuliko huduma yako wewe ambaye unalewa na sifa za watu lakini kuomba hutaki!
Sisi tutapona? Shetani alikuwa hana kitu kwa yesu lakini bado yesu alikuwa
anaomba. Tusidanganywe na sifa zinazotoka vinywani mwa watu.
Tuweke
ratiba kwamba! Kuanzia muda fulani ni muda wa maombi. Hapo hata simu ipigwe
hakuna kupokea, tunakwenda mahali pasipokuwa na watu kifikra! Yesu alikwenda
sehemu halisi! Lakini kama mazingira yetu hayaturuhusu kufanya hivyo, tunapaswa
kwenda mbali na watu kifikra! Wakati wa kuomba ikiwezekana zima simu yako au
weka silent kama simu yako ndio kila kitu! Nikiwa na maana kuna bible n.k.
Yesu naye
tungesema hana muda, kwa sababu pale alikuwa kazini! Lakini alijua umuhimu wa
maombi! Kama wewe huna muda usile chakula basi! Kinachokufanya ule nini wakati
huna muda?
Nb: maombi
ni kwa faida yetu wenyewe
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼

0 coment�rios: