MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 2)

KUTAZAMA VIDEO YAKE BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


PICHA ZAKE ZOTE AKIWA MTUPU BONYEZA
HAPA CHINI▼▼


MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 2)
Kwa nini tunazuiwa kuomba? Pamoja na sababu nyingine zinaonekana kama ni za msingi! Angalia hii!
(b) maombi yanaweza kubadili maamuzi ya mungu aliyoyapanga kwa taifa au kwa mtu n.k.
Hii tunaipata kwa nabii isaya! Tusome maandiko haya kwa makini saaana! Isaya 38:1 “siku hizo hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na isaya nabii, mwana wa amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, ‘bwana asema hivi, tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa,wala hutapona’.”
Ni ujumbe kutoka kwa nabii! Mungu mwenyewe hapo anasema kwamba “utakufa”, hebu jaribu kufikiri! Ingekuwa wewe mungu anakwambia hivyo ungefanyaje? Lakini mfalme huyu alijua hata kama mungu amesema, bado ninaweza kubadili maamuzi yake kwa sasa kwa njia ya maombi! Alichokifanya mfalme ni hiki! Isaya 38:2 “basi hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba bwana..hezekia akalia sana sana.” Hezekia alijua na aliamini kwamba maombi yanaweza kubadili maamuzi ya mungu kabisa! Baada ya maombi hayo angalia kilichotokea. Isaya 38:4, “ikawa, neno la bwana likamjia isaya, kusema, enenda ukamwambie hezekia, ‘mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako…”. Hapo kuna vitu viwili mungu aliviangalia wakati hezekia anaomba,
(1) kuomba kwa imani. “ikawa, neno la bwana likamjia isaya, kusema, ‘enenda ukamwambie hezekia, mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako.” (isaya 38:4).
(2) machozi yaliyoambata na kuomba, japokuwa wako watu huwa wanasema walokole wanalialia, tunalia ili mungu ayapokee maombi yetu, sisi hatulii kama hao waliliao mapenzi usiku na mchana!
Maombi hapa yaligeuza maamuzi ya mungu, nafikiri sasa unaweza kuelewa kwa nini tunazuiwa kuomba. Ndugu kama unaomba; hata kama ni nani alitamka kitu gani kwako, au katika ukoo wako kwa kulaani laana zozote zile, unakuta familia nyingine hakuna maendeleo yoyote yale pamoja na bidii zote za kufanya kazi na kusoma! Hakuna kuoa wala kuolewa n.k. Maombi yana uwezo wa kubadilisha laana na kuwa baraka na kufumua fumua kila vitu vibaya vinavyohusika kutukandamiza na kutudidimiza katika maeneo fulani fulani. Hata kama bosi alisema nitakusimamisha kazi, maombi yanaweza kubadili maamuzi ya bosi! Kama maombi yaliweza kugeuza maamuzi ya mungu sembuse bosi ? Sembuse rais wa nchi?
Twende kwenye mfano wa pili uone maombi ambavyo yanakitu cha kipekee.
Hapa sasa tunaona ibrahimu ambavyo alikuwa anawashawishi malaika waliotumwa na mungu kwa ajili ya kuiangamiza sodoma na gomora. Mwanzo18:32. “je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu wala hutaacha mji.hasha usifanye hivyo,…bwana akasema, nikiona katika sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha kwa ajili yao.”
Ibrahimu aliendelea kusema na wale malaika mpaka akafikia hesabu ya watu 10! Na ibrahimu akaishia hapo, kama ibrahimu angeendelea kusihi bila shaka maangamizo yasingetokea. (mwa 18:30-32). Zaidi sana walichokifanya malaika ni kumuondoa lutu na mkewe na wanawe ambao inaonyesha hawakufika 10 kama wangekuwa 10 wasingetolewa ili mji uangamizwe kwa sababu ibra alifanya maombi na yakajibiwa kwamba kwa idadi ya watu 10 tu na kama hao 10 wangekuwepo sodoma na gomora isingeangamizwa, wangeachwa na mungu angetumia njia nyingine! Maana alisema kama wamgekuwa 10 asingeuangamiza mji.                                                                                                               
Maombi ni ni kumshawishi mungu kufanya yale ambayo wewe unataka ambayo yatakuwa ndani ya mpango wake. Kama maombi yanaweza kubadilisha maamuzi ya mungu; sembuse kubadilisha maaumuzi ya mtu? Ndio maana sijatoka kuzungumzia mifano ya maamuzi ya wanadamu yalivyobadilishwa baada ya maombi, nimezungumzia upande wa mungu ili uone maombi ambavyo yana nguvu! Kuna kitu gani umetamkiwa? Kuna kitu gani unakitaka? Muombe mungu kwa imani!

 MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 3)
(c) kuwaacha watu na kwenda kuomba!
Hili ni tendo la ajabu sana ambalo yesu alilifanya! Lilikuwa ni fundisho kwetu! Hebu jaribu kufikiri; kwa jinsi yesu ambavyo ana kila kitu, lakini pamoja na yesu na kuwa na kila kitu, lakini alijua pasipo maombi yote aliyokuwa nayo haiwezekani! Yesu mwenyewe alikuwa anajua hapa bila maombi hamna kitu! Alifikia mahali anawaacha makutano halafu anakwenda kuomba. Luka 5:12-16. Hebu tusome mstari wa 16.
“lakini yeye alikuwa akijiepua,akaenda mahali pasipokuwa na watu,akaomba.”
Hapo yesu anawakimbia makutano na kuelekea zake kwenye maombi, japokuwa ni ngumu sana kwa baadhi ya watu kuwaacha watu na kwenda kwa kuomba katika mazingira kama haya ya yesu, kwao ni utukufu. Ikiwa yesu alifanya hivyo, sisi tunapaswa kufanya hivyo na kuzidi kulingana na maisha yetu na dunia ya leo, lakini leo mtu anasema hana muda wa kuomba, eti kazi zinambana, na kwa sababu nyingine zinazofanana na hizo, lakini bado mtu huyohuyo ambaye anasema hana muda wa kuomba huyo huyo unaweza kumuona katika makundi ya watu au marafiki akiongea muda mrefu, lakini hao hao wanaosema hawana muda wa kuomba ni watu hodari sana kwa kuchat, hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuchat na watu kwa njia ya whatsapp, muda wote anafanya kazi huku yuko whats app! Hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuongea na watu kwenye simu masaa na masaa, hana mua wa kuomba lakini anaangalia movie masaa na masaa; hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuangalia mpira …ninaweza kusema huyu hana muda wa kuongea na mungu lakini ana muda wa kuongea na watu! Kwa sababu maombi ndiyo kuongea na mungu.

Kuongea na watu si vibaya; si vibaya kuchat na watu kwa njia mbalimbali za mitandao, lakini ni mbaya kama tuna muda wa kufanya hivyo lakini hatuna muda wa kuomba! Ni mbaya sana! Sana ! Inatakiwa ifikie mahali tunaongea na watu lakini ukifika muda fulani tunajiepua na kwenda mahali kusikokuwa na watu au mahali ambapo tutaweza kuomba bila buguza! Hapa yesu hakwenda kanisani! Maombi tunaomba popote pale kama mazingira hayaturuhusu kwenda kanisani, tukipata nafasi tu kidogo tu; tunaomba hata kimoyomoyo! Kuomba sio lazima iwe kanisani.

Bila maombi tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki! Maisha ya uhitaji wa kupitiliza na kujikuta kwenye madeni wakati wote, ukiondoa maombi hata unahubiri kila siku lazima iko siku utaanguka tu! Lazima! Tuache mambo ya kukaa kaa na watu na kuongeaongea muda mwingi tunaumalizia kwa watu. Tena wakati mwingine mambo mengine hayana hata maana, tunaopoteza kuongea na watu ambao hata tukienda kulala hata hawajui yanayotusibu katika usingizi wetu. Hawana sifa ya kuongea na sisi kabla ya kuongea na mungu wetu! Kama yesu aliomba mwenye huduma kubwa kuliko huduma yako wewe ambaye unalewa na sifa za watu lakini kuomba hutaki! Sisi tutapona? Shetani alikuwa hana kitu kwa yesu lakini bado yesu alikuwa anaomba. Tusidanganywe na sifa zinazotoka vinywani mwa watu.
Tuweke ratiba kwamba! Kuanzia muda fulani ni muda wa maombi. Hapo hata simu ipigwe hakuna kupokea, tunakwenda mahali pasipokuwa na watu kifikra! Yesu alikwenda sehemu halisi! Lakini kama mazingira yetu hayaturuhusu kufanya hivyo, tunapaswa kwenda mbali na watu kifikra! Wakati wa kuomba ikiwezekana zima simu yako au weka silent kama simu yako ndio kila kitu! Nikiwa na maana kuna bible n.k.

Yesu naye tungesema hana muda, kwa sababu pale alikuwa kazini! Lakini alijua umuhimu wa maombi! Kama wewe huna muda usile chakula basi! Kinachokufanya ule nini wakati huna muda?

Nb: maombi ni kwa faida yetu wenyewe
KWA NAFASI ZA KAZI POPOTE TANZANIA, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
[3.00 MB]VIDEO YA ALIKIBA AKIBANDUANA NA JOKATE, BONYEZA
HAPA CHINI▼▼



0 coment�rios: