VI. ASILI INAYOTOKANA NA TABIA MBAYA
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
VI. ASILI
INAYOTOKANA NA TABIA MBAYA
1kor 2:14”
mwanadamu ya tabia ya asili hayapokei mambo ya roho wa mungu…….”
Baadhi ya
watumishi au waumini wanasumbuliwa na tabia mbaya mbaya kutoakana na asili
mbaya ya kishetani iliyo ndani yao. Mfano; tabia ya jeuri, tabia ya ukorofi,
kuwa mkali sana, hasira kali sana, na ubishi uliovuka mpaka au kawaida.
VII. ASILI
INAYOTOKANA NA MANENO ULIYOTAMKIWA UKIWA TUMBONI.
ezekieli
16:5 “ hapana jicho lililokuhurumia ili kukutendea lolote la mambo hayo kwa
kukuhurumia, lakini ulitupwa nje uwandani, kwakuwa nafsi yako ilichukiwa ktk
siku ile uliyozaliwa”
maneno
uliyotamkiwa siku ile uliyozaliwa, yanahusiana na hatma yako au yale
yanayotokea hivi sasa maishani mwako.
Jiulize
maswali haya;
a) siku
uliyozaliwa wajomba zako walitamka maneno gani?
B) au wakwe
zake mama yako walisema nini siku uulizokuwa tumboni?
C)
iliposemekana kuwa umezaliwa, watu walifurahi au walichukia?
D) mawifi
zake mama yako walikutamkia maneno gani?
Majibu ya
maswali haya waweza kuyapata kwa njia ya ufunuo wa roho mtakatifu,fu 1kor
2:10…….. Au fanya utafiti uliize kwa wazazi wako au wakubwa zako walokuwepo
siku hizo.
VIII. ASILI
INAYOTOKANA NA MAPITO ULIYOPITIA
waamuzi
11:1-4
mapito
uliyopitia yanaweza kujenga usugu fulani, na kuamsha asili fulani ya kishetani
ndani yako na kuleta maadhara fulani. Mfano:
i. Mateso:
yanaathiri mfumo wa akili na saikolojia.
Ii. Kuvuta
bangi: akili inaharibika.
Iii. Ulevi:
unaleta ufukara na upumbavu.
Isaya 55:6
“mtafuteni bwana maadam anapatikana, mwiteni maadam yu karibu”….
Sasa ,
kumtafuta mungu aliye hai, inamaana yuko umbali fulani, ulimwengu wa roho. Ni
lazima ujue kanuni na maarifa ya kuutafuta uso wa bwana…
anaposema
“mwiteni bwana”, maana yake ni kusema; yuko sehemu au mahali fulani, mahali
mbapo ukimlilia na kuliitia jina lake, atakusikia… hii nayo yataka ufahamu wa
ki-mungu wa kukusaidia kujua namna ya kumwita mungu aliye hai
Math 7:7
"ombeni,nanyi mtapewa,tafuteni nanyi mtaona,bisheni nanyi
mtafunguliwa"
1.maombi ni
kutafuta,kubisha hodi kwa mungu.luka 18:1 "akawaambia mfano,ya kwamba
imewapasa kumwomba mungu sikuzote wala wasikatetamaa"
2.maombi ni
kumwendea mungu
ebr 11:6b
"kwa maana mtu amwendeaye mungu lazima aamini kwamba yeye yuko,na kwamba
huwapa thawabu wale wamtafutao"
3.maombi ni
kuzungumza na mungu isaya 1:18 "haya njoni tusemezane,asema bwana wa
majeshi,
4.maombi ni
kuweka wazi haja/mahitaji yetu mbele za mungu ,filip 4:6 "msijisumbue kwa
neno lolote,bali katika kila neno kwa kusali na kuomba,pamoja na kushukuru haja
zenu na zijulikane na mungu"
5.maombi ni
ibada mbele za mungu..mdo 13:2 "basi hawa walipokuwa wakimfanyia bwana
ibada na kufunga,roho mtakatifu akasema,
6.maombi ni
kupigana vita vya kiroho,efeso 6:18 "kwa sala zote na maombi mkisali kila
wakati katika roho,mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea
watakatifu"
7.maombi ni
kutulia na mungu isaya 30:15 "kwa maana bwana mungu asema hivi,kwa kurudi
na kustarehe mtaokolewa,nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kumtumaini lakini
hamkukubali"
KWANINI
YATUPASA KUOMBA?? MATH 7.7
1..tunaomba
ili tupewe haja zetu, "ombeni nanyi mtapewa",tena neno la mungu
linasema wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi,yakobo 4:2 "mwatamani wala
hamna kitu,mwaua na kuona wivu,wala hamwezi kupata,mwafanya vita na
kupigana,wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi"
2.ni agizo
kutoka kwa yesu..luka 18:1 "akawaambia mfano,ya kwamba imewapasa kumwomba
mungu siku zote,wala wasikate tamaa"
1thes 5:17
"ombeni bila kukoma"
3.kwa sababu
kuomba ni huduma..huponya taifa,familia,kanisa na watu wanaponywa magonjwa na
shida zao na kazi yake jehova hufanikiwa
2nyak 7:14
"ikiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu,watajinyenyekesha,na kuomba na
kunitafuta uso na kuziacha njia zao mbaya basi nitasikia toka mbinguni na
kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao"
4. Isaya
59:16 "akaona ya kuwa hapana mtu,akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi basi
mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu na haki yake ndiyo
iliyomsaidia"
yak 5:14-16
"mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa nao wamwombee na
kumpaka mafuta kwa jina la bwana na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa
yule na bwana
Atamwinua
hata ikiwa amefanya dhambi atasamehewa ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi,na
kuombeana mpate kuponywa,kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa
bidii"
5..kwa
sababu ya kujenga mahusiano yetu karibu na mungu
yak 4:8
"mkaribieni mungu naye atawakaribia ninyi,itakaseni mikono yenu enyi wenye
dhambi na kuisafisha mioyo yenu,enye wenye nia mbili"
6..kwa kuwa
mungu ni baba na sisi ni watoto wake,yatupasa kumwomba haki zetu tukiwa kama
watoto..
Math 6:9
"basi ninyi salini hivi,baba yetu uliye mbinguni,jina lako
litukuzwe,ufalme wako uje"
MAISHA YA
MAOMBI KWA MKRISTO (1)
Wako
wakristo ambao tunashindwa kuwa na maisha ya maombi kwa sababu zifuatazo.
(1) kukosa
muda wa kuomba kwa sababu ya majukumu ya muhimu ya hapa na pale.
(2)
mazingira ya mtu anapoishi.
(3) mwingine
hajui faida za maombi wala umuhimu wake.
(4) mwingine
anasema huwa anaishiwa maneno kwa haraka anapokuwa kwenye maombi.
(5) mwingine
hapendi maombi tu!
(6) shetani.
(7) mwili.
KATIKA
MAOMBI KUNA VIKWAZO VINGI, KWA SABABU MAOMBI YANA NGUVU!
(a) maombi
yanaongeza uhusiano wa mtu na mungu!
Maombi ni
mawasiliano baina ya mwanadamu na mungu au ni njia ambayo tunaweza kuwasiliana
na mungu. Tunafanya mawasiliano na mungu kwa njia ya maombi, na kama tunavyojua
kwamba! Mawasiliano yanaongeza uhusiano wa mtu na mtu, hata wewe ni shahidi
katika hili! Unaweza ukawa na ndugu wengi sana au marafiki wengi sana n.k.
Lakini yule ambaye atawasiliana na wewe mara kwa mara huyo ndiye anayeukuza
ukaribu kupita wengine. Na pia uhusiano wa mtu unaanzishwa kwa mawasiliano na
vilevile unaweza ukafa au kupungua kwa kukosa mawasiliano ya mara kwa mara na
kuelekezwa kule kwenye mawasiliano ya mara kwa mara! Mawasiliano yamewafanya watu
wengi kuwa karibu, kupitia mitandao yetu. Mtu alipoanza mawasilano na wewe kwa
njia ya kukutumia ujumbe wa maandishi au wa picha ulipojibu! Mawasilano yakakua
mwisho wake ukaribu ukaongezeka kati yako na huyo….
Tunapokuwa
tunaomba mara kwa mara uhusiano wetu na mungu unakuwa kwa kasi sana kuzidi yule
asiyeomba, au yule anayeomba mara moja moja au yule anayeomba kwa viwango vya
juu zaidi! Na kama tujuavyo, kadiri uhusiano wa mtu na mtu unavyokuwa na
kuongekezeka ndivyo wanavyoweza kushirikishana mambo mengi saaaana!
Ndivyo
inavyokuwa kwa mungu kwetu! Kwa sababu mahusiano yetu yanakuwa na kuongezeka!
Mungu hataacha kutushirikisha mambo mengi yanayoendelea ili kuyaombea au kuzuia
yasitokee au kuwashauri watu n.k. Mungu atatuonyesha hata hatari iliyopo mbele
yetu, kwamba! Kuna ajali mbaya itatokea na kusababisha hiki na hiki na jinsi ya
kuikwepa n.k. Yakiambatana na maelekezo yake jinsi ya kufanya ambayo yatakuwa
na lengo la kujenga na si kubomoa! Utakuwa na furaha na amani wakati woote hata
kwenye dhiki za namna gani! Sijui nitumie lugha gani nieleweke jamani: ili
uelewe hili na kulishika kwamba! Maombi yanaongeza uhusiano wa mtu na mungu!
Tuanze
maisha ya maombi kuanzia sasa ili uhusiano wetu na mungu ukue, anzisha
mahusiano yako na mungu kwa kuwasiliana naye mara kwa mara kwa njia ya maombi.
Hata kama zamani tulikuwa na bidii ya kuwasiliana na mungu kwa njia ya maombi
halafu tukayakata mawasilano hayo! Bado tunaweza kuyaanzisha upya na kuyakuza!
Pia usiache kuwasiliana na mungu mara kwa mara kwa njia ya maombi kwa sababu
kwa kutofanya hivyo utauvunja au utaupunguza uhusianao wako na mungu!
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼

0 coment�rios: