USHIRIKA NA MUNGU
HAPA CHINI▼▼
HAPA CHINI▼▼
UTANGULIZI:
JE, umewahi kuwasikia watu wakisema kuwa wanaabudu kwa namna zao wenyewe?
Wamechoshwa na “kanisa” na kwamba kukutanikia jangwani ni bora zaidi kwa sababu
jangwa haliwaambii maneno yasiyo mazuri. Ingawa ni ukweli kwamba ni muhimu
kutenga muda binafsi wa kuwa na mungu, katika somo letu juma hili yakobo
anaelezea manufaa ya kushirikiana [kuchangamana] kiibada na wakristo wenzetu.
Hebu tuzame kwenye somo letu la biblia ili tujifunze zaidi!
USHIRIKA NA
MUNGU
A. SOMA
YAKOBO 5:13. Maelezo ya fungu hili yanatuhusu watu wengi. Uwezekano mkubwa ni
kwamba aidha tuna matatizo au hatuna furaha. Tunatakiwa kuitikiaje uzoefu huu
wenye tofauti kubwa? (kwa kumgeukia mungu. Ama tunatakiwa kuomba kwa ajili ya
kupata msaada au tunatakiwa kumsifu mungu kwa njia ya nyimbo.)
1. Mwitikio wako kimaadili ni upi unapojikuta
kwenye matatizo? (siku za nyuma, papo hapo nilifanya kile nilichoweza ili
kutatua tatizo. Sasa nimejifunza kwamba hatua ya kwanza lazima iwe ni kumgeukia
mungu.)
2. Je, huwa unakasirika unapokabiliana na
matatizo? (asili ya mwanadamu huwa ni kuwalaumu watu wengine, na kisha
kukasirika kutokana na kile walichotutendea. Ikiwa, kwa uwezo wa roho
mtakatifu, tutamgeukia mungu kwanza, itatuepusha kusema au kutenda jambo baya
papo hapo kwa sababu ya hasira. Hii itaepusha kufanya tatizo kuwa gumu zaidi.)
B. Mtazamo
wa namna gani unaakisiwa kwenye ushauri wa yakobo kwa ajili yetu kuomba au
kusifu? (mungu ndiye anayeyashikilia maisha yetu. Yeye ndiye chanzo cha
mibaraka yote. Tunamgeukia ili kupata msaada na tunamshukuru kwa kumpa sifa.)
USHIRIKA NA WAUMINI
A. Soma yakobo 5:14-15. Kuugua ni mfano mahsusi
wa tatizo. Kwa nini usijiombee tu wewe mwenyewe – kama anavyobainisha yakobo
katika mstari wa 13? Kwa nini kuwahusisha wazee katika jambo hili? (mungu
hahitaji wazee kumshawishi ili afanye uponyaji, lakini wazo la kushirikiana na
waumini wenzako linaelezewa hapa.)
1. Kuna
nyakati kadhaa nilikuwa sehemu ya kundi la wazee waliomwombea na kumpaka mafuta
mgonjwa. Nchini marekani, watengenezaji wa dawa wanaeleza bayana athari za dawa
zao wakati ule ule wanapotangaza jinsi dawa zao zinavyoweza kutibu. Mke wangu
alikuwa akiniambia kwamba nilitakiwa kubainisha jambo hili nilipokuwa sehemu ya
wanaofanya maombi na kupaka mafuta katika kipindi cha nyuma ambapo wagonjwa
hawakupona. Mke wangu alikuwa akitania, lakini hadi siku za hivi karibuni,
jambo hilo lilibakia kuwa ukweli mtupu. Je, yakobo anatoa ahadi za uongo kuhusu
uponyaji?
A. Je, mimi ndiye niliyekuwa tatizo? Yakobo
anapoandika “na kule kuomba kwa imani,” je, alikuwa akiandika kuhusu imani ya
wazee? Kama sivyo, anaelezea imani ya watu gani, je, ni imani ya mgonjwa?
B. Soma
marko 2:1-5. Je, hapa yesu anazungumzia imani ya nani? (haiko wazi. Yesu
anaonekana kuzungumzia imani yao wote.)
C. Soma mathayo 18:19. Vipi kama mgonjwa alikuwa
na imani na mzee mmoja pekee ndiye alikuwa mwenye haki, je, imani hiyo
ingetosha kuleta uponyaji? (utagundua kwamba yesu haonyeshi kiwango cha imani
au haki inayotakiwa, anabainisha tu idadi ya waumini waliokubaliana. Wawili
wanatosha.)
D. Hebu
tuangalie tena yakobo 5:15. Je, yakobo anatoa muda wa kuinua na kuponya?
(hapana. Nina uhakika kila mtu aliyekuwa kwenye huduma ya kupaka mafuta ambapo
mimi pia nilihusika alikuwa mdhambi – kuanzia mgonjwa hadi kwa wazee wote.
Yakobo hasemi kwamba hatutakiwi kuwa na dhambi, anasema kwamba tunatakiwa kuwa
na imani. Kwa kuongezea, hatoi muda kwa ajili ya uponyaji. Ninaamini mungu
atawafufua katika uzima wa milele wote waliolala wakimtumaini yeye.)
E. Kipindi cha hivi karibuni kabisa ambapo
nilikuwa sehemu ya kundi la wazee waliokwenda kufanya maombi, mgonjwa
aliponywa. Mungu anatenda miujiza maishani mwangu, na kwenye maisha ya wale
ninaowaombea, na ninaamini hili linahusiana zaidi na mapenzi ya mungu mwenye
enzi, badala ya haki yangu. Je, wewe unadhanije?
UPONYAJI,
IMANI NA DHAMBI
A. Angalia
tena sehemu ya mwisho ya yakobo 5:15 na marko 2:5. Yesu anamwambia mwenye
kupooza kwamba dhambi zake zimesamehewa. Yakobo anasema, dhambi zinaweza
kusamehewa. Je, kuna uhusiano gani kati ya uponyaji na dhambi?
B. Soma yohana 9:1-3. Kwa nini wanafunzi
waliuliza kuhusu dhambi na upofu? (uelewa wa kipindi hicho ulikuwa ni kwamba
dhambi ilisababisha magonjwa. Nadhani bado kuna ukweli mwingi kwenye uelewa
wao.)
1. Je, yesu alisema kuwa sababu ya upofu ni ipi?
(ili mungu aweze kutukuzwa. Haikuwa suala la dhambi.)
2. Dhambi inapoungamwa na kusamehewa, je, mungu
anatukuzwa? (ndiyo! Angalao kauli za yakobo na yesu kuhusu ugonjwa na dhambi
zina maelezo ya aina mbili. Kwanza, ni uelewa wa watu wa kipindi hicho. Lakini,
jambo la muhimu zaidi ni kwamba, mungu anataka kutuponya dhambi. Lengo lake kuu
kwetu ni kuwa na maisha yasiyo na dhambi na ugonjwa – na lengo hilo litatimia
mbinguni.)
C. Siku
chache zilizopita nilikuwa mapumzikoni kwa muda wa siku kadhaa eneo la “disney
world,” ambapo watu wanene wanakusanyika na kuendesha vijigari. Kiukweli, watu
wengi waliokuwepo mahali pale pia walikuwa wanene. (katika kuzungumzia suala la
unene, niliweza kuongezeka uzito wa kilogramu 1.8 nilipokuwa likizo!) Wakati
huo huo, sikumwona mtu hata mmoja akivuta sigara. Inaonekana kwamba hatari ya
kiafya inayotokana na uvutaji wa sigara imebadilishwa na hatari ya kiafya
inayosababishwa na unene mkubwa kupita kiasi. Swali gumu ni hili: je, dhambi
inaweza kuingiliana na uponyaji?
1. Kama utasita kumwombea mvuta sigara ili aweze
kuponywa, vipi kuhusu mtu mnene kupita kiasi?
2. Je, kiasili baadhi ya watu si ni wanene tu?
Je, hilo linajalisha?
3. Nimesoma sana kuhusu ubongo, na
ninashawishika kwamba mazoezi ni tiba ya watu wote kwa magonjwa ya aina yote,
yakiwemo masuala ya kiakili. Je, kushindwa kufanya mazoezi ni dhambi
inayotuzuia tusiponywe?
4. Je, nimemtukana takribani kila mtu?
Ninachokimaanisha ni kwamba tunawaangalia wavuta sigara wanaougua saratani ya
mapafu, na wasenge wanaougua ukimwi, na hatuwahurumii sana kutokana na matendo
yao.
KUTUBU
[KUUNGAMA] DHAMBI
A. Soma tena yakobo 5:15. Muda wa msamaha ni
upi? (baada ya mtu kuponywa. Hii inaashiria kwamba uponyaji upo kwa ajili ya
watu wote.)
B. Soma yakobo 5:16. Hebu subiri kidogo! Baada
ya mjadala wetu juu ya dhambi, je, yakobo anasema kuwa tunatakiwa kutubu dhambi
zetu ili tuweze kuponywa? Au, je, kuombeana sisi kwa sisi ndio kigezo pekee
kinachohusiana na uponyaji?
C. Angalia
tena yakobo 5:16. Unafikiria nini kuhusu kutubu dhambi kwa waumini wenzetu?
D. Soma
zaburu 51:4, zaburi 32:5 na 1 yohana 1:9. Je, mafungu haya yanapendekeza kwamba
tutubu dhambi zetu kwa nani? (tunatenda dhambi dhidi ya mungu, na mungu ndiye
ana uwezo wa kusamehe dhambi. Hivyo, inaleta mantiki kutubu dhambi zetu kwa
mungu.)
E. Unapotafakari kuhusu jambo hili, je, kuna
aina mbalimbali za kutubu? (ninadhani hivyo. Kwanza, kuna kutubu na msamaha wa
dhambi, jambo ambalo ni suala kati yako na mungu. Pili, mathayo 18:15, luka
17:4 na mambo ya walawi 6:1-5, mafungu yote hayo yanaashiria kwamba kuna dhambi
ambazo tunatakiwa kuombana msamaha sisi kwa sisi. Tatu, ni kile ninachodhani
yakobo anakizungumzia; mantiki ya jumla kwamba tunatenda kazi na waumini
wenzetu ili kuelekea kwenye haki. Tunaombeana sisi kwa sisi, tunajadiliana
dhambi zetu sisi kwa sisi, tunajadiliana masuala ya kiroho sisi kwa sisi.)
NGUVU YA
MAOMBI
A. Soma
yakobo 5:17-18 kisha usome sehemu ya mwisho ya yakobo 5:16. Tumekuwa tukijadili
juu ya dhambi, lakini nadhani yakobo amejikita kwenye maombi. Kwa nini yakobo
anamtaja eliya kama mfano? (anasema alikuwa “mwanadamu mwenye tabia moja na
sisi.” Sote tuna uwezekano wa kuwa na maombi yenye nguvu na ufanisi mkubwa.)
1. Soma 1
wafalme 19:3-4. Kwenye mjadala wetu hadi tulipofikia, nimelinganisha
[nimehusianisha] masuala ya kiafya na dhambi. Katika mathayo 15:16-18 yesu
anapendekeza kwamba mlingayo huu si sahihi. Kwa upande mwingine, kutokumtumaini
mungu ni dhambi (ufunuo 21:8). Yakobo anapotuelekeza kwa eliya, je, anasema
nini? (imani na udhati katika maombi ndio ufunguo wa uponyaji, sio kutokuwepo
kwa dhambi.)
B. Soma
yakobo 5:19-20. Haya yanaonekana kama madai ya mwisho ya “matendo” – ikiwa
tutawaongoa upya “waliorudi nyuma” dhambi nyingi zitasamehewa. Je, muktadha huu
unaashiria kuwa uelewa sahihi wa jambo hili ni upi? (unazungumzia juu ya uelewa
wetu wa dhambi, badala ya asili ya wokovu. Sura hii ilikuwa inazungumzia juu ya
kufanya ushirika [kuchangamana]. Ikiwa mtazamo wako ni kuwaunga mkono na
kuwaokoa washiriki wenzako wa kanisa, basi kitendo hicho, badala ya kupoteza
muda, ndicho kilicho cha muhimu machoni mwa mungu.)
C.Rafiki,
je, wewe ni sehemu ya watu wanaofanya ushirika wa mara kwa mara? Kama wewe si
sehemu ya kundi hilo, basi unakosa kipengele cha muhimu sana cha kuwa mkristo.
Kwa nini usitubu juu ya jambo hili na kuungana na kundi linaloshikilia imani na
utii?
MAOMBI YA
KUSAMBARATISHA UCHAWI NA NGUVU ZA GIZA
Baba katika
jina la yesu. Laana zote nilizo tupiwa na wabaya wangu zimeshindwa kwa jina la
yesu na nazivunja na kuzisambaratisha kwa damu ya yesu. Mshindwe wote mnao tuma
laana kwangu katika jina la la yesu.
Nawavunja na
kuwaharibu na kuwakatakata wachawi wote kwa damu ya yesu.
Nasambaratisha
kila neno la uovu lililosemwa juu yangu na famila yangu katika jina la yesu.
Naharibu na
kuisambaratisha madhabahu yenu mliyo fanyia kafara kwa damu ya yesu.
Navunjavunja
na kubomoa kila uovu na uchawi mnaonifanyia katika jina la yesu.
Nairudisha
misukule yote na majini yote yawarudie nyie na kuwalipa dhambi zote mnazo fanya
katika jina la yesu.
Naharibu
kila uchawi, kila urogi, kila ndumba kila aina ya uovu ambao mnaufanya ili
uniumize mimi na familia yangu katika jina la yesu.
nawateketeza
kupitia damu ya yesu wachawi wote walio tumiwa kunitumia uchawi katika jina la
yesu.
Nawateketeza
na kuwaharibu majini yote yaliyo tumwa kuja kufanya kazi hiyo waliyo tumwa na
wachawi katika jina la yesu.
Nawateketeza
na kuwauwa makuhani wote ambao walienda kunishitaki kwa wachawi ili waniharibie
maisha, nawateketeza kupitia damu ya yesu. Nawachoma kwa moto wa roho mtakatifu
katika jina la yesu.
Nateketeza
aina zote za vyombo vya kichawi vilivyo tumiwa kuja kunichunguza katika jina la
yesu.
Naharibu
fikra zao zote ambazo wanazitumia kufanya kazi zao za kichawi katika jina la
yesu.
Nafuta
kumbukumbu zoote zangu ambazo wamewapa mashetani, majini, roho chafu, nafuta
hizo kumbukumbu kwa kutumia damu ya yesu, katika jina la yesu aliye hai.
Nawateketeza
waweka kumbukumbu wa kimashetani kupitia damu ya yesu aliye hai. Naharaibu na
kuchoma kupitia moto wa roho mtakatifu makabrasha yote yenye kumbukumbu zangu
katika jina la yesu.
Kila uchawi
ulio fanywa ili uje kuharibu maisha yangu na ubomoa kupitia damu ya yesu.
Kila uchawi
ulio fanywa ili uje kuniua nauvunja na kuuteketeza kupitia damu ya yesu.
Kila uchawi
ulio fanywa ili kuja kuiba mali zangu, nauvunja na kuubomoa na kuuharibu
kupitia damu ya yesu.
Kila uchawi
ulio fanya kuja kuniharibia familia yangu, nausambaratisha na kuuvunja na
kuubomoa katika jina la yesu.
Kila neno la
kichawi lililo tumwa ili kuja kuniharibia, kunidhihaki, kunitendea mabaya
nalirudisha kwa aliye lituma katika jina la yesu.
Kila uovu,
uchawi, wanga, ndumba, ramli, yaliyo tumwa kuja kwangu navunja yote hayo
kupitia damu ya yesu na katika jina la yesu.
Nyota yangu
ambayo wanaita nairudisha kupitia damu ya yesu. Nyota yangu ya baraka nailinda
na kuzungushia na kuizingira na damu ya mwana kondoo katika jina la yesu.
Namteketeza
yule mtu aliye kuja kuiba nyota yangu katika jina la yesu.
Nateketeza
mbinu zote wanazo tumia ili kuja kuiba nyota yangu katika jina la yesu.
Nateketeza
wivu wao, chuki yao, laana zao, maovu yao na kila aina ya uchafu ambao wanao
kwa ajili yangu katika jina la yesu.
Naizungushia
na kuizingira nyumba yangu na damu ya yesu.
Naishungushia
na kuizingira familia yangu na damu ya yesu.
Nashungushia
na kuzingira maisha yangu yote na damu ya yesu.
Navunja
laana zote zilizo semwa na mabau zangu katika jina la yesu.
Navunja
laana zato ambazo zilisemwa bila ya mimi kufahamu, nazivunja na kuziharibu
kupitia damu ya yesu na katika jina la yesu.
Narudisha
kila mali walizo ziiba kutoka kwangu katika jina la yesu.
Narudisha
kila baraka walizo ziiba kwangu katika jina la yesu.
Narudisha
amani na upendo katika familia yangu.
Damu ya yesu
ipo juu ya maisha yangu na inasafisha kila uovu, kila uchawi unaaribiwa na damu
ya yesu katika jina la yesu.
Leo hii
mtaiona nguvu iliyopo katika damu ya yesu.
Katika jina
la yesu aliye hai ninaomba.
Amen
MUNGU
AKUBARIKI SANA KWA KUPATA KITABU NINAMANI KITAKUSAIDIA / KIMEKUSAIDIA KATIKA
KAISHA YAKO YOTE.
HII NI
SEHEMU YA KWANZA YA KITABU JUU YA SOMO LA MAOMBI.
KIMEANDALIWA
NA MWINJILIST LAURENT E. MPOMA.
KANISA LA
PENTECOSTAL CHRISTIAN CENTER – MISUNA SINGIDA
KUJIPATIA
VITABU VINGINE AU UNAHITAJI MAOMBI FIKA KANISANI PENTECOSTAL CHRISTIAN CENTER –
MISUNA –SINGIDA
AU PIGA
SIMU:+255763652896, 714890889.
MUNGU
AKUBARIKI SANA>>>>>>AMINA.
HAPA CHINI▼▼
During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip.
HAPA CHINI▼▼

0 coment�rios: