SOMO LA ARDHI, SEHEMU YA KWANZA

0 coment�rios
Image result for PICHA YA ARDHI
SOMO: KUMBEA  ARDHI

SABABU YA KWANZA

SOMA: MWANZO 3:17-19

Akamwambia Adamu,Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako ,ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza,  nikisema,Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;

Michongoma na miiba itakuzalia , nawe utakula mboga za kondeni; Kwa  jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi ,ambayo katika hiyo ulitwaliwa ;kwamaana  u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.Biblia inasema “Ardhi imelaaniwa kwa ajili yako “ … Neno laana maana yake…..kutokustawi, kutokufanikiwa, kutokufurahi,kutokufikia kiwango cha mafanikio Mungu alicho kikusudia  kwa ajili ya maisha  yako.


Ardhi imepata shida kwa sababu ya laana iliyobebwa na mtu.

SABABU YA PILI
SOMA: MWANZO 4:11-12
Basi sasa umelaaniwa  wewe katika ardhi , iliyofumbua kichwa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako
Utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake ; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikoa duniani.

Hi ni tofauti na ile sura ya tatu..surs ys tatu laana iko ndani ya Adamu sura ya nne laana ipo ndani ya Ardhi …maana yake kila atakaye kanyanga ardhi laana itatoka chini na kumfuata
Huwezi kutulia mahali,unajaribu kujenga hapa pana kataa unajaribu kukaa hapa panakataa lakini haujajua ya kwamba unapata shida  kwa sababu ya shida iliyopo kwenye ardhi…uharibifu uliotokea kwenye ardhi unakufanya  kutotulia …Biblia isinge semesha masuala haya ingekua shida sana

Kuna tofauti ya kuombea ardhi ( kuna laana iliyopo ndani ya ardhi na  na laana iliyopo kwa mtu anayetumia ardhi)

SABABU YA TATU
SOMA: 2 NYAKATI 7:12-14
Bwana akamtokaea Sulemani usiku, akamwambia , nimesikis ulivyo omba na mahalia hapa nimejichagulia kuwa nyumba yangu  ya dhabihu .
Nikizifunga mbingu isiwe mvua , tena nikiamuru nzige kula nchi au nikiwapelekea watu wangu tauni;

Ikiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu watajinyenekesha na kuomba na kunitafuta uso na kuziacha njia zao mbaya  basi nitasikia kutoka mbinguni nan a kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao


 Nchi ni mipaka yenye ardhi halali na taifa ni kundi la watu waliokubalia kuwa na mfumo wa uongozi wa kuwaunga pamoja
Ndio maaana kweny Biblia familia inaweza kuwa taifa ..na watu wengi sana wengi sana wanapotaka kuliombea taifa …

Haizungumzii  juu ya uponyaji wa watu bali uponyaji wa ardhi amabayo watu wanakaa.


 Mungu anapo weka mstari wa ahadi cheki mwiso wake. Itafsiri Biblia jinsi ilivyo, Cheki Mungu ameahidi nini lasivyo utapata shida sana .

SABABU YA NNE
SOMA: YEREMIA 22:29-30
Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neon la Bwana
Bwana asema hivi, Andikeni habri za mtu huyu kwamba hana watoto , kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zote ; maana hapana mtu katika uzao wake akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi na kutawala tena katika Yuda.

Unaombaje wakati ardhi imepewa amri na agizo kwamba ; Hautafanikiwa wewe wala watoto wako.Huyu ni Mungu anazungumza nan chi (ardhi)……Maana yake ardhi au udongo unaweza kutunza kumbukumbu….inaweza kufuatilia kumbukumbu zilizopo ndani.

Wakati adhabu inatolewa kwa mtu huyu alikuwa bado hana watoto , kwa hiyo kumbukumbu kwenye ardhi ni kwamba  ni kwamba hana moto na kumbukumbu zina sema kwamba hata atakapopata watoto hata fanikiwa .

Adhabu ilitolewa kwa sababu gani; cheki ule mstari wa 21 …..huyu mtu alifanikiwa mwazoni lakini kutokana na kutotii sauti ya Mungu ; Mungu akasema its ok ngoja niondoe hayo mafanikioa  na ardhi inisaidie kuweka kumbukumbu kwa sababu huyu jamaa yupo duniani  atakanyanga ardhi tu na ardhi ishaandika hana motto na atakapoppata watoto hatawatafanikiwa maisha yao yote.

Fikiria wewe ni motto na umeingia kwenye adhabu ya baba au mama na unatafuta kufanikiwa na haufaninikiwi  sio kwamba akili huna no unazo lakini umezuiliwa kufanikiwa je unaombaje?


SABABU YA TANO
SOMA: MWANZO 28: 10-20
10 Yakobo akatoka  Beer-sheba , kwenda harani 11 Akafika mahali Fulani akalala huko usiku kucha , maana jua lilikuwa  limekuchwa ,akatwaa jiwe moja la mahali pale  akaliweka chini ya kichwa chake , akalala usingizi palapale 12 Akaota ndoto, na tazama ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni .Tena tazama malaika  wanapanda na kushuaka juu ya yake  13   Na tazama Bwana amesimama juu yake , akasema mimi ni Bwana, Mungu wa Ibrahim baba yako na Mungu wa Isaka , nch hii uilalayo ntakupa wewe na uzao wako


 Ninachotaka uone , Ardhi unayolala  ,iwe ni nyumba uliyolala , au ni hotel,au kwenye basi au shambani halafu ghafla  ukaota ndoto , shukuru Mungu kwa sababu kakuonesha kinachoendelea katika ulimwengu wa Roho saa hiyo  saa ingine anaweza akakujulisha tafsiri yake baadae au asikujulishe kabisa … au unaamka unajikuta una hali tofauti na ile uliyokuwa nayo wakati ulipokuwa umelala

Alipo lala ardhi na roho ya umiliki ya mahali pale  ikaamua kumtembelea na kugusa maisha yake jumla , Mungu alijifunua kwake.

Na watu wengi sana wanapata shida au wanakwama kutegemeana na roho ya mahali wanapo lala. Ndio maana usipojua namna ya y kujikung’uta utapata shida sana na kitu ambacho unaweza kuwa umekutana nacho either kwenye hotel.. kikakutesa maisha yako jumla.
Nimeona wengine wamekuwa wakiteseka kutokana na mahali walipo lala wakiwa shuleni(bording)

Piawatumishi wengine  wakienda kwenye huduma  mahali wakatokewa na nuru wanafikiri ni Mungu na maisha yake ya huduma yana badilika completely na  na maana yake hakujua namna ya kuomba ,,,, alijiombea yeye akasahau ardhi ya mahali alipolala na hakuna mtu aliyemfundisha kuomba kwa stail hiyo.


•             
SABABU YA SITA
SOMA: 2 SAMWELI 21:1
Kulikuwa na njaa siku za daudi  muda wa miaka mitatu , mwaka hadi mwaka  naye Daudi akautafuta uso wa Bwana , Bwana akasema ni kwa ajili ya Saul, na nyumba yake yenye damu  kwa kuwa aliwaua hao wagibeoni.

Usishangae sana kuona hali ya njaa  ukasema hii haihusiani na hali ya kiroho ya ardhi.
Ukisoma ule mstari wa 14.. unaona Mungu anaiponya ardhi ;
Kwa hiyo Mungu alikuwa anaponya ili kumsaidia daudi kwenye kipindi chake ambapo kulikuwa na njaa kusiwe na njaa na kuwe na chakula …. Biblia inasema ….. alipata kibali ikaachiliwa Baraka, Baraka iliondolewa makusudi kabisa

Usishangae sana Daudi alikaa na upako lakini njaa ilikuwepo kwanini? Kwa sababu alishindwa kuunganisha shida ya njaa na tatizo la ardhi.  Hadi pale Mungu alipomwonesha .

Biblia inasema akatafuta uso wa Bwana kutaka kujua chanzo.

SABABU YA SABA
SOMA: UFUNUO 12:12- 15
Kwa hiyo shangilieni; enyi mbigu ,nanyi mkaao humo ole wan chi na bahari ! kwa maana Yule ameshuka kwenu kwenye ghadhabu nyingi akijua ya kuwa ana mda mchache tu
Na Yule joka alipoona ametupwa katika nchi alimwudhi mwanamke Yule aliyezaa  mtoto mwanaume
Mwanamke Yule akapewa mabawa mawili ya tai Yule mkubwa ili aruke aende zake nyikani , hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati mbali na nyoka huyo,
Nyoka akatoa katika kinywa chakenyuma ya huyo mwanamke maji kama moto amfanye kuchukuliwa na mto ule.

SABABU YA NANE
SOMA: YOELI  7:9-13
Utaombaje ikiwa hali ya kiroho ya ardhi imesababisha sadaka zizuiliwe kutolewa kanisani.

Wachungaji wapo kanisani wao wanamwomba Mungu awasaidie  watu watoe sadaka sawasawa  Mungu ana sema hapana shida sio kutoa sadaka sawasawa sadaka zilikuz zinakuja ni mimi niliyezizuia  … badala ya kuombea wakristo ombea hali ya ardhi ya nyumbani kwao ..ikishapona ardhi swala la kutoa sadaka litakuwa rahisi sana


SABABU YA TISA
SOMA: KUMBUKUMBU LA TORATI 8 7-12
Nilitaka uone lile neno kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake  ina mahusiano na Baraka za Mungu juu ya watu walioingizwa kwenye nchi  au kwenye mipaka halali ya umiliki

Ndio maana kati ya adhabu mojawapo inaifikia nchi ni miji kubomolewa au kukosa wakazi, kuwa ukiwa , kuwa mahame;…….laana aliyoilaani Yesu miji ya Bethsaida katiaka nchi ya Israeli tumepita kule ni magofu mpaka leo.

Biblia inazungumza Mungu  akirudia eneo anawapa na uwezo watu wliorudi kujenga pale kwa upya , wanajenga na wana kaa nadni yake . Na wale ambao Mungu aliwabbarikia na wakajenga halafu wakamkorofisha Mungu,  Biblia inasema watajenga na wasikae ndani.



inaendelea>>>>>>





















Read More »

SOMO: KUTEMBEA NA MUNGU

1 coment�rios

VITU VYA KUZINGATIA UNAPOAMUA KUTEMBEA NA MUNGU

Mwanzo 5:21-24
1. Mwisho wa maisha yako ni wa muhimu sana kuliko mwanzo wako.

"Mwanzo wako ni kiashiria cha mwisho wako lakini mwisho wako hutuonesha/hudhihirisha hatima yako"

Biblia inatoa hesabu ya idadi ya siku zote alizoishi Henoko kuwa ni miaka mia tatu na sitini na mitano (365), lakini inasema katika miaka hiyo Henoko alitembea na Mungu miaka mia tatu (300). Maana yake miaka sitini na mitano (65) Henoko alikuwa akitembea kwenye njia yake mwenyewe. Biblia inaweka wazi kabisa kuwa Henoko alianza kutembea na Mungu baada ya kumzaa Methusela na utakumbuka kuwa Methusela alizaliwa Henoko akiwa na miaka sitini na mitano (65). 

”Enock alipomzaa Methusela akiwa na umri wa miaka 65 aliamua kutembea na Mungu kwa imani katika muda wa miaka 300. Hii ikiwa na maana kuwa maisha ya Enoko kabla ya kufanya uamuzi wa kukubaliana na Mungu kutembea pamoja katika kila hatua ya maisha yake, alitembea katika njia zake mwenyewe au katika mwelekeo aliodhania mwenyewe kuwa ulimfaa, ni mpaka pale alipoamua kwenda na Mungu katika mwelekeo anaotaka Mungu.

2.kutembea na Mungu kunahusisha uamuzi na utayari.

Mungu hawezi kutembea na mtu ikiwa mtu huyo hayupo tayari kutembea na Mungu. Ni kwa yule ambaye anatafuta kwa bidii kutembea na Mungu ndiye atakaye weza kutembea na Mungu. Kwa lugha rahisi naweza kusema ni mpaka utakapogundua umuhimu na uhitaji wa kutembea na Mungu kwenye maisha yako na kuchukua hatua ya kutafuta ndipo ufahamu huo utakusukuma kwenye hatua ya kuanza kutafuta kutembea na Mungu. Waebrania 11:6 Waebrania 11:6 inasema "6 Na pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu kwa maana kila mtu anayemjia ni lazima aamini kuwa yupo na kwamba yeye huwapa tuzo wale wanaomtafuta kwa bidii.

Wakristo wengi wanaona kuwa wanaweza kwenda mwendo wa maisha yao bila uwepo wa Mungu kwenye kila kitu ambacho kinazunguka maisha yao. Kutokujua au kuona umuhimu wa jambo hilo, kumesababisha wengi kwenda uelekeo wowote wanaoutaka kwenye maisha yao kwasababu kukosekana kwa Mungu kwenye hatua za maisha ya mwanadamu humfanya mtu kuwa huru kwenda uelekeo wowote lakini kuwepo kwa Mungu katika matembezi yako hukupa nidhamu inayokusaidia kwenda kwa uelekeo ambao Mungu anataka uende nae. Hii ni kwasababu "Kujua unapokwenda hukusaidia kutokwenda katika mwelekeo usiotakiwa kwenda"

3. kutembea na Mungu kunahusisha kuishi tofauti na tamaduni zilizokinyume na maadili ya ufalme wa Mungu

Kutembea na Mungu kwenye maisha yetu kunahusisha kuishi katika mila, desturi na tamaduni za ufalme wa Mungu uliekubali kutembea pamoja nae ili ikusaidie kwenda pamoja nae.Kwa lugha rahisi naweza kusema "kutembea na Mungu kunahusisha kuishi kinyume na tamaduni zilizokinyume na maadili ya ufalme wa Mungu"uliekubaliana nae kwenda pamoja katika safari yenu.
Enoko kutembea na Mungu katika wakati wake kulihitaji uamuzi mgumu na utayari wa moyo kwasababu wakati alioishi, jamii iliyomzunguka, maadili ya watu katika jamii yake yalikuwa yameharibika sana. Aliamua kuishi kwa mujibu wa kanuni na mila za ufalme wa Mbinguni ambazo zilitofautiana sana na kupingana na tamaduni za jamii aliyokuwa akiishi wakati huo.

Mungu alipoumba ulimwengu huu alikuwa amekusudia ulimwengu huu utawaliwe kwa kanuni, Mila na desturi za mbinguni. Hii ni kwasababu dunia ni ulikuwa ni mwendelezo wa kiutawala wa serikali ya mbinguni. Ni muhimu kufahamu wakati wa ukoloni kuwa ni serikali za kifalme tu ndio zilikuwa zinamiliki makoloni ambapo koloni lilihesabiwa kuwa ni mwendeleo wa eneo lakini ambalo liko mbali na serikali inayotawala koloni hilo.

4.Kutembea na Mungu kunahusisha kwenda na Mungu katika kila hatua unayopiga katika maisha yako.

Kutembea na Mungu kunahusisha makubalino katika uhusiano wako na Mungu. Amos 3:3 inasema " Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja wasipokuwa wamepatana? "
Kutembea uhusisha hatua moja kwenda nyingine na uhusisha kwenda katika uelekeo mmoja, hatua kwa hatua. Biblia haisemi kuwa Enoko na Mungu walitembea kwa miaka 30 kisha Enoko akatembea mwenyewe kisha alipofikisha miaka 80 akaanza tena kutembea na Mungu, Hapana! Mwendo wao ulikuwa ni wa kila siku kwa miaka 300.

Kutembea kwa Enoko na Mungu kulikuwa na maana hii ni kumfanya Mungu kuwa ni sehemu ya maamuzi yako, sehemu ya mawazo yako, ni sehemu ya kalenda (ratiba yako), ni sehemu ya muda wako, ni sehemu ya mahusiano yako. Kila hatua unayochukua kila siku kwenye maisha yako, Mungu anakuwa sehemu muhimu, hakuna unachokifanya bila yeye kuhusika 


5.Kutembea na Mungu kunahusisha Imani.
Enock aliweza kutembea na Mungu kwa njia ya Imani sio kwa kuona. Inawezekana labda alipata nafasi ya kusikia habari kuhusu Mungu na akaamua kuamini kuhusu Mungu huyo. Miaka 300 aliweza kuwa na uhakika na Mungu ambaye hajawahi kumuona kwa macho lakini akaamini kuhusu Mungu huyo. Katika wakati alioishi Enoko hapakuwa na Bliblia kama ilivyo kwetu leo, hata amri sheria alizotoa Mungu kupitia Musa zilikuwa bado hazijatolewa, hapakuwa na mashujaa wa imani kama akina Ibrahimu, Daniel na wengine wengi ambao tunasoma habari zao leo na zinatusaidia kuinua viwango vya imani mioyo mwetu kuhusu Mungu. 

Waebrania 11:6 inasema"
Wakati alizoishi Enoko inawezekana kutembea kwake na Mungu kwa maana ya kumshirikisha Mungu katika kila eneo la maisha yake ilionekana ni kama kupoteza muda au kuwa mshamba, lakini mwisho wa matembezi yao Mungu alimpa thawabu ya uaminifu wake katika matembezi yao ya miaka 300 kwakua haikuwa jambo rahisi.

6.Kutembea na Mungu kunahusisha mazungumzo kati yako na Mungu.
Watu wawili wanapokuwa wanatembea ni lazima mazungumzo yanajitokeza katikati yao, kila mmoja anazungumza na mwenzake na kushirikiana mawazo au mipango waliyonayo. Ndio maana Biblia inasema 1Wathesalonike5:16 inasema"Ombeni bila kukoma"

Haiwezekani kutenganisha Neno la Mungu,maombi na mtu alieamua kutembea na Mungu. Maombi na kusoma Neno la Mungu ni njia pekee ambayo hudumisha/uhimarisha mazungumzo kati yetu na Mungu. Kwa maombi unapata nafasi ya kumueleza Mungu na kwa Neno lake Mungu anazungumza na wewe. Ikiwa watu wawili wanatembea safari ndefu bila mazungumzo(conversation), huona safari yao kuwa ni ndefu, ngumu na yenye kuchosha sana, lakini wanapozungumza hujikuta safari yao imekuwa fupi Licha ya kuwa ilikuwa na uchovu mwingi, ni tofauti na mtu anaetembea Peke yake.
Hiki ndicho kitu kinachotokea mtu anapokuwa anazungumza na Mungu kwa njia ya maombi na kumsikiliza Mungu katika Neno lake katika safari ya maisha tunayoishi, kwa kadiri tatizo alilonalo mtu anavyoliona kubwa, kila wakati anapozungumza na Mungu kwa njia ya maombi, hujikuta anaona tatizo alilonalo sio zito au kubwa kama alivyokuwa akifikiri. 

7 . kutembea na Mungu kunahitaji kuwa na picha kamili ya wapi unapoelekea.

"Kujua unapokwenda hukusaidia kutokwenda katika mwelekeo usiotakiwa kwenda "
Neno la Mungu hutusaidia kufahamu zaidi kuhusu njia tunayoiendea, ni muhimu kwa mtu anaetembea na Mungu kufahamu na kuliishi neno la Mungu. Kulifahamu Neno ni jambo jingine na kuliishi neno ni hatua nyingine. Wakristo wengine wana fahamu Neno ila wameshindwa kuliishi Neno kama linavyoelekeza, hivyo inapoteza ile maana ya Kulifahamu Neno, ni sawa na mwanafunzi aliyepelekwa shule kuelimika halafu tunamleta kwenye elimu ya vitendo anashindwa ku apply ujuzi, maarifa na ufahamu alionao maana kunakuwa hakuna tofauti na ambaye hakwenda shule kujifunza ulichojifunza.

Yuda 1:14-15 inasema " Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu (mwandishi hakutaka wasomaji wachanganyikiwe maana kulikuwa na Henoko wawili katika familia ya mzee Adamu Mwanzo 4:17, hivyo mwandishi alitaka wasomaji waelewe kuwa alikuwa hazungumzi Henoko huyo mtoto wa Kaini bali nazungumzia Henoko baba yake Methusela kwasababu watu wanaweza kuwa na majina yanayofanana lakini wasiwe na tabia zinazoendana au kufanana.tofauti yao ilikuwa hivi; Henoko mtoto wa Kaini alifahamika na watu kwasababu baba yake alijenga mji na kuuita Henoko lakini Henoko huyu baba yake Methusela hakufahamika sana na watu lakini alifahamika sana na Mungu mbinguni. Swali ni unataka nani kulijua jina lako?), mwandishi wa kitabu cha Yuda anaendelea kusema Henoko huyo baba wa Methusela...alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu, ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake." 

8.Namna unavyoishi inaamua namna unavyoondoka (How you live will determine how you leave).

Paulo katika 2Timotheo 4:6-8 inasema “6Kwa maana mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. 7Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, imani nimeilinda

mungu akubariki
ukihitaji maombi
piga 0763652896, 0782859946, 0714890889


Read More »

Mungu Ni Nani?

1 coment�rios


Mwanamke akisali kwa Mungu
1. Kwa nini tumwabudu Mungu?

Mungu wa kweli ndiye Muumba wa vitu vyote. Hana mwanzo wala mwisho. (Zaburi 90:2) Yeye ndiye Chanzo cha habari njema inayopatikana katika Biblia. (1 Timotheo 1:11) Kwa kuwa Mungu ndiye aliyetuumba, tunapaswa kumwabudu yeye peke yake.​—Soma Ufunuo 4:11.

2. Mungu yukoje?
Hakuna mwanadamu ambaye amewahi kumwona Mungu kwa kuwa yeye ni Roho. Mungu hana mwili wa nyama na damu kama viumbe wanaoishi hapa duniani. (Yohana 1:18; 4:24) Hata hivyo, tunaweza kutambua utu wa Mungu kupitia vitu alivyoumba. Kwa mfano, matunda na maua ya aina mbalimbali yanafunua upendo na hekima ya Mungu. Ukubwa wa ulimwengu unafunua nguvu za Mungu.​—Soma Waroma 1:20.

Tunaweza kujifunza mengi zaidi kuhusu utu wa Mungu kwa kuisoma Biblia. Kwa mfano, Biblia inatueleza mambo ambayo Mungu anapenda na anayochukia, na jinsi anavyoshughulika na watu katika hali mbalimbali.​—Soma Zaburi 103:7-10.

3. Je, Mungu ana jina?
Jina la Mungu, Yehova, katika lugha mbalimbali
Yesu alisema: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.” (Mathayo 6:9) Ingawa Mungu ana majina mengi ya cheo, ana jina moja tu. Linatamkwa kwa njia tofauti katika kila lugha. Katika Kiswahili kwa kawaida jina hilo linatamkwa “Yehova.” Lakini watu fulani wanalitamka “Yahweh.”​—Soma Zaburi 83:18.

Jina la Mungu limeondolewa katika Biblia nyingi na mahali pake kuchukuliwa na majina ya cheo Bwana au Mungu.  Lakini Biblia ilipoandikwa, jina la Mungu lilipatikana mara 7,000 hivi. Yesu alifanya jina la Mungu lijulikane alipokuwa akiwafundisha watu kuhusu Mungu.​—Soma Yohana 17:26.

4. Je, Yehova anatujali?
Baba na mama wakimhangaikia mtoto wao ambaye ni mgonjwa
Kama baba huyu mwenye upendo, Mungu anatenda kwa njia itakayotuletea manufaa ya kudumu

Kwa kuwa tunateseka sana leo, je, hilo linamaanisha kwamba Yehova ni Mungu asiyetujali? Watu fulani wanadai kuwa Mungu anatuacha tuteseke ili atujaribu. Lakini hilo si kweli.​—Soma Yakobo 1:13.

Mungu amempa mwanadamu uhuru wa kufanya maamuzi. Tunathamini sana uhuru tulio nao wa kuchagua kumtumikia Mungu. (Yoshua 24:15) Hata hivyo, watu wengi wamechagua kuwafanyia wengine mambo mabaya, ndiyo maana kuna mateso mengi. Yehova anaumia anapoona ukosefu huo wa haki.​—Soma Mwanzo 6:5, 6.

Yehova ni Mungu anayetujali. Anataka tufurahie maisha. Hivi karibuni, ataondoa mateso na wale wanaoyasababisha. Kwa sasa, ana sababu nzuri ya kuwaruhusu wanadamu wateseke kwa muda fulani. Tutajifunza kuhusu sababu hiyo katika Somo la 8.​—Soma 2 Petro 2:9; 3:7, 13.

5. Tunaweza jinsi gani kumkaribia Mungu?
Mwanamke akisali kwa Mungu
Yehova anatualika tumkaribie kupitia sala. Anapendezwa nasi tukiwa mtu mmojammoja. (Zaburi 65:2; 145:18) Yuko tayari kutusamehe. Anatambua jitihada zetu za kumpendeza, hata ingawa nyakati nyingine tunakosea. Kwa hiyo, licha ya kutokamilika kwetu, kwa kweli tunaweza kufurahia urafiki wa karibu pamoja na Mungu.​—Soma Zaburi 103:12-14; Yakobo 4:8.

Kwa kuwa Yehova ametupa uhai, tunapaswa kumpenda kuliko tunavyompenda mtu mwingine yeyote. (Marko 12:30) Kadiri unavyoonyesha upendo wako kwa Mungu kwa kujifunza mengi kumhusu na kufanya yale anayotaka, ndivyo utakavyomkaribia zaidi.​—Soma 1 Timotheo 2:4; 1 Yohana 5:3.

Inayotangulia
Inayofuata
Pata Kujua Mengi Zaidi

HABARI NJEMA KUTOKA KWA MUNGU!

Je, Mungu Ana Jina?
Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile, Mweza-Yote, Muumba, na Bwana. Lakini jina la kibinafsi la Mungu limetumiwa mara 7,000 hivi katika Biblia.




Read More »

AINA YA MIFUNGO:

0 coment�rios

Image result for picha neno la mungu
AINA YA MIFUNGO:
1. Mfungo kamili
Katika mfungo huu hakuna kula kabisa chakula kigumu bali waweza kunywa maji au kimiminika chochote cha kukusupport.
Siku ngapi waweza kufunga mfungo wa aina hii unategemea na neema na malengo yako katika mfungo huo. Wengine huenda siku moja, mbili, tatu, wiki, n.k n.k

2. Mfungo nusu
Mfungo nusu huanzia saa 12 asbh hadi saa 9 mchana au kuanzia jua linapoibuka hadi linapozama. Mfungo ambao madhehebu mengine wamewazoeza waumini wao kuufanya. Wengine wameweza kuufanya kila ijumaa. Madhehebu ambayo yamewazoesha watu wao kufunga angalau kila wiki mara moja wameweza kuwa na mafanikio makubwa sana katika kuzifungua nira na vifungo mbali mbali

3. Mfungo wa Daniel
Daniel alifunga mifungo miwili ya aina yake;
• Katika Sura ya I Daniel alifunga alikula mboga mboga tu (Yaweza kuwa alikula mboga mboga na juisi Fulani Fulani)
• Katika sura ya 10 Daniel alifunga kwa siku 21 kwa kutokula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwake”

Ngoja nikomee hapa kwa leo hadi wakati mwingine na Mungu akubariki sana na kama umependezwa na ujumbe huu hebu share na mwingine ili naye abarikiwe.

Nakushukuru sana wewe ambaye umekuwa ukibarikiwa na neno la Mungu ambalo tumekuwa tukijifunza pamoja kwenye huduma hii na umeona ni vema kuungana nasi kuwafikishia pia wengine injili (hasa walioko vijijini) kwa njia ya vipeperushi. Nawashukuru wote mnaoendelea kujitoa kwa ajili ya hili. Lengo letu ni kutengeneza vipeperushi angalau 5,000 kwa mwezi. Kipeperushi 1 ni tshs 250 tu. Kama unabarikiwa na neno ambalo tumekuwa tukishirikishana naamini utapenda pia watu walioko mazingira yasiyokuwa na Internet wafikiwe na injili hii kwa njia ya vipeperushi.

Ungana nasi kwenye huduma hii kwa kadri ya kufanikiwa kwako na Mungu akubariki. ‘Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema” #2KOR. 9:6-8. Hebu fanya kazi nasi kwa njia hii kwa kupenda. Ukichangia hata vipeperushi 2 (tshs 500 tu) kwa wiki au kwa mwezi waweza kuwafikishia injili watu zaidi ya 10. Utakuwa umeshiriki utume mkuu pamoja nasi. Basi changia kwa kadri ya kufanikiwa kwako.

YASIYOWEZEKANA KWA WANADAMU, KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA.


Read More »

NJIA SABA(7) ZA KUPIGANA VITA YA KIROHO KWA MAOMBI

0 coment�rios
mwinjilisti: LAURENT ELIAS MPOMA
2. Kufunga na kufungua.


Mathayo 16:19 ''Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.''

Hii ni njia yenye vipengele viwili tofauti lakini kila kipengele kinamhitaji mteule wa KRISTO.
Kufunga maana yake kukataa jambo lisitokee.
Kufunga ni kuzuia jambo la kishetani ambalo lilipangwa likupate, lakini kwa maombi yako ya kulizuia hakika jambo hilo halitakupata.
Unaweza ukazuia ajali kwa maombi yako, unaweza ukazuia ugonjwa, unaweza ukazuia kuonewa, unaweza ukazuia kuteswa na wachawi, unaweza ukazuia kutokuzaa, unaweza ukazuia kila kazi ya shetani katika maisha yako. Ni Mamlaka hiyo MUNGU amekupa kama Mteule wake ili ukizuia vitu katika ulimwengu wa roho hakika vinazuiliwa.

Mathayo 18:18 '' Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.''

Kipengele cha pili ni kufungua.
Hiyo maana yake unaruhusu kilicho cha MUNGU kitokee.
Unaruhusu kilicho haki yako ambacho kilizuiliwa kipepo sasa kitokee kupitia maombi yako ya kufunga kazi za shetani na kufungulia baraka zako.
Katika njia hii ya kufunga na kufungua ni muhimu sana kuwa mtu unayeongozwa na ROHO MTAKATIFU ndipo utashinda kwa urahisi.
Kumbuka sio vitu vyote unaweza kufunga na sio kila kitu unaweza kufungua. Maombi ni somo pana sana na maombi sahihi ni yale ambayo ROHO MTAKATIFU anakuongoza tu.
Kazi ya ROHO MTAKATIFU ni kutuongoza katika kweli ya MUNGU hivyo hata katika maombi yako ya kufunga kazi za shetani na kufungulia baraka zako zilizokuwa zimeshikiliwa kipepo na mawakala wa shetani hakika unamuhitaji sana ROHO MTAKATIFU ili akujulishe ni nini cha Kufunga kwa maombi na ni nini cha Kufungua kwa maombi.
Ukikataa ushauri na maongozo ya ROHO MTAKATIFU huwezi kuwa sahihi hata siku moja.
Zaburi 32:8 '' Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.''

Mteule wa MUNGU una mamlaka kuu sana MUNGU amekupa kwa sababu umekubali kumpokea YESU KRISTO kama Mwokozi wako, lakini mamlaka ya kimaombi ya kufunga mambo ya giza na kufungua mambo ya baraka unahitaji sana sana ROHO MTAKATIFU akufundishe na kukujulisha.
Ndugu unayo mamlaka kubwa sana ambayo wasio na YESU hawana, wasio na ROHO MTAKATIFU hawana lakini unahitaji sana kumwambia ROHO MTAKATIFU akusaidie na kukujulisha ni vitu gani vya kufunga na ni vipi vya kufungua.

3. Kuziondoa nguvu za giza.

Marko 16:17-18 '' Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu WATATOA PEPO; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.''

Maandiko haya yana vitu vingi lakini kwenye somo langu nahusika na kanuni/Njia za kiroho za kupigana vita ya kiroho.
Njia hii inaitwa kutoa nje nguvu za giza ndio maana Biblia inasema ''Watatoa mapepo''
Mapepo ni nguvu za giza ambazo zinaweza zikawekwa na mawakala wa shetani popote.
Wengi sana wanateswa na majini ambayo ndiyo hayo hayo mapepo.
Unaweza ukateswa na ugonjwa mbaya sana na ambayo huwa unaondoka na kurudi kumbe ulirushiwa jini likajigeuza ugonjwa usiopona na ugongwa huo unakutesa.
Kuna ambao hadi walikufa kwa kuteswa na magonjwa ya ajabu huku hawajui kama ni majini walirushiwa yakajigeuza ugonjwa ndani ya miili yao na magonjwa hayo yanawatesa na wengine magonjwa mengine hata wakienda hospitalini vipimo havionyeshi kama wanaumwa, lakini wao wanaumwa sana sana.
Hata biashara yako inaweza ikarushiwa majini na wachawi wanaokusakama.
Ufahamu wako unaweza ukatupiwa mapepo kiasi kwamba huwa unalitumikia kusudi la shetani na sio la MUNGU.
Mapepo kama nguvu za giza zinaweza zikatesa ndoa, ukoo, familia au mwili wako.
Neema ya MUNGU ni ya ajabu sana sana maana kwa waliookoka haswa MUNGU ametupa Mamlaka na uwezo wa kuwatoa nje majini wote na kila nguvu za giza ili watoke katika miili yetu na maisha yetu.
Bwana YESU alisema kwamba moja ya kazi za wateule wake ni kuzitupa nje kazi za shetani ziitwazo mapepo/majini.
Ni kazi ya mteule wa KRISTO kuyatoa nje ya mwili au familia au ukoo au biashara mapepo yote yaliyotumwa.



4. Kushindana.

Waefeso 6:11-13 ''Vaeni silaha zote za MUNGU, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za MUNGU, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.''

Tunashindana kimaombi na tunashinda.
Tunashindana na viumbe wasioonekana lakini tunawashinda na kuwangamiza.
Ni Mamlaka tumepewa na ni ushindi kwetu ni lazima.
Ni muhimu sana kuomba maombi ya kushindana na adui ili umshinde.
Kumbuka adui hakuogopi wewe ila anamuongopa YESU KRISTO Mwokozi wako.

Adui anamuogopa ROHO MTAKATIFU aliye ndani yako.
Unahitaji kuwa muombaji sana ili uwashinde maadui zako kiroho.
Kiufunuo unaweza kujikuta hata unaomba maombi ya kufunga ili kuwashinda maadui zako.
Mawakala hao wa shetani wanajua kabisa kwamba wewe ukikaa katika nafasi yako ya maombi hakika unawashinda na kuwadhuru sana, ndio maana moja ya kazi ambazo shetani anazifanya kwako ili akufunge zaidi basi ni kuhakikisha hujifunzi Neno la MUNGU la kukusaidia na huombi.
Lakini kwa wanaojitambua hakika uko ushindi mkuu kutoka kwa MUNGU kwa wewe kuomba maombi ya kuwapiga adui zako ili wakimbie.

Shetani na watoto wake hawana jinsi wakisikia jina la YESU KRISTO, Ni lazima wakimbie hakika. Ndugu hakikisha unaitumia mamlaka ya KRISTO iliyo ndani yako kuwashinda maadui zako.
Biblia inasema ''Kushindana kwetu sio juu ya damu na nyama'' maana yake kumbe tunapaswa kushindana na mawakala wa shetani.

Usiposhindana nao watakuonea sana maana hawatakutana na vita wakikuvamia.
Ndugu itumie kanuni hii ya kushindana nao ili uwashinde.
Huwezi ukawa na jina la YESU KRISTO, Damu ya YESU KRISTO, Nguvu za ROHO MTAKATIFU na Neno la MUNGU harafu adui ashindwe kukukimbia, haiwezekani.
Unahitaji kuomba maombi ya kuwashindana maadui zako, hiyo ni kanuni ya kimaombi na njia ya kimaombi inayokuhitaji wewe muombaji.
Msaada wa MUNGU huwa ni mkubwa sana kwa mtu anayejua kupigana vita vya kiroho vya kushindana na mawakala wa shetani.
Yeremia 1;19 '' Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema BWANA, ili nikuokoe. ''

5. Kupinga.

Yakobo 4:7 '' Basi mtiini MUNGU. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. ''
Hii kanuni muhimu sana yaani kimaombi unapinga kila kazi ya shetani na hakika haitafanikiwa kazi hiyo ya giza.

Kumtii MUNGU ndio kumpinga shetani.
Tunahitaji kumpinga shetani katika mambo yake yote, ni kanuni ya wateule wa MUNGU.
Kipengele hiki kina maana ya kumwingilia shetani katika kazi zake na kumzuia kuendelea kufanya kazi hizo, hiyo ni mamlaka ya mteule wa MUNGU.

Tunampingaje Shetani?
1.Tunampinga shetani kwa maombi ya kumpinga.
2. Tunampinga kwa kukataa kufuata kazi zake na matendo yake.
3. Tunampinga shetani kwa sisi kulitii Neno la MUNGU.
4. Tunampinga shetani kwa sisi kuongozwa na ROHO MTAKATIFU.
5. Tunampinga shetani kwa Neno la MUNGU.
1 Petro 5:8-9 ''Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani. ''

Ndugu, ni kazi yako na jukumu lako kumpinga shetani.
Kumpinga shetani ni kanuni ya kimaombi iliyo muhimu sana.
Kumpinga shetani ni kumzuia kuendelea kukunyanyasa na kukuonea.
Kumpinga shetani ni kumkataza kuingilia ndoa yako, uchumi wako, uchumba wako, au akili yako.
Kwa maombi hakika unaweza kuwapinga ,mawakala wa shetani na wakakimbia hakika maana wanajua kwamba yeye shetani hana nguvu hata moja kwa aliyeko ndani yetu yaani ROHO wa MUNGU wetu.

1 Yohana 4:4 ''Ninyi, watoto wadogo(Wateule wa KRISTO), mwatokana na MUNGU nanyi mmewashinda(Mawakala wa shetani), kwa sababu yeye aliye ndani yenu(ROHO MTAKATIFU) ni mkuu kuliko yeye(Shetani) aliye katika dunia.''

6. Angusha.

2 Kor 10:3-5 '' Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika MUNGU hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya MUNGU; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii KRISTO; ''

Kanuni nyingi muhimu ya kimaombi ni kuteka fikra ili zipate kumtii YESU KRISTO.
Ni kanuni ambayo kanisa la MUNGU linaagizwa liitumie katika maombi.
Unaweza ukawa na mawazo ndani yako ya kufanya kitu fulani kumbe ni mawazo ambayo hayatokani na MUNGU, Usipojua kuyaangusha mawazo na fikra mbaya ambazo ziko kinyume na Neno la MUNGU hakika unaweza kujikuta wewe ni mtu wa kufanyia kazi wazo la shetani kila siku na mwisho wake hakuna baraka za MUNGU katika wazo lililotokana na shetani.
Hakikisha unaangusha kila fikra iliyo kinyume na Bwana YESU ndipo utapata fikra ya MUNGU.
Tiisha mawazo yako ili yawe mawazo yanayokubaliana na Neno la MUNGU.
Kuna mawazo ya kipepo mengi tu yanaweza kukukumba na hakikisha unaangusha mawazo hayo na fikra hizo zilizo kinyume na Neno la MUNGU.

Moja ya fikra ambazo inawezekana unazo na hizo fikra ni potofu sana na za kipepo ni hizi hapa.
1. Mawazo ya dhambi.
2. Mawazo ya kujilaumu.
3. Mawazo ya kujiona hufai hata kama umeshatubu na kuokoka.
4. Mwazao ya kujihukumu bila kosa
5. Mwazao ya kujidhania huwezi bila watu fulani n.k
Ni aina nyingi sana za mawazo ya kipepo ambayo mtu wa MUNGU unaweza kujikuta unafanyia kazi na kwa njia hiyo unapishana na kusudi la MUNGU.
Unahitaji sana kuitumia kanuni hii ya kimaombi ya kuangusha kila mawazo na fikrra ili zipate kumtii KRISTO na Neno lake.
Mawazo ya shetani siku zote yako kinyume na Neno la MUNGU.
Hakikisha unaangusha kila fikra na mawazo ili yapate kumtii KRISTO.
Tumia kanuni hiyo ya kimaombi ya kuangusha fikra na mawazo mabaya yote ili yasifanye kazi katika maisha yako.

7. Kung'oa, Kubomoa, Kuharibu na kuangamiza

Yeremia 1:10 ''angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda. ''



Read More »

KITABU CHA USHINDI WA MAOMBI , SOMA HAPA

0 coment�rios


1. Maombi ni nini?
Maombi ni mawasiliano kati ya mungu aliye hai na mmwanadamu, kupitia; sala,shukrani, maombezi, dua na maombi. 1tim 2:1
kwa ajili hii ni lazima pawepo na njia mbili, yaani: kuomba, na kujibiwa. Kwahiyo ukiomba ni lazima ujibiwe.
2. AINA ZA MAOMBI
i. Maombi ya kufunga.
Ii. Maombi ya rufaa.
Iii. Maombi ya utetezi.
Iv. Maombi ya mapatano.
V. Maombi ya shukrani.
Vi. Maombi ya kuteka mateka.
Vii. Maombi ya vita.
Viii. Maombi ya kubariki.
Ix. Maombi ya kulaani.
X. Maombi ya kunuiza.
Xi. Maombi ya ulinzi.
Mt 4:1-3, yosh 1:1-3, zab 35:1-9, hes 6:22-24, 1tim 2:1-4, uf 8:1-5, zab 34:7-9.



MAANDALIZI YA MAOMBI; KUT 19:7-20
Kabla haujaingia katika maombi ya muda mrefu au siku kadhaa, zingatia yafuatayo;
i. Andaa chumba utakachofanyia maombi.
Ii. Fanya usafi katika chumba hicho utakachofanyia maombi.
Iii. Na wewe binafsi uwe msafi, yaani uoge vizuri.
Iv. Vaa nguo safi kila asubuhi, baada ya kuoga.
V. Uwe na biblia , daftari na kalamu.
Vi. Unapoingia ili kuanza maombi, jitakase kwanza kwa damu ya yesu kristo wa nazareth.
Vii. Takasa chumba unamofanyia maombi.
Viii. Imba nyimbo kadha.
Ix. Fungua mbingu.
X. Mwangushe mfalme wa giza wa anga.
Xi. Karibisha malaika wa maombi, ulinzi, nguvu, vita na wa enzi ya mungu baba.
Xii. Mtukuze mungu baba, mwana na roho mtakatifu.
Xiii. Panga mahitaji ya kuombea kwa kuzingatia sheria za ufalme wa mbinguni, na ulimwengu wa roho.
Xiv. Hakikisha simu yako uwe umeizima siku zote za maombi.
Xv. Baada ya kupeleka mahitaji yako, tenga muda wa kutafakari neno kwa kujisomea biblia.
Xvi. Tenga muda tena wa kutulia ili usubirie majibu ya maombi yako.

4. NJIA ANAZOTUMIA MUNGU KUKUJIBU MAOMBI
i. Njozi. Dan2:27.
Ii. Ndoto. Mwa 37:1-9.
Iii. Maono. Ezek 8:1-3.
Iv. Ufunuo. Uf 1:1-11.
V. Dhamiri safi au njema, mdo 23:1.

5. NAMNA YA KUHAKIKI MAJIBU YA MAOMBI
amuz 6:14-17
ili uwe na uhakika na sauti inayo sema na wewe kutoka ulimwengu wa roho, uliza hivi: “ni nani wewe unayesema nami katika jina la yesu?” Rudia swali hili mara 3, wakati unahoji juu ya sauti au kiumbe hai kinachosema na wewe wakati huo kutoka ulimwengu wa roho….. Kama ni ni malaika kutoka mbinguni, atajitambulisha kwako. Kama ni pepo au shetani atakimbia.

6. AINA ZA MAJIBU YA MAOMBI
i. Niko pamoja na wewe- ayubu.
Ii. Nitakusaidia- yesu kristo.
Iii. Nitakupigania- mfalme daudi. (hili ndilo jibu zuri).
Isa 41:8-13, zab 35:1-9.

7. BAADA YA KUMALIZA MAOMBI
Umalizapo maombi, tenga muda wa kutulia nyumbani kwako. Epuka haya yafuatayo;
i. Epuka kwenda kukaa kijiweni.
Ii. Epuka maongezi ya kipuuzi yasiyokuwa na maana.
Iii. Epuka kuongea kwa makelele sana, bali uwe mtulivu.
Iv. Epuka vijiwe vya umbea na masengenyo, maana yanapunguza; utukufu na nguvu.
V. Epuka kuangali vipindi vya runinga kama filamu au tamthilia zenye matukio ya kuhuzunisha, au kusikitisha au ya aibu.
Vi. Epuka kukaa maeneo yenye makelele.
Vii. Kama wewe ni mchungaji, askofu au kiongozi wa huduma fulani; tulia nyumbani kwako siku3, siku ya jumapili usihubiri wewe, bali mwachie mwingine ahubiri madhabahuni. Maana baada ya maombi malaika wataendelea kukuhudumia, huku wakikujenga utu wa ndani, wakikukarabati utu wa ndani kama watakavyokuwa wameelekezwa na mungu, hii ni pamoja na kukuvika silaha za mbinguni, vipawa na karama na kukuumba utu wa ndani. (mt 4:1-11).
Viii. Aidha jitenge na marafiki wapagani na wasiomcha mungu, mapema tu baada ya kumaliza maombi. Bali ambatana na wale walio jaa nguvu za mungu na wanao maanisha katika utumishi na maombi. Luka 9:28-32.

8. FAIDA ZA KIROHO ZA MAOMBI
i. Maombi ni silaha.
Ii. Maombi ni nguvu.
Iii. Maombi ni ulinzi.
Iv. Maombi ni dawa.
V. Maombi ni afya.

9. UPENYO WA MAOMBI KATIKA KUVUNJA LAANA NA ASILI ZINAZOWATESA WATU.
Zifuatazo ni aina 8 za asili zinazo watesa wanadamu katika sura ya laana, ambazo, kwa njia ya maombi ya ukombozi, na kwa msaada wa uongozi wa roho mtakatifu, 1kor 2:10-14, tunafanikiwa kuponyeka na kuwekwa huru kwa jina la yesu kristo wa nazareth.
Kama kiongozi wako wa; taifa, mkoa, wilaya, kanisa, msikiti, kampuni, shirika, kabila au ukoo anasumbuliwa na asili hizi mbaya, atawasumbua sana. Na nivigumu kutoboza au kustawi kiuchumi, kijamii kiroho na kiutumishi. Tafakari mafundisho haya ili upate maarifa, halafu uyafanyie kazi kuanzia leo kwa faida yako wewe , familia yako na yenu, jamii nzima na kanisa unalolichunga na kulisimamia.
Ukichunguza kwa makini, utagundua, asili hizi mbaya, ndio chanzo cha ufisadi, wizi na rushwa , hapa tanzania na duniani mwote.

ASILI HIZI ZINASUMBUA TAKRIBANI DUNIA NZIMA NA WALE WAKAAO KATIKA USO WA NCHI KUPITIA MAAENEO HAYA YAFUATAYO;
i. Asili na laana ya utaifa.
Ii. Asili na laana ya ukabila.
Iii. Asili inayotokana na namna ulivyo zaliwa.
Iv. Asili na laana inayotokana na siku au tarehe uliyozaliwa.
V. Asili inayotokana na madhabahu za kishetani za ukoo.
Vi. Asili na laana inayotokana na tabia sugu na mbaya ya kifamilia.
Vii. Asili inayotokana na maneno uliyotamkiwa ukiwa tumboni.
Viii. Asili inayotokana na mapito uliyopitia.

I. ASILI INAYOTOKANA NA UTAIFA
ezekiel 16:3 “useme bwana mungu auambia yeerusalemu hivi;asili yako na kuzaliwa kwako kwatoka katika nchi ya mkanaani, mwamori alikuwa baba yako, na mama yako alikuwa mhiti”
kama nchi imefanya uovu fulani, laana inaingia hadi ardhini. Ukizaliwa hapo laana inakutafuna. Ezekiel 22:3-4, “ nawe utasema bwana mungu asema mji umwagao damu ndani yake, ili wakati wake upate kuja, mji ufanyao vinyago juu ya nafsi yake ili ujitie unajisi, umekuwa na hatia ktk damu yako uliyoimwaga, nawe umekuwa unajisi kwa vinyago vyako ulivyovifanyanawe umezileeta karibu siku zako, nawe umefika karibu na miaka yako, basi kwa sababu ya hayo nimekufanya kuwa lawama, kwa mataifa na kuwa dhihaka ktk nchi zote”
kila taifa hapa duniani lina wakilishwa na alama ya mnyama. Mfano; tanzania alama ya mnyama wake ni twiga. Mnyama huyu anashingo ndefu anaona mbali na kutazama wakati mwingine, wenzake wakiliwa na chui, na yeye hachukui hatua yoyote. Hii ni hali ya kuzubaa, hofu na kutojitambua. Nchi ta tanzania imekuwa ikiibiwa rasilimali zake kama; madini, lakini watu walikuwa wakitazama na kusema bila ya kuchukua hatua. Lakini ashukuriwe mungu, tanzania imempata rais; magufuli, aliyeliona hili na kuwarudishia wa-tanzania haki ya kufaidi keki ya taifa.
Alama ya mnyama ya kenya ni jogoo. Hii ni alama iletayo ufuska na ukahaba. Na hili ndilo tatizo la nchi ya kenya kiroho. Alama ya mnyama ya marekani ni ndege aitwaye; tai. Maana ya tai ni ufalme uliotukuka. Ndio maana marekani inatawala dunia; kiuchumi, kisayansi na kijeshi.

II. ASILI INAYOTOKANA NA KABILA ULILOTOKA
ezekiel 16:3 “useme bwana mungu auambia yeerusalemu hivi;asili yako na kuzaliwa kwako kwatoka katika nchi ya mkanaani, mwamori alikuwa baba yako, na mama yako alikuwa mhiti”
kila kabila hapa duniani linasumbuliwa na asili fulani chafu ambayo si njema na inawavunjia heshima na kuwaletea aibu. Mfano: wahehe wanatatizo la kujinyonga, wachaga wanatatizo la roho ya wizi, wapare ni ubaili, wasambaa ni umbea, wasukuma wanasumbuliwa na roho ya uchawi, wakurya ni ukatili na kuua , wangoni uchawi na mizimu, wamakonde wanasumbuliwa na roho za ujinga na ushirikina. Shida hii imelitatiza sana taifa hili, taasisi zake, jamii na makanisa.

III. ASILI INAYOTOKANA NA JINSI ULIVYOZALIWA
zaburi 51:5 “ tazama mimi naliumbwa ktk hali ya uovu, mama yangu alinichukuwa mimba hatiani”
zaburi 58:3 “wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao, tangu tumboni wamepotea wakisema uongo”
ni muhimu kujua haya kuwa; mimba yako ilitungwaje?, kulikuwa na tukio gani siku hiyo? Waamuzi 11:1-3. Kama mama yako yuko hai muulize ili ujue namna utakavyo omba ili ujinusuru. Hii ni kwakuwa; yale yaliyotoke siku unazaliwa, yanahusiana na hatma ya maisha yako, nay ale yanayokupata hivi sasa.

IV. ASILI INAYOTOKANA NA TAREHE AU SIKU ULIYOZALIWA
ayubu 3:1-7
tarehe uliyozaliwa imebeba hatma ya maisha yako. Baadhi ya mambo yanayokupata yanahusiana na tarehe au siku uliyozaliwa. Jiulize maswali haya; siku uliyozaliwa ni siku iliyo barikiwa ulimwengu wa roho au la?. Nyota gani ilionekana angani? Mathayo 2:1-2. Nyota yako ina mvuto kiasi gani?,
mathayo2:9-11. Siku hiyo mwezi ulikuwa na umbile gani?...... Nani walikuwepo

V. ASILI INAYOTOKANA NA MADHABAHU ZA KISHETANI NA ZA UKOO
isaya 60:2, “ maana tazama giza litafunika dunia, na giza kuu litafunika kabila za watu……………………….”
Ezekiel 20:30-34.
Giza kuu linalifunika makabila ni mambiko, maagano ya kishetani ktk makabila na ukoo. Vilevile giza kuu ni kuabudu mizimu na kushiriki mambo ya waganga na wachawi. Mambo haya yote yanaleta madhara makubwa ya kiroho na ya kimwili ktk uso wa nchi.
Maombolezo 5:7 “baba zetu walitenda dhami hata hawako, na sisi tumeyachukuwa maovu yao”
adhabu itakayo shambulia kabila au ukoo ulioshiriki matendo haya ya giza ni: laana, magonjwa, vita, ufukara, kutokufanikiwa ktk utumishi, na kudumaa kwa kihuduma.

VI. ASILI INAYOTOKANA NA TABIA MBAYA
1kor 2:14” mwanadamu ya tabia ya asili hayapokei mambo ya roho wa mungu…….”
Baadhi ya watumishi au waumini wanasumbuliwa na tabia mbaya mbaya kutoakana na asili mbaya ya kishetani iliyo ndani yao. Mfano; tabia ya jeuri, tabia ya ukorofi, kuwa mkali sana, hasira kali sana, na ubishi uliovuka mpaka au kawaida.

VII. ASILI INAYOTOKANA NA MANENO ULIYOTAMKIWA UKIWA TUMBONI.
ezekieli 16:5 “ hapana jicho lililokuhurumia ili kukutendea lolote la mambo hayo kwa kukuhurumia, lakini ulitupwa nje uwandani, kwakuwa nafsi yako ilichukiwa ktk siku ile uliyozaliwa”
maneno uliyotamkiwa siku ile uliyozaliwa, yanahusiana na hatma yako au yale yanayotokea hivi sasa maishani mwako.

Jiulize maswali haya;
a) siku uliyozaliwa wajomba zako walitamka maneno gani?
B) au wakwe zake mama yako walisema nini siku uulizokuwa tumboni?
C) iliposemekana kuwa umezaliwa, watu walifurahi au walichukia?
D) mawifi zake mama yako walikutamkia maneno gani?
Majibu ya maswali haya waweza kuyapata kwa njia ya ufunuo wa roho mtakatifu,fu 1kor 2:10…….. Au fanya utafiti uliize kwa wazazi wako au wakubwa zako walokuwepo siku hizo.

VIII. ASILI INAYOTOKANA NA MAPITO ULIYOPITIA
waamuzi 11:1-4
mapito uliyopitia yanaweza kujenga usugu fulani, na kuamsha asili fulani ya kishetani ndani yako na kuleta maadhara fulani. Mfano:
i. Mateso: yanaathiri mfumo wa akili na saikolojia.
Ii. Kuvuta bangi: akili inaharibika.
Iii. Ulevi: unaleta ufukara na upumbavu.
Isaya 55:6 “mtafuteni bwana maadam anapatikana, mwiteni maadam yu karibu”….
Sasa , kumtafuta mungu aliye hai, inamaana yuko umbali fulani, ulimwengu wa roho. Ni lazima ujue kanuni na maarifa ya kuutafuta uso wa bwana…
anaposema “mwiteni bwana”, maana yake ni kusema; yuko sehemu au mahali fulani, mahali mbapo ukimlilia na kuliitia jina lake, atakusikia… hii nayo yataka ufahamu wa ki-mungu wa kukusaidia kujua namna ya kumwita mungu aliye hai

Math 7:7 "ombeni,nanyi mtapewa,tafuteni nanyi mtaona,bisheni nanyi mtafunguliwa"

1.maombi ni kutafuta,kubisha hodi kwa mungu.luka 18:1 "akawaambia mfano,ya kwamba imewapasa kumwomba mungu sikuzote wala wasikatetamaa"

2.maombi ni kumwendea mungu
ebr 11:6b "kwa maana mtu amwendeaye mungu lazima aamini kwamba yeye yuko,na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao"

3.maombi ni kuzungumza na mungu isaya 1:18 "haya njoni tusemezane,asema bwana wa majeshi,


4.maombi ni kuweka wazi haja/mahitaji yetu mbele za mungu ,filip 4:6 "msijisumbue kwa neno lolote,bali katika kila neno kwa kusali na kuomba,pamoja na kushukuru haja zenu na zijulikane na mungu"

5.maombi ni ibada mbele za mungu..mdo 13:2 "basi hawa walipokuwa wakimfanyia bwana ibada na kufunga,roho mtakatifu akasema,

6.maombi ni kupigana vita vya kiroho,efeso 6:18 "kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika roho,mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu"

7.maombi ni kutulia na mungu isaya 30:15 "kwa maana bwana mungu asema hivi,kwa kurudi na kustarehe mtaokolewa,nguvu zenu zitakuwa katika kutulia na kumtumaini lakini hamkukubali"

KWANINI YATUPASA KUOMBA?? MATH 7.7

1..tunaomba ili tupewe haja zetu, "ombeni nanyi mtapewa",tena neno la mungu linasema wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi,yakobo 4:2 "mwatamani wala hamna kitu,mwaua na kuona wivu,wala hamwezi kupata,mwafanya vita na kupigana,wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi"
2.ni agizo kutoka kwa yesu..luka 18:1 "akawaambia mfano,ya kwamba imewapasa kumwomba mungu siku zote,wala wasikate tamaa"
1thes 5:17 "ombeni bila kukoma"

3.kwa sababu kuomba ni huduma..huponya taifa,familia,kanisa na watu wanaponywa magonjwa na shida zao na kazi yake jehova hufanikiwa
2nyak 7:14 "ikiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu,watajinyenyekesha,na kuomba na kunitafuta uso na kuziacha njia zao mbaya basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao"

4. Isaya 59:16 "akaona ya kuwa hapana mtu,akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi basi mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu na haki yake ndiyo iliyomsaidia"
yak 5:14-16 "mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa nao wamwombee na kumpaka mafuta kwa jina la bwana na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule na bwana
Atamwinua hata ikiwa amefanya dhambi atasamehewa ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi,na kuombeana mpate kuponywa,kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa bidii"

5..kwa sababu ya kujenga mahusiano yetu karibu na mungu
yak 4:8 "mkaribieni mungu naye atawakaribia ninyi,itakaseni mikono yenu enyi wenye dhambi na kuisafisha mioyo yenu,enye wenye nia mbili"

6..kwa kuwa mungu ni baba na sisi ni watoto wake,yatupasa kumwomba haki zetu tukiwa kama watoto..
Math 6:9 "basi ninyi salini hivi,baba yetu uliye mbinguni,jina lako litukuzwe,ufalme wako uje"

MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (1)
Wako wakristo ambao tunashindwa kuwa na maisha ya maombi kwa sababu zifuatazo.
(1) kukosa muda wa kuomba kwa sababu ya majukumu ya muhimu ya hapa na pale.
(2) mazingira ya mtu anapoishi.
(3) mwingine hajui faida za maombi wala umuhimu wake.
(4) mwingine anasema huwa anaishiwa maneno kwa haraka anapokuwa kwenye maombi.
(5) mwingine hapendi maombi tu!
(6) shetani.
(7) mwili.

KATIKA MAOMBI KUNA VIKWAZO VINGI, KWA SABABU MAOMBI YANA NGUVU!
(a) maombi yanaongeza uhusiano wa mtu na mungu!
Maombi ni mawasiliano baina ya mwanadamu na mungu au ni njia ambayo tunaweza kuwasiliana na mungu. Tunafanya mawasiliano na mungu kwa njia ya maombi, na kama tunavyojua kwamba! Mawasiliano yanaongeza uhusiano wa mtu na mtu, hata wewe ni shahidi katika hili! Unaweza ukawa na ndugu wengi sana au marafiki wengi sana n.k. Lakini yule ambaye atawasiliana na wewe mara kwa mara huyo ndiye anayeukuza ukaribu kupita wengine. Na pia uhusiano wa mtu unaanzishwa kwa mawasiliano na vilevile unaweza ukafa au kupungua kwa kukosa mawasiliano ya mara kwa mara na kuelekezwa kule kwenye mawasiliano ya mara kwa mara! Mawasiliano yamewafanya watu wengi kuwa karibu, kupitia mitandao yetu. Mtu alipoanza mawasilano na wewe kwa njia ya kukutumia ujumbe wa maandishi au wa picha ulipojibu! Mawasilano yakakua mwisho wake ukaribu ukaongezeka kati yako na huyo….
Tunapokuwa tunaomba mara kwa mara uhusiano wetu na mungu unakuwa kwa kasi sana kuzidi yule asiyeomba, au yule anayeomba mara moja moja au yule anayeomba kwa viwango vya juu zaidi! Na kama tujuavyo, kadiri uhusiano wa mtu na mtu unavyokuwa na kuongekezeka ndivyo wanavyoweza kushirikishana mambo mengi saaaana!
Ndivyo inavyokuwa kwa mungu kwetu! Kwa sababu mahusiano yetu yanakuwa na kuongezeka! Mungu hataacha kutushirikisha mambo mengi yanayoendelea ili kuyaombea au kuzuia yasitokee au kuwashauri watu n.k. Mungu atatuonyesha hata hatari iliyopo mbele yetu, kwamba! Kuna ajali mbaya itatokea na kusababisha hiki na hiki na jinsi ya kuikwepa n.k. Yakiambatana na maelekezo yake jinsi ya kufanya ambayo yatakuwa na lengo la kujenga na si kubomoa! Utakuwa na furaha na amani wakati woote hata kwenye dhiki za namna gani! Sijui nitumie lugha gani nieleweke jamani: ili uelewe hili na kulishika kwamba! Maombi yanaongeza uhusiano wa mtu na mungu!
Tuanze maisha ya maombi kuanzia sasa ili uhusiano wetu na mungu ukue, anzisha mahusiano yako na mungu kwa kuwasiliana naye mara kwa mara kwa njia ya maombi. Hata kama zamani tulikuwa na bidii ya kuwasiliana na mungu kwa njia ya maombi halafu tukayakata mawasilano hayo! Bado tunaweza kuyaanzisha upya na kuyakuza! Pia usiache kuwasiliana na mungu mara kwa mara kwa njia ya maombi kwa sababu kwa kutofanya hivyo utauvunja au utaupunguza uhusianao wako na mungu!

 MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 2)
Kwa nini tunazuiwa kuomba? Pamoja na sababu nyingine zinaonekana kama ni za msingi! Angalia hii!
(b) maombi yanaweza kubadili maamuzi ya mungu aliyoyapanga kwa taifa au kwa mtu n.k.
Hii tunaipata kwa nabii isaya! Tusome maandiko haya kwa makini saaana! Isaya 38:1 “siku hizo hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na isaya nabii, mwana wa amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, ‘bwana asema hivi, tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa,wala hutapona’.”
Ni ujumbe kutoka kwa nabii! Mungu mwenyewe hapo anasema kwamba “utakufa”, hebu jaribu kufikiri! Ingekuwa wewe mungu anakwambia hivyo ungefanyaje? Lakini mfalme huyu alijua hata kama mungu amesema, bado ninaweza kubadili maamuzi yake kwa sasa kwa njia ya maombi! Alichokifanya mfalme ni hiki! Isaya 38:2 “basi hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba bwana..hezekia akalia sana sana.” Hezekia alijua na aliamini kwamba maombi yanaweza kubadili maamuzi ya mungu kabisa! Baada ya maombi hayo angalia kilichotokea. Isaya 38:4, “ikawa, neno la bwana likamjia isaya, kusema, enenda ukamwambie hezekia, ‘mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako…”. Hapo kuna vitu viwili mungu aliviangalia wakati hezekia anaomba,
(1) kuomba kwa imani. “ikawa, neno la bwana likamjia isaya, kusema, ‘enenda ukamwambie hezekia, mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako.” (isaya 38:4).
(2) machozi yaliyoambata na kuomba, japokuwa wako watu huwa wanasema walokole wanalialia, tunalia ili mungu ayapokee maombi yetu, sisi hatulii kama hao waliliao mapenzi usiku na mchana!
Maombi hapa yaligeuza maamuzi ya mungu, nafikiri sasa unaweza kuelewa kwa nini tunazuiwa kuomba. Ndugu kama unaomba; hata kama ni nani alitamka kitu gani kwako, au katika ukoo wako kwa kulaani laana zozote zile, unakuta familia nyingine hakuna maendeleo yoyote yale pamoja na bidii zote za kufanya kazi na kusoma! Hakuna kuoa wala kuolewa n.k. Maombi yana uwezo wa kubadilisha laana na kuwa baraka na kufumua fumua kila vitu vibaya vinavyohusika kutukandamiza na kutudidimiza katika maeneo fulani fulani. Hata kama bosi alisema nitakusimamisha kazi, maombi yanaweza kubadili maamuzi ya bosi! Kama maombi yaliweza kugeuza maamuzi ya mungu sembuse bosi ? Sembuse rais wa nchi?
Twende kwenye mfano wa pili uone maombi ambavyo yanakitu cha kipekee.
Hapa sasa tunaona ibrahimu ambavyo alikuwa anawashawishi malaika waliotumwa na mungu kwa ajili ya kuiangamiza sodoma na gomora. Mwanzo18:32. “je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu wala hutaacha mji.hasha usifanye hivyo,…bwana akasema, nikiona katika sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha kwa ajili yao.”
Ibrahimu aliendelea kusema na wale malaika mpaka akafikia hesabu ya watu 10! Na ibrahimu akaishia hapo, kama ibrahimu angeendelea kusihi bila shaka maangamizo yasingetokea. (mwa 18:30-32). Zaidi sana walichokifanya malaika ni kumuondoa lutu na mkewe na wanawe ambao inaonyesha hawakufika 10 kama wangekuwa 10 wasingetolewa ili mji uangamizwe kwa sababu ibra alifanya maombi na yakajibiwa kwamba kwa idadi ya watu 10 tu na kama hao 10 wangekuwepo sodoma na gomora isingeangamizwa, wangeachwa na mungu angetumia njia nyingine! Maana alisema kama wamgekuwa 10 asingeuangamiza mji.                                                                                                                
Maombi ni ni kumshawishi mungu kufanya yale ambayo wewe unataka ambayo yatakuwa ndani ya mpango wake. Kama maombi yanaweza kubadilisha maamuzi ya mungu; sembuse kubadilisha maaumuzi ya mtu? Ndio maana sijatoka kuzungumzia mifano ya maamuzi ya wanadamu yalivyobadilishwa baada ya maombi, nimezungumzia upande wa mungu ili uone maombi ambavyo yana nguvu! Kuna kitu gani umetamkiwa? Kuna kitu gani unakitaka? Muombe mungu kwa imani!

 MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 3)
(c) kuwaacha watu na kwenda kuomba!
Hili ni tendo la ajabu sana ambalo yesu alilifanya! Lilikuwa ni fundisho kwetu! Hebu jaribu kufikiri; kwa jinsi yesu ambavyo ana kila kitu, lakini pamoja na yesu na kuwa na kila kitu, lakini alijua pasipo maombi yote aliyokuwa nayo haiwezekani! Yesu mwenyewe alikuwa anajua hapa bila maombi hamna kitu! Alifikia mahali anawaacha makutano halafu anakwenda kuomba. Luka 5:12-16. Hebu tusome mstari wa 16.
“lakini yeye alikuwa akijiepua,akaenda mahali pasipokuwa na watu,akaomba.”
Hapo yesu anawakimbia makutano na kuelekea zake kwenye maombi, japokuwa ni ngumu sana kwa baadhi ya watu kuwaacha watu na kwenda kwa kuomba katika mazingira kama haya ya yesu, kwao ni utukufu. Ikiwa yesu alifanya hivyo, sisi tunapaswa kufanya hivyo na kuzidi kulingana na maisha yetu na dunia ya leo, lakini leo mtu anasema hana muda wa kuomba, eti kazi zinambana, na kwa sababu nyingine zinazofanana na hizo, lakini bado mtu huyohuyo ambaye anasema hana muda wa kuomba huyo huyo unaweza kumuona katika makundi ya watu au marafiki akiongea muda mrefu, lakini hao hao wanaosema hawana muda wa kuomba ni watu hodari sana kwa kuchat, hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuchat na watu kwa njia ya whatsapp, muda wote anafanya kazi huku yuko whats app! Hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuongea na watu kwenye simu masaa na masaa, hana mua wa kuomba lakini anaangalia movie masaa na masaa; hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuangalia mpira …ninaweza kusema huyu hana muda wa kuongea na mungu lakini ana muda wa kuongea na watu! Kwa sababu maombi ndiyo kuongea na mungu.
Kuongea na watu si vibaya; si vibaya kuchat na watu kwa njia mbalimbali za mitandao, lakini ni mbaya kama tuna muda wa kufanya hivyo lakini hatuna muda wa kuomba! Ni mbaya sana! Sana ! Inatakiwa ifikie mahali tunaongea na watu lakini ukifika muda fulani tunajiepua na kwenda mahali kusikokuwa na watu au mahali ambapo tutaweza kuomba bila buguza! Hapa yesu hakwenda kanisani! Maombi tunaomba popote pale kama mazingira hayaturuhusu kwenda kanisani, tukipata nafasi tu kidogo tu; tunaomba hata kimoyomoyo! Kuomba sio lazima iwe kanisani.
Bila maombi tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki! Maisha ya uhitaji wa kupitiliza na kujikuta kwenye madeni wakati wote, ukiondoa maombi hata unahubiri kila siku lazima iko siku utaanguka tu! Lazima! Tuache mambo ya kukaa kaa na watu na kuongeaongea muda mwingi tunaumalizia kwa watu. Tena wakati mwingine mambo mengine hayana hata maana, tunaopoteza kuongea na watu ambao hata tukienda kulala hata hawajui yanayotusibu katika usingizi wetu. Hawana sifa ya kuongea na sisi kabla ya kuongea na mungu wetu! Kama yesu aliomba mwenye huduma kubwa kuliko huduma yako wewe ambaye unalewa na sifa za watu lakini kuomba hutaki! Sisi tutapona? Shetani alikuwa hana kitu kwa yesu lakini bado yesu alikuwa anaomba. Tusidanganywe na sifa zinazotoka vinywani mwa watu.
Tuweke ratiba kwamba! Kuanzia muda fulani ni muda wa maombi. Hapo hata simu ipigwe hakuna kupokea, tunakwenda mahali pasipokuwa na watu kifikra! Yesu alikwenda sehemu halisi! Lakini kama mazingira yetu hayaturuhusu kufanya hivyo, tunapaswa kwenda mbali na watu kifikra! Wakati wa kuomba ikiwezekana zima simu yako au weka silent kama simu yako ndio kila kitu! Nikiwa na maana kuna bible n.k.
Yesu naye tungesema hana muda, kwa sababu pale alikuwa kazini! Lakini alijua umuhimu wa maombi! Kama wewe huna muda usile chakula basi! Kinachokufanya ule nini wakati huna muda?
Nb: maombi ni kwa faida yetu wenyewe

 MAISHA YA MAOMBIKWA MKRISTO (PART 4)
(d) maombi yanatupa nguvu ya kutoingia majaribuni!
Yesu aliwawaambia wanafunzi wake maneno haya kwa uzito sana baada ya kuona wanafunzi hawana maisha ya maombi! Walikuwa wanafikiri jukumu la kuomba ni la yesu tu! Kama sisi tunavyofikiri sasa, kwamba jukumu la kuomba ni la watu fulani tu, na si la kwetu! Kila mahali ambapo yesu alikuwa anaomba wanafunzi wake ambao leo tunawatambua kama mitume! Walikuwa hawana maisha ya maombi. Angalia hapa luka 9:28-32,
“baada ya maneno hayo yapata saa nane, akawatwaa petro na yohana na yakobo, akapanda mlimani ili kuomba (hilo ndio lilikuwa lengo lakini angalia matokeo yake).ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka….”. (hapa yesu anaomba peke yake wale aliopanda nao walishamwacha walikuwa na usingizi). Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi:lakini walipokwisha amka…”
Inaonyesha wazi walikuwa wamelala wakati yesu anaomba! Walikuwa wanaona shida kuomba kama sisi tunavyoona shida! Lakini tatizo lilikuwa linajirudia tena na tena kwa wanafunzi mpaka ikabidi yesu awaambie madhara ya kutokuwa na maisha ya maombi! Hapa lilikuwa tukio jingine sio lile la mlimani! Mathayo 26:40-41,
“akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia petro, je! Hamkuweza kukesha nami hata saa moja?.kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni.”
Sio toeni sadaka ili msiingie majaribuni, sio hubirini sana ili msiingie majaribuni, hapa yanatajwa maombi pekee. Kinyume chake hatutaweza kukabiliana na majaribu, tutashindwa bila shaka. Maombi ndio yananifanya mimi na wewe kutoingia majaribuni, majaribu yamejaa kila kona katika dunia ya leo, lakini tutawezaje kuyashinda kama hatuna maisha ya maombi? Hatutaweza kamwe! Kamwe! Yesu akishasema amesema! Mtu yeyote ambaye hana maisha ya maombi ana maisha ya kuingia majaribuni! Mtu ambaye kuomba anaona shida; mtu huyo haina haja ya kupeleleza maisha yake. Jibu lake linajulikana ni mtu wa kuingia majaribuni na matokeo yake anajikuta anaishi maisha ya unafiki! Anaonekana anahubiri na kufundisha, anaoneka anapost vitu vya kutia moyo, anaonekana anaombea watu, lakini maisha yake ni ya kujilaumu wakati wote hana uwezo wa kushinda majaribu. Ndugu yangu hata kama sisi tunajiita mtume nabii hata kama! Hata kama tunajulikana vipi kiuimbaji na kukubalika katika nyimbo za injili, sifa na kuabudu, kama hatuna maisha ya maombi majaribu yakija lazima tutaingia majaribuni! Hatutaweza kushinda hata siku moja! Leo tunaweza tukajipiga piga vifua kama petro,na kusema, “mimi nimuache yesu”. Ukisalimiwa “mambo”, unajibu “mambo kwa yesu”. Misimamo hiyo kama huna maisha ya maombi lazima siku moja utaingia majaribuni tu! Misimamo bila maombi! Hakuna matokeo ya ushindi.
Namkumbuka binti mmoja ambaye alikuwa ameokoka! Binti huyu tulikuwa tunaishi naye jirani! Binti alikuwa na misimamo ya hatari sana! Ilikuwa tukimsalimia “mambo?”. Aanajibu “mambo kwa yesu.” Alikuwa hajibu kwa mizaha! Alikuwa hataki mchezo mchezo ukizingatia pia kwao pesa zipo na wakati huo yupo kidato cha tatu! Mimi wakati huo nilikuwa mbali na ufalme wa mungu! Misimamo ya binti huyu haikudumu kwa sababu hakuwa na maisha ya maombi! Akaangukia kwa muuza mitumba na uwokovu akauacha! Akakataa shule wakati huo tayari ameshaanguka tayari; wakati hilo halijaisha vizuri mimba ikaingia akamwacha yesu! Misimamo bila maisha ya maombi ninakuambia waziwazi wewe binti ambaye unajulikana shuleni kwako unaposoma, chuoni kwako au kazini kwako, bila maisha ya maombi unaweza kujikuta unaanguka mahali usipoptarajia.
Yesu alimwambia petro waziwazi katika mathayo 26:34-35, “…yesu akamwambia, ‘amin, nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Petro akamwambia, ‘ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe.’”
Petro anajigamba wakati hana maisha ya maombi; muda wa maombi yeye anasinzia, na ndivyo ilivyokuwa, alimkana yesu kwa kiapo na alisema mathayo 26:69-74, “ndipo alipoanza kulaani na kuapa na kusema, simjui mtu huyu.” Unaona, anasema “mtu huyu.”  Wakati petro alikuwa ananyenyekea kwa bwana! Alikuwa anamuita yesu bwana! Lakini hapa anasema “mtu huyu “. Ndivyo ilivyowatokea wengine ambao walipuuza maombi, leo ukiwaona utashangaa! Unajiuliza huyu si alikuwa moto wa kuhubiri, kuomba, kutoa, kuimba n.k.! Peleleza maisha yake kabla, utakuja gundua alikuwa hana maisha ya maombi! Na ndivyo itakavyotokea kwetu kama hatutakuwa na maisha ya maombi, ninakuambia wazi kabisa utashindwa tu!
Ndugu yangu omba! Omba! Omba! Ndani ya maombi ndio kuna nguvu ya kutuwezesha kushinda ushawishi huu uliotanda kila kona katika dunia, kila siku inafunguliwa mitandao mipya ya kuturahisishia kufanya mambo mema na hapohapo ya kuturahishia kuingia majaribuni! Tutawezaje kushinda vishawishi kama hatuna maisha ya maombi? Tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki na mwisho ya siku tutamwita yesu “mtu ” badala ya “bwana” kama ilivyotokea kwa petro! Tusipoomba kuingia majaribuni sio jambo la kutafuta! Mtu yeyote ambaye hana maisha ya maombi, mtu huyo hawezi kujizuia katika majaribu, kama sivyo yesu tunamfanya yesu kuwa ni muongo, na kamwe yesu hawezi kuwa muongo!
Nb: maombi ni kwa faida yetu wenyewe, tukiacha kuomba kwa sababu zozote kumkana yesu kuko karibu! Omba! Omba! Omba!

 MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 5)
Mambo ya kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu tunapokuwa katika maombi.
(1) hatupaswi kuwa na mashaka yoyote!
Maandiko yanasema katika yakobo 1:5-7,
“…ila naombe kwa imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye mashaka ni kama wimbi la bahari la bahari lililochukuliwa na upepo,na kuleperushwa huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa bwana.”
Hayo ndiyo maandiko! Hata kama tunaomba masaa 100 mfululizo, hata kama tunaomba kwa viwango vya vinavyoonekana vya juu sanaa kibinadamu, lazima maombi yetu yawe ndani ya kanuni, lazima tuombe pasipokuwa na mashaka tena mashaka yoyote! Hayo ndio maandiko hakuna njia ya mkato; kama tunamuomba mungu lakini tuna mashaka moyoni au vinywani hilo ni tatizo linalopelekea kutopokea majibu yetu ya maombi! Kwa nini nasema mtu anaweza akawa na mashaka moyoni. Mtu mwingine anaweza akaonekana ana imani katika mazungumzo yake, hasa pale anapokutana na watu , lakini ndani ya moyo wake kumejaa mashaka, na mashaka hayo mungu huyaona pale mtu anapokuwa peke yake katika fikra au pale mambo yanapokwenda kinyume na alivyotarajia kutokana na maombi yake! Akizungumza na watu ni kama amejaa imani! Lakini moyoni kumejaa mashaka makubwa! Mashaka ni ile hali ya wasiwasi ya kutokuamini. “hivi kweli mungu inawezekana kweli? Itakuwa kweli? Mungu ananisikia kweli?” N.k.
Hayo yote ni mashaka na kwa mashaka hayo kamwe hatutaweza kupokea majibu yetu ya maombi! Kamwe! Tukiruhusu mashaka hata kama ni kidogo tunaambiwa waziwazi, “maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kutoka kwa bwana.” Yaani, hata ile kudhani, kutegemea, kufikiri, isiwepo. Mashaka ni adui mkubwa sana anayeshindana na majibu ya maombi yetu yasitufikie.
Wakati mwingine mashaka yanakuwepo baada ya kuomba kitu muda mrefu na kutoona majibu ya maombi! Wakati mwingine inatokana na kuona mambo yanakuwa mabaya zaidi kuliko mwanzo! Au uzito wa jambo pia linaweza kuchangia kukaribisha mashaka na hata shetani pia anahusika lakini anapitia maeneo hayo hayo!
Ili tuone majibu ya maombi yetu yakiwa dhahiri, hatupaswi kuruhusu mashaka yoyote hata kidogo! Tukishaomba tu! Mawazo yetu yanapaswa kufikiri sawasawa na majibu ya maombi yetu, kusema kwetu kuendana na majibu yetu ya maombi kwa imani, inaweza kuwa sio rahisi kuishi hivyo haiwezi kuwa rahisi hata kidogo! Na hakuna mbadala wake lazima mashaka yasiwepo ili tupokee majibu yetu ya maombi! Tunamuomba mungu kwa sababu sisi hatuwezi, tumeshindwa ndio maana tunaomba! Kama mtu unawashwa mgongoni utamwomba mungu “niwezeshe kujikuna?” La! Tutajikuna kwa sababu jambo hilo liko ndani ya uwezo wetu!
Tunapomuomba mungu maana yake sisi hatuwezi, tumeshindwa! Rahisi kufikiri nguvu za mungu hazipo; rahisi kufikiri ukimwomba mungu basi majibu yanachukua muda mrefu! Hatupaswi kuyaruhusu mawazo hayo kufanya kazi ndani yetu kamwe! Sisi tunachotakiwa kuamini mungu yupo na anajibu maombi na hakuna gumu la kumshinda! Mashaka yanapokuwa yanakuja kwa njia zozote zile, iwe kupitia watu kwa maneno yao; n.k. Hatupaswi kuyaruhusu kwa sababu, tukiruhusu mashaka maandiko yanasema tusitarajie kupokea kitu kutoka kwa bwana!
Kuna wakati yesu alikuwa anatembea juu ya bahari! Na petro akaomba atembee au apewe uwezo na yesu wa kutembea juu ya bahari! Yesu akayajibu maombi yake na akamwambia petro atembee…lakini petro aliporuhusu mashaka baada ya kuuona upepo, akazama mbele ya yesu! Yesu akamuokoa kwa kumshika mkono sio kwa kumuombea bali alimshika mkono na akamwambia! (mathayo 14:26-31.31):
“mara yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, ‘ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?’”
Unaona hapa! Petro anazama mbele ya yesu kwa sababu aliruhusu mashaka, na sisi sio kama tukimuomba mungu kitu fulani basi kinakuwa mtelemko! Inaweza ikatokea upepo mkali kwenye biashara zetu kwa viwango vya kuporomosha kabisa mitaji yetu! N.k. hatutakiwi kuwa na mashaka katika hali yoyote! Tusimamie matokeo tusiangalie mazingira tuliyonayo kwa sasa, tukiwa na mashaka tutazama tu hata kama yesu yupo ndani mwetu!
Wakati wote tunapomuomba mungu, tuombe bila mashaka yoyote yale! Mungu yupo na nguvu zake zipo vilevile! Hata mimi nikikufanyia maombi na ukaanza kuona matokeo, yaani, unatembea juu ya bahari kama petro! Lolote likitokea kama upepo likiwa na lengo la kubadilisha hilo, hupaswi kuwa na mashaka unapaswa kuendelea kuamini! La sivyo utazama kama petro na kuupoteza muujiza wako! Kama petro alizama mbele ya yesu kwa sababu ya kuruhusu mashaka! Sembuse mwanadamu anayeitwa….. .
Yakobo 1:5-6,
“…ila naombe kwa imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye mashaka ni kama wimbi la bahari la bahari lililochukuliwa na upepo, na kuleperushwa huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa bwana.”
Tumwombe mungu atuongezee imani atupilie mbali mashaka yaliyomo ndani mwetu na atupe kuyashinda kila yanapoinuka. Hata kama maombi yetu yatachukua muda mrefu bila kuona majibu yake, bado hatupaswi kuruhusu mashaka, tena mashaka yoyote yale.

 MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO ( 6)
Mambo ya kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu, tunapokuwa katika maombi.
(2) kuomba vibaya ili tuvitumie kwa tamaa zetu!
Tunaweza tukawa kweli tunaomba, tunaomba ili tupate kazi fulani, tunaomba mungu atutumie tukiombea watu wapone na mungu akutane na haja zao! Mwingine anaomba apate nyumba nzuri, mwingine gari, honda, n.k. Yote haya ni mema, lakini kama mtu anaomba moyoni kumejaa nia nyingine (kama uchoyo au kiburi), moyoni anasema au anawaza kwamba, “nikipata gari ninalolitaka, watu watanikoma.” “nikipata pesa hee! Watanitambua”, n.k.
Mwingine ni kipofu tangu kuzaliwa anamuomba mungu lakini moyoni anawaza au anasema, “sijawahi kuona mwanamke tangu kuzaliwa kwangu, nikiona sijui itakuwaje watanikoma, maana naishia kusikia tu na kuhisi” unaona! Mtu anaomba lakini moyoni mwake anawaza nikikipata nitakutumia hivi au vile, matumzi yenyewe ni nje ya mpango wa mungu. Ndugu yangu hapo tutaomba na kuombewa lakini kamwe hatuwezi kupokea majibu ya maombi! Tunataka mtoto lakini hatujaoa/hatujaolewa wala hatutaki kusikia habari za kuoa au kuolewa!
Mwingine anataka mungu amtumie lakini moyoni mwake kumejaa mashindano ya dhahiri, anawaza kumzidi yule, mwingine anataka sifa tu! Mwingine anawaza utajiri kwamba nitakuwa napata sadaka nyingi za watu n.k. Maandiko yanasema katika yakobo 4:3,
“hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.”
Unaona maandiko hayo? Kama tunamuomba mungu tukiwa na hali hiyo! Kamwe hatuwezi kupokea majibu ya maombi. Ni kupoteza muda tu! Na mwisho wa siku tunaona kama mungu hayupo; mungu yupo na anajibu maombi! Tatizo lipo kwetu tu! Tunaomba ili tukipata tuvitumie vibaya! Kama tunataka kumuona mungu lazima tuzingatie tunaomba ili tuvitumiaje? Nje ya mpango wa mungu! Tuko watu wengi tunaomba na kufikia wakati tunafunga! Lakini tunaomba ili tuvitumiaje hivyo tunavyovitaka kwa njia ipi?
“hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.” Yakobo 4:3.
Kuomba tunaomba kweli! Lakini hatupati kwa sababu tunaomba vibaya ili tuvitumie kwa tamaa zetu! Tangu wakati huu tuhakikishe nia zetu zinakuwa safi mbele za mungu ili tuyaone majibu yetu ya maombi na nguvu ya maombi! Maombi yana kanuni zake na ikiwa mtu anataka kumuomba mungu na kumuona mungu dhahiri akijidhihirisha kwake binafsi hatuna budi kuzingatia yote tunayopaswa kuyazingatia.
Lolote tunaloliomba lazima tangu moyoni huko ambako mungu anaanza nako kwa kumuangalia mtu anataka hili ili iwe nini? Mwingine anatumia pesa kunyanyasa watu, mungu huwa hamuinui mtu ambaye ana visasi, yaani mungu akinipa hivi fulani atanikoma! Kila anachofanya mungu ni kwa utukufu wake tu sio kwa utukufu wa mtu yeyote.

MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (7)
Mambo ya kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu, tunapokuwa katika maombi.
(3) hatupaswi kukata tamaa na kuachia maombi njiani baada ya kuona tunaomba muda mrefu bila kuyaona majibu yetu ya maombi kwa dhahiri!
Hakuna sehemu ngumu inayotushinda watu wengi kama hii! Watu wengi tunataka tukishaomba tu; basi tupokee majibu yetu ya maombi muda huo huo! Mungu hafanyi kazi hivyo ndugu yangu! Mungu ni wa utaratibu sana! Tunapomuomba mungu tunatakiwa kuamini kwamba imekuwa. (matha 7:7).
Hilo ndilo la kuliamini na kulishikilia wakati wote, haijalishi majibu yetu ya maombi tutayaona lini, sisi tuamini kwamba mungu ametenda huku tunaendele kumwomba mungu mpaka liwe dhahiri lile tunaloliomba. Mungu aliumba mbingu na nchi kwa muda wa siku 6, (mwa 1:1). Unafikiri kwa uwezo wa mungu! Kwa nini hakutumia siku moja tu kufanya kila kitu? Je! Hakuwa na uwezo huo? Uwezo upo mkubwa tena sana – mungu ni wa utaratibu sana, ana nguvu ana uwezo lakini ni wa utaratibu mno! Mnoooo! Mbona basi wewe na mimi tunakata tamaa mapema hivyo na kuacha kuendelea kuomba! Tunaona mungu hatusikii ni kama anawasikia wengine! Ni kama ana watu wake maalumu na sio sisi? Hatupaswi kuwaza hivyo hata kidogo, na tusiyape nafasi mawazo hayo! Tunapaswa kuendelea kung’ang’ania mbele za bwana mpaka tuone majibu yetu ya maombi yawe dhahiri. Maandiko yanasema katika luka 18:1,
“akaawambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba mungu sikuzote, wala wasikate tamaa”.
Hayo ni maandiko! Mungu anatambua kwamba! Mtu anaweza akaomba jambo na likachukua muda mrefu na mpaka mtu anafikia mahali kukata tamaa na kuacha kuomba, ndio maana inatajwa hapo “wala wasikate tamaa”.
Uwezekano wa kuchelewa kuyaona majibu yetu ya maombi unawekwa wazi na bwana mwenyewe, lakini hatupaswi kukata tamaa! Marufuku kukata tamaa, usikate tamaa! Endelea kuomba, usiachie njiani hata kidogo! Usiwaze “ooh! Labda kuna makosa nimeyafanya, labda nimefanya dhambi.” Kwani ukifanya dhambi hujui? Maandiko yanasema! 1 petro 5:6, “basi nyenyekeeni chini ya mkono wa mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake”. Kumbe kuna wakati wa mungu! Wakati wa mungu ni mzuri ndugu kuliko wakati wetu sisi! Mungu ndio anajua wakati mzuri wa kukupa jibu lako la maombi! Usione unakawia, wakati wako ndio unakawia, lakini wakati wa mungu ni bora saaana! Mungu anajua wakati gani ukipata kazi utakuwa mzuri kuliko wakati fulani; mungu ndio anajua wakati gani ukipata mtoto utakuwa mzuri zaidi! Wewe unataka mtoto sasa lakini mungu akiangalia anona sasa sio salama! Unataka mungu akutumie kwenye hili au lile n.k. Sisi tuendelee kumlilia bwana! Kupokea ni lazima! Kukata tamaa ni marufuku! Hatupaswi kukata tamaa kamwe! Tuyashinde mawazo ya kutukatisha tamaa! Mungu yupo na anajibu maombi.

 MAISHA YA MAOMBI KWA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 8)
Mambo ya kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu,tunapokuwa katika maombi.
(4) Tunapaswa kuwa na imani kwamba mungu yupo na anatusikia na anajibu maombi!
Ndugu yangu, hata kama tutaomba na kujigalagaza na kulia kwa uchungu mpaka kutoka makamasi! Lakini kama hatuna imani ni buuure, bure!

IMANI NI NINI? Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana na mambo yasiyoonekana, waebrania 11:11. Hiyo ndio imani! Tunaomba tunatarajia kupokea, sasa imani ni kuwa na uhakika kwamba! Hiki ninachikiomba kinakwenda kuwa sawasawa na nilivyoomba! Imani huwa haingalii mtu wala huwa haijilinganishi na mtu yeyote! Imani inaangalia uwezo wa mungu tu na neno lake basi! Imani haingalii mazingira n.k. Imani inaweza kukufanya wewe kuwa wa kwanza kukipata hicho unachokiomba! Maandiko yanasema,
“lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” (waebrania 11:6).
Tunatakiwa kuwa hivyo tunapokuwa tunamuomba mungu, tusiombe ili mradi tu, tusiombe ili kutimiza wajibu tu, tusiombe kwa desturi na mazoea! Kwa kufanya hivyo tutadangayika kwamba hakuna nguvu yeyote katika maombi, kumbe ni uongo wa ibilisi tu. Tunapaswa kumuamini mungu tunapokuwa tunaomba! Na imani pasipo matendo imekufa! Baada ya maombi lazima uonyeshe matendo na sio unalala tu na kupigapiga soga na watu! Lazima ufanye matendo kama ni kazi tafuta kazi n.k.
Kutokuwa na imani ni dhambi vilevile! Ndugu yangu inawezekana umekuwa una muomba mungu kwa muda mrefu lakini huna imani! Yesu alikutana na vipofu,angalia hapa! “yesu alipokuwa akipita kutoka huko,vipofu wawili wakimfuata wakipaza sauti. Yesu akawaambia, ‘mnaamini kwamba naweza kufanya hili?’ wakamwambia, ‘naam bwana.’ ndipo alipowagusa macho yao yakafumbuka.” Mathayo 9:27-30.
Unaona hapo? Baada ya kusema wanaamini ndipo yesu alipowajibu majibu yao kwa kuwafumbua macho yao! Na hakuwafumbua macho kabla ya kujibu kwamba anaweza! Kabla ya kuionyesha imani yao! Na sisi mungu anatuuliza kila tunapomuomba! Je! Tunaamini kwamba anaweza kufanya hilo au hayo tunayomuomba? Kila tunapoomba swali linakuja katika ulimwengu wa roho kwako binafsi, “je! Unaamnini naweza kufanya hili?”
Imani ni lazima tunapokuwa katika maombi!

MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (PART 9)
Mambo ya kuzingatia tunapokuwa tunamuomba mungu, tunapokuwa katika maombi.
Sehemu ya 9 na mwisho kwa somo hili!
(5) DHAMBI
Maandiko yanasema katika kitabu cha isaya,
“tazama, mkono wa bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si nzito,hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafirikisha ninyi na mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone hata hataki kusikia.” (isaya 59:1-2).
Kama tunafanya dhambi, mungu kamwe! Hawezi kutusikiliza. Kamwe! Lazima maisha yetu yampendeze yeye tunayemuomba ili atupe kile tunachomuomba! Tunapaswa kuhakikisha dhambi kwetu ni mwiko kabisa kuzifanya wala kuziwaza! Tukiwa hivyo tunauhakika wa wazi wa kupokea majibu yetu ya maombi! Na hivi ndivyo ninavyohitimisha somo la maisha ya maombii! Maandiko yanasema katika isaya 53:1,




Kwa nini tuombe?
Kwa mkristo, maombi ni kama kupumua. Ni rahisi kufanya kuliko kutofanya. Tunaomba kwa ajili ya sababu mbalimbali. Kwa sababu moja maombi ni njia ya kumtumikia mungu (luka 2:36-38) na kumtii. Tunaomba kwa sababu mungu anatuamuru kuomba (wafilipi 4:6-7). Maombi yamedhihirishwa kwetu na yesu pamoja na kanisa la kwanza (mariko 1:35; matendo ya mitume 1: 14; 3:1; 4: 23-31; 6:4; 13:1-3). Kama yesu aliehesabu kuwa maombi ni kitu cha maana, pia nasi lazima. Kama aliitajika kuomba ili asalie katika mapenzi ya baba yake, je tunahitajika kuomba kiazi gani?

Sababu nyingine ya kuomba ni kuwa mungu anataka maombi yawe njia kupata suluhisho lake kwa hali zetu. Tunaomba tukijiandaa kufanya maamuzi muimu (luka 6:12-13); ilitushinde vizuizi vya shetani (mathayo 17:14-21); kukusanya wafanyi kazi kwa sababu ya mavuno ya kiroho (luka 10: 2); kupata nguvu ili tuyashinde majaribu (mathayo 26:41); na kupata njia ya kuwatia wengine nguvu kiroho (waefeso 6:18-19).

Tunakuja kwa mungu katika mahitaji yetu kamili, na tuko na ahadi ya mungu kwamba maombi yetu si ya bure, hata kama hatupati chenye tunauliza (mathayo 6:6; warumi 8:26-27). Ameahidi kuwa tunapouliza vitu ambavyo viko katika mapenzi yake, atatupa chochote tuitizacho (1 yohana 5: 14-15). Wakati mwingine anakawisha majibu yake kulingana na hekima yake kwa manufaa yetu. Katika hali hii tunastahili kuwa makini na kudumu katika maombi (mathayo 7:7; luka 18:1-8). Maombi yasionekane kama njia zetu za kumfanya mungu kutenda mapenzi yetu duniani, bali iwe ni njia ya mungu kutenda mapenzi yake duniani. Hekima ya mungu inapita hekima yetu.

Kwa hali ambazo hatuwezi jua mapenzi ya mungu kamili, maombi ni njia ya kutambua mapenzi yake. Ikiwa mwanamke myunani aliyekuwa na binti aliyepagagwa na mapepo angeponywa (mariko 7:26-30). Ikiwa kibofu nche ya yeriko angemwita kristo kwa sauti, angebaki kibofu (luka 18: 35-43). Mungu amesema kuwa kila mara tunaenda bila kwa sababu hatuulizi (yakobo 4:2). Kwa njia nyingine maombi ni kama kushiriki injili na watu. Hatujui ni nani ataitikia ujumbe wa injili hadi pale tunapoishiriki. Kwa njia hiyo hiyo, hatuwezi kuyaona matunda ya maombi yakijibiwa hadi tuombe.

Ukusefu wa maombi yaonyesha ukosefu wa imani na ukosefu wa imani katika neno la mungu. Tunaomba ili tuonyeshe imani yetu kwa mungu, kuwa atatenda vile ameahidi katika neno lake na kubariki maisha yetu utele zaidi ya vile tumeuliza na kutumainia (waefeso 3:20). Maombi ni njia ya kuona kazi ya mungu katika maisha ya wengine. Kwa sababu ni njia yetu ya “kujitupa ndani” ya nguvu za mungu, ni njia yetu ya kumshinda shetani na jeshi lake ambalo hatuna nguvu za kulishinda sisi wenyewe. Kwa hivyo mungu anatupata kila mara mbele ya kiti chake cha enzi, kwa vile tuko nakuani mkuu mbinguni anayeweza jua yote amboyo tunayapitia (waebrania 4:15-16). Tuko na ahadi yake kuwa maombi ya mwenye haki yatatenda mengi (yakobo 5:16-18). Na mungu atukuze jina lake katika maisha yetu tunapomwamini na kukuja kwake kila mara katika maombi.

AINA ZA MAOMBI YA KUFUNGA
Tunapofunga na kuomba tunayatafuta mapenzi ya mungu katika jambo fulani. Bwana yesu alitufundisha kuomba na akasema tuombapo tuombe ya kwamba “mapenzi ya mungu yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni” #mathayo 6:10. Kwa hyo kusudi la kufunga na kuomba ni kuyatimiza mapenzi ya mungu hapa duniani kama huko mbinguni! Kuyatimiza mapenzi katika hayo tunayoutafuta uso wa mungu.
Kufunga na kuomba hakumfanyi mungu ayabadilishe mapenzi yake. Hatufungi kuwaonyesha wanadamu ya kwamba sisi ni wa kiroho sana. Kwamba labda twamjua mungu sana. Hapana. Tunayatafuta mapenzi ya mungu maishani mwetu. Haijalishi umeokoka miaka mingi ilopita au hivi karibuni.
Tukumbuke maneno ambayo mungu aliyasema ktk 2nyak 7:14 “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao”
kwa kufunga na kuomba tunamruhusu roho mtakatifu azihuishe nafsi zetu na kutufanya tuweze kusikia sauti ya mungu na kumtii katika maisha yetu.

KWA UJUMLA TUNAFUNGA ILI:
• kuna watu wanafunga kwa sababu za kimwili kabisa. Kwamba miili yao imefika wakati inawapa shida. Matamanio ya mwili yameshindwa kuwasiliana vizuri na roho. Kuna nyakati tamaa za mwili zinakuwa kubwa na hivyo kwa kufunga na kuomba waweza kuutiisha mwili huu. Kwa vijana hasa, vyakula na vinywaji tunavyokula vinaleta shida wakati mwingine ndani ya mwili. Kwa kufunga unautiisha mwili na kuzinyamazisha tamaa hizo. Wengine wanafunga kwa ajili ya kuyatiisha mawazo. Bwana yesu akasema mawazo ndiyo yamtiayo mtu unajisi. Kabla mtu hajafanya uasi fulani huanza kujichafua katika mawazo yake. Ndani ya mawazo yake ataua, atamtukana mtu, atazini, ataiba yani atafanya kila lililo baya kabla hajalifanya katika ulimwengu wa kimwili. Rafiki yangu mmoja akasema ikiwa mwanadamu anaweza kupangilia mipango mbali mbali miovu hadi akaitimiza kwa nn asiweze kufanya hivyo hivyo kwa ajili ya mungu? Kwa hyo wakati mwingine mtu anafunga kuyatiisha mawazo machafu ndani yake. Mawazo machafu hututia unajisi! Ndo maana mtume paulo akasema “basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha mungu” 2kor 7:1
• lakini kiroho tunafunga ili kuweka mahusiano yetu na mungu vizuri rohoni. Ezra 8:21-23
“ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote.

AINA YA MIFUNGO:
1. MFUNGO KAMILI
katika mfungo huu hakuna kula kabisa chakula kigumu bali waweza kunywa maji au kimiminika chochote cha kukusupport.
Siku ngapi waweza kufunga mfungo wa aina hii unategemea na neema na malengo yako katika mfungo huo. Wengine huenda siku moja, mbili, tatu, wiki, n.k n.k
2. MFUNGO NUSU
mfungo nusu huanzia saa 12 asbh hadi saa 9 mchana au kuanzia jua linapoibuka hadi linapozama. Mfungo ambao madhehebu mengine wamewazoeza waumini wao kuufanya. Wengine wameweza kuufanya kila ijumaa. Madhehebu ambayo yamewazoesha watu wao kufunga angalau kila wiki mara moja wameweza kuwa na mafanikio makubwa sana katika kuzifungua nira na vifungo mbali mbali
3. MFUNGO WA DANIEL
daniel alifunga mifungo miwili ya aina yake;
• katika sura ya i daniel alifunga alikula mboga mboga tu (yaweza kuwa alikula mboga mboga na juisi fulani fulani)
• katika sura ya 10 daniel alifunga kwa siku 21 kwa kutokula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwake”

MAOMBI KWAAJILI YA WAGONJWA.
Bwana yesu ninakushukuru kwaajili ya majira na muda huu ambao umenipa kibali kwaajili ya kuombea wagonjwa. Nakushukuru sana mungu wetu kwani wewe ni mwuumbaji wetu. Mungu ulituumba kwa mfano wako na kwa sura yako. Nakushukuru mungu. Asante kwa mamlaka ambayo umetupati wanao kwa damu yako takatifu iliyomwagika msalabani. Asante kwani ulisema tutaweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya. Asante mungu kwani wewe si mwanadamu hata useme uongo.nakuja kwako muda huu kwa unyenyekevu mkuu nikiomba toba kwaajili ya wagonjwa wote. Natubu kwaajili yao bila kujali kuwa magonjwa waliyonayo ni matokeo ya dhambi ipi. Haijalishi iwe ni matokeo ya zinaa,kukiuka kanuni za uumbaji,uchafu,uchawi,uganga au ushirikina natubu mungu wangu. Najua wewe ni mungu wa rehema naam utatusamehe. Natubu kwakutokuamini kwetu naomba utusamehe mungu wetu. Umesema nami ktk neno lako la zaburi 103:3 kuwa akusamehe maovu yako yote,akuponye magonjwa yako yote.ndivyo hivyo mungu leo tenda kwa wagonjwa wote. Haijalishi ni ugonjwa gani mtumishi wako anasumbuliw,haijalishi taarifa ya daktari inasemaje juu ya ugonjwa wake,haijalishi wauguzi wake wamemtishaje na wala haisumbui kuwa dawa zake hazipo duniani kote lakini ninachojua kuwa upo wewe yesu usiyeshindwa jambo. Ktk jina la yesu kristo naachilia uponyaji wa mama yule,baba yule,kijana yule,mtoto yule na wana wa kike kwa wa kiume.pokea uponyaji ktk jina la yesu kristo. Naharibu makao yote ya shetani ndani yako ktk jina la yesu. Nang'oa kila pando lisilotokana na mungu ndani yako sasa ktk jina la yesu kristo. Nafuta maneno yote machafu yaliyosemwa kinyume nawe naam napanda maneno ya kristo ndani yako sasa. Sikia hii ripor ya daktari imesema una ukimwi nami kwa mamlaka ya yesu kristo naifuta riport hiyo naninatangaza riport ya yesu kuwa huna ukimwi tena ktk jina la yesu kristo. Daktari kakuandikia kuwa poor prognosis yaani unakufa nami leo nakuandikia ktk jina la yesu kuwa huta kufa bali utaishi na utasimulia ukuu wa mungu. Ktk jina la yesu natangaza uponyaji kwa kila mgonjwa au ndugu wa mgonjwa aliyesoma sala hii kwa imani. Umekuwa mzima ktk jina la yesu kristo mwana wa mungu. Amina..

Kama una mgonjwa hajiwezi au yupo mbali nawe basi soma sala hii kwa imani kisha ukimaliza mpigie mwambie anywe au anyweshwe maji kidogo kwenye glass na mara atapokea uponyaji ktk jina la yesu. Na wale wenye virusi vya ukimwi baada ya sala hii wakae siku saba alafu wakapime virusi naam wataona mungu atakavyo washangaza. Mrudishie mungu sifa na utukufu kwani yeye ndiye afanyaye

NAMNA YA KUMWITA,KWENDA NA KUMUOMBA MUNGU ILI AKUSIKILIZE.
.yeremia 29:12 “nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza”.
Watu wengi wamekuwa wakitamani maombi wanayoyapeleka mbele za mungu kusikilizwa.watu wanaomba kila aina ya maombi inayowezakana maadam mungu asikie na kuwaokoa kutoka kwenye shida waliyonayo au kuwapa haja za mioyo sawasawa na uhitaji wao.
Wapo wanaoomba na wanaona majibu yao yanajibiwa lakini pia lipo kundi jingine kubwa ambalo wanaona kama vile mungu amenyamaza,amewaacha,hawasikii, au wanajiona kama vile mungu amewakataa na kuziona ahadi za mungu kwamba si za kweli na mbaya zaidi wengine wamefika mahali pa kumwacha mungu kwa sababu ya kushindwa kuvumilia majibu kutoka kwa mungu na hivyo kutafuta njia mbadala za kutatua matatizo yao.wapo walioomba kuhusu watoto,ndoa zao,afya zao,ajira,biashara,elimu zao nk. Walipoona katika fahamu zao mungu hajibu basi wakaamua kwenda kwa waganga wa kienyeji,wachawi na kwa miungu mingine kutafuta msaada huko.
Sasa ili mungu aweze kusikiliza au kujibu maombi yako huenda kuna mambo mengi ya msingi ambayo mwombaji anapaswa kuyajua na kuyatendea kazi.sasa baada ya kuona maombi mengi ninayoomba na pia ambayo wana wa mungu pia wanaomba hayajibiwi ili nilazimu nimuombe mungu anifundishe vizuri kuhusu hili neno.
Hivyo hayo ninayoenda kukushirikisha ni sehemu ya yale ambayo mungu amekua akifundisha naamini na wewe yatakusaidia maana nimeona yakinisaidia binafsi pamoja na wale ambao mungu amenipa kuwafundisha kwa njia nyingine.
Lengo la ujumbe huu ni kukupa maarifa yatakayokusaidia kuomba maombi ambayo wewe mwenyewe.pindi unapoomba utakua na uhakika mungu anakusikiliza kwa wakati  huo.zaidi ujumbe huu umekusudia kukufundisha namna unavyoweza ukapeleka maombi mbele za mungu.
Siku moja nikiwa chuoni mwaka wa kwanza majira ya tisa jioni,nilikua nikipandisha ngazi kuelekea chumbani kwangu ambacho kilikua ghorofa ya tatu juu kabisa.wakati naanza kupandisha zile ngazi nikasikia mtu ananiuliza ndani yangu je hivi mungu huwa anaitwaje?anaendwaje?anatafutajwe?anakaribiwaje? Nilipofika chumbani nikaanza kutafakari haya maswali na baadae ndipo nikapata hii mistari katika yeremia 29:12-13 inayosema “nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza. nanyi mtanifuata na kuniona,mtakaponifuata kwa moyo wenu wote.”Baada ya kuisoma vizuri ndio nikagundua karibu maswali yale yote yalitoka hapa.
Mungu anasema nanyi mtaniita, sasa na mimi nikuulize swali, hivi umeshawahi kujiuliza mungu tunamwitajemwitaje? Tunamwendeaje? Na tunamtafutaje. Usiishie kusema mungu ameseam nikaribieni nami nitawakaribia, umneshawahi kujiuliza anaposema tumkaribie yeye yuko wapi? Na pia tunamkaribia kwa namna gani? Sasa hayo ndio maswali yaliokuwa yakinijia.
Picha ambayo mungu alitaka niipate kwenye zile ngazi ni hii, nifikirie kwamba kile chumba kule juu ndiko aliko yeye yaani mbinguni. Sasa baada ya kufikiria hivyo ndio niwaze na nijiulize amesema nimuite nimwendee nimtafute n.k sasa hivi ndio ninamwitaje, ninamwendeaje na ninamtafutaje? Nilipozidi kutafakari hiyo mistari roho mtakatifu akanifundisha yafuatayo:
Kwanza alinionyesha makosa matatu ambayo watoto wake mara nyingi tumekuwa tukiyafanya wakati wa maombi. Na ningependa na wewe uyajue kwa maana itakusaidia ili bado unayafanya basi usiyafanye tena.

KOSA LA KWANZA, KUOMBA KINYUME AU NJE YA MAPENZI YA MUNGU.
1 yohana 5:14 inasema na huu ndio ujasiri tulionao kwake ,ya kuwa,tukiomba kitu sawa na mapenzi yake atusikia” moja ya tafsiri za kiingereza inasema “we are certain that god will hear our prayers when we ask for what pleases him” kosa kubwa ambalo tumekuwa tukilifanya mara nyingi ni kuomba vitu au mambo ambayo ni kinyume na mapenzi ya mungu.
Anaposema sawasawa na mapenzi ya mungu maana yake ni lazima ujue kwanza nini ni mtazamo au mawazo ya mungu juu ya hilo unalotaka kuliombea.maombi ni kuzungumza au kusemezana na mungu kwa kumwambia yale ambayo amesema kwenye neno lake kuhusu haja zako wewe.
Kwa lugha nyingine usiombe kitu ambacho hujui nini mawazo ya mungu juu ya hicho kitu. Mawazo ya mungu juu ya kila haja ujyonayo yako ndani ya neno lake .hivyo ni lazima neno la mungu likae kwa wingi ndani yako ili unapoomba uombe kulingana na ahadi zake na pia sawa na kile alichokisema.
Zaidi pia wengi wanapotaka kuomba huenda kuhusu ndoa,kanisa,ajira,watoto ,biashara nk huwa wanomba kimazaoea. Maana yake ni hii wengi wamezoea ninpoombea ndoa nitaombea amani,upendo ,furaha nk sasa sina maana hayo maombi hayafai ila ninachotaka ukipate ni hiki hoja unazozipeleka mbinguni hakikisha umefunuliwa na mungu mwenyewe.maana yake mungu ndiye akupe mambo ya kuombea kuhusu nchi ,ndoa,biashara yako nk.

KOSA LA PILI:, KUKOSA UTULIVU NA USKIVU WA ROHONI WAKATI WA MAOMBI NA BAADA YA MAOMBI.
Sikiliza mungu anayo mambo mengi ya kukuambia wewe kuliko yaje wewe uliyonayo wewe kumweleza yeye. Chungu hakiwezi kumwambia mfinyanzi kwamba ulinumba kwa kazi hii tu, bali mfmyazi ndiye mwenye mengi kuhusu kile chungu.
Ndio maana yesu anasema si ninyi mlionichagua mimi bali ni mimi niliyewachagua njnyi (yohana 15:16),sasa watu wengi sana wana bidii nzuri ya maombi wanaweza wakakaa hata masaa matatu mfululizo na hata zaidi wanamuomba mungu tu.
Katika mda huu wote wao ndio wanaojieleza na mara wanapomaliza ni kusema ameni na kuondoka.hii ni picha ya mtoto anayekuja kwako kama mzazi anasema baba/mama naomba hela ya daftari, nauli na ya kula shuleni, pia naomba uninunulie suruali nk. Sasa kabla wewe hujamjibu yeye ameshafungua mlango na kuondoka.sasa kibiblia ndiko kunaitwa kukosa utulivu na usikivu wa rohoni mbele za mungu.
Mara zote unapoomba jifunze kuwa na wakati wa kutulia kusikiliza mungu naye anasema nini.kwenye utulivu ndiko mungu anakosema sio kwenye kelele maana anjua hamwezi kusikilizana.soma isamwel 3:1-10 utaelewa ninachokisema hapa.mungu alisema na samweli alipotulia.

KOSA LA TATU, KUMUOMBA MUNGU WAKATI TAYARI UMESHAJITAFUTIAJIBU LA SHIDA ULIYO NAYO.
Hili ni kosa jingine kubwa ambalo wana wa mungu wamekuwa wakilifanya. Wengi wana mahitaji mbalimbali.wapo watu wengi ambao kweli wanaomba kwa kumaanisha mbele za mungu na wengine hata kufunga kwa masaa mengi lakini tatizo lao katika fahamu zao wameshafanya uamuzi wa nini watafanya baada ya maombi yao.sasa hata mungu akikushirikisha mawazo yake si rahisi ukamwelewa kwa sababu tayari kwenye nafsi na ufahamu wako kuna jibu na biblia inasema aonavyo mtu katika nafsi yake ndivyo alivyo.
Sambamba na hilo, kosa linalofanana na hili ni wale watu wanaomwomba mungu afanye kama vile wao waonavyo kataka nafsi zao. Yaani wanamtaka mungu akubaliane na mawazo yao na njia zao juu ya shida au haja walizo nazo wao wenyewe.
Na jambo hili tunalielewa vizuri tunaposoma katika kitabu cha luka 9:12 -17 .habari za wanafunzi wa yesu pindi njaa ilipokuwa ikiwauma watu wakati yesu anaendelea na mkutano. Wao walimwambia bwana waage watu wakajijinunulie chakula vijijini na mashambani, wao walidhani hili ndilo jibu la njaa ya watu. Hawakufikiri kwamba sio wote wenye pesa za kununua chakula, kuwaaga watu kungemaanisha yesu aache kufundisha nk. Sasa jibu la njaa ya wale watu halikuwa kama wanafunzi walivyowaza na walivyotaka bali jibu lilikuwa kwa yesu kufanya muujiza wa kubariki mikate mitano na samaki wawili vitosheleze watu wote 5000.
Sasa baada ya kuwa tumeona hayo makosa makubwa matatu tuangalie mungu anaposema nanyi mtaniita,mtakwenda na kuniomba,nami nitawasikiliza ana maana gani?.
Katika mstari huu kuna mambo makubwa matatu yamezungumziwa.

MOJA NI MTANIITA,MBIII MTAKWENDA NA KUNIOMBA, TATU NI NAMI NITAWASIKILIZA.
JAMBO LA KWANZA NI ,MTANIITA.
Ukisoma kitabu cha yeremia 33:3 anasema “niite,nami nitakuitikia ,nami nitakuonyesha mambo makubwa,magumu usiyoyajua. Mungu ansema utakapomwita yeye atafanya mambo mawili.moja atakuitikia na mbili atakuoyesha mambo makubwa,magumu usiyoyajua.
Maana yake ni hii, kukuonyesha mambo makubwa,magumu usiyoyajua ni kukufunulia mambo ambayo ulikuwa huyajui katika lile ulilomuita.hivyo basi kumuita mungu ni kumuomba au kumtaka mungu akufunulie mambo makubwa na magumu usiyoyajua kuhusu shida au hitaji au haja uliyonayo mbele zake.mfano unamuita mungu akufunulie ndoa yako jinsi ilivyo, nini kinaendelea usichokijua, nini ukiombee, nini hakijakaa sawasawa kwenye hiyo ndoa k.
 hivyo basi unapotaka kuomba juu ya jambo lolote lile ni vizuri kwanza ukamuita mungu juu ya hilo jambo.maana yake muombe mungu akupe picha kamili ya hilo unalotaka kuliombea,akufunulie jinsi lilivyo ili ujue uanzie wapi kuomba.,kama ni ndoa,nchi,mke au mme mtarajiwa,huduma yako nk.

JAMBO LA PILI MTAKWENDA NA KUNIOMBA.
Sasa baada ya kuwa umemuita mungu kinachofuata ni kwenda na kumuomba mungu. Anaposema mtakweda na kuniomba ana maana mtaanza kuomba sawasawa na vile nilivyowaonyesha au nilivyowafunulia wakati mliponiita katika haja zenu.hivi ulishawahi kujiuliza ni mambo gani makubwa na magumu ambayo mungu atakuonyesha_pindi utakapomuita?. Kumbuka tulikotoka tumeona kumuita mungu ni kumfanya mungu akufunulie mambo usiyoyajua kuhusu hitaji lako ili ujipange vizuri kuyaombea.
Sasa kwenda na kuomba maana yake ni kuomba sawasawa na vile mungu alivyojifunua kwako kuhusu hitaji ulilonalo.utakapoomba namna hii ndiko kunaitwa kuomba sawasawa na mapenzi ya mungu maana yake unaombea mambo ambayo mungu anataka uyaombee kwa wakati huo. Kwa lugha nyepesi jifunze kuomba mambo ambayo mungu anakuongoza kuyaombea. Labda nitoe mifano michache ndio somo litaeleweka vema.
Mfano wa kanza huenda mnaombea mgonjwa au mtu aliyefungwa na mapepo. Ni kweli biblia imesema mtaweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya.sasa si kila mgonjwa ni wa kuweka mikono na kuanza kukemea ugonjwa au mapepo, kuna magonjwa mengine yanasababishwa na mawazo yaani tatizo ni mtu mwenyewe, mwingine huenda ni kwa sababu ya kujeruhiwa nafsi yake na mwingine huenda ni kwa sababu ya dhambi, na mwingine huenda mikataba aliyoingia mwenyewe na mapepo na huenda mengine ni mungu mwenyewe ameruhusu shetani aguse afya ya huyo mtu kama alivyomruhusu shetani kwa ayubu nk..
Saa nafikiri mpaka hapa umeshaona si wagonjwa wote utakawawekea mikono watapona. Hivyo ni vema umuite mungu akufunulie nini cha kufanya, mwingine atakuambia huyu anahitaji ushauri tu wala si maombi,mwingine anaweza kukuambia huyu ametenda dhambi hii na hii akizitubia nitamponya, na mwingine atakuambia huyu hicho ni kipimo chake mpe tu neno la uvumilivu na ushindi,mwingine atakuambia huyu ndugu mwenyewe au wazazi wake waliingia mkataba na mapepo hivyo vunja kwanza mktaba huo nk.
Mfano wa pili,huenda mnaombea kanisa lenu. Ni rahisi kusema tumuombe mchungaji ndani ya kanisa,mara tuombee kamati ya ujenzi tuombe mungu kuhusu ujenzi nk.kweli ni maombi mazuri lakini una uhakika mungu kwa wakati huo anataka muombee hayo mambo.huenda kuna roho ya mpinga kristo ina vamia washirika au kuna maajenti wanajiingiza kwa siri makanisani na kuwapofusha macho ninyi mnakazana kuombea ujenzi. Maana yangu ni hii ikiwa wewe ni mchungaji au kiongozi wa maombi katika kundi lolote lile ni vema kila wakati kumuita mungu akupe mambo ya kuombea kwa wakati huo. Mungu atakufunulia nini unachotakiwa kuombea kwa wakati huo.
Nina ujasiri na ninachokisema kwa sababu siku moja tukiwa katika kambi la vijana.nilikuwa kwenye timu ya maombi ya hilo kambi.ndani ya hiyo timu tulikuwa na wajumbe wa shetani kutoka kuzimu yaani maajenti (vibaraka wa shetani).hawa jamaa walikuwa wakiomba na kufimga kuzidi masaa yale tuliyokuwa tukifunga sisi.na wakati wa kuomba walikuwa wanapendekeza tuombee na kukemea roho ambazo hazifanyi kazi katika lile eneo tulilokuwepo.na walikuwa wanajita watumishi wa mungu.nina uhakika wa habari hii kwani mungu alinifungua macho tukaomba na nguvu za mungu ziliposhuka mmoja wo akasema “sisi ni wajumbe wa shetani kutoka kuzimu,tulitumwa kuleta uharibifu lakini katika yale tuliyotumwa tumeshindwa kuyatekeleza”.
Nakuambia tangia siku hiyo ndipo nilipofunguka macho yangu ya ndani na kuanza kuhitaji uongozi wa mungu katika yale tunayoomba kila siku.hujawahi kuona kiongozi wa maombi anasema jamani hee tutaombea hili na hili na hili,lakini mnapoanza kuomba unakuta mungu anakuongza kuombea vitu vingine kabisa ?.
Kumbuka siku zote katika kila unaloliomba ,mwambie mungu nifunulie zaidi kuhusu mambo ya kuomba kuhusu hili jambo.lwe ndoa,kanisa,mkutano au semina,watoto,elimu nk sasa nimalizie kwa kusema kuomba kwa namna hii ndiko kibiblia kunaitwa kumtafuta bwana.sikiliza huwezi kumtafuta mtu mahali asikopatikana.unapomtafuta bwana ni lazima umtafute kwenye maeneo yake yaani kule anakopatikana.sasa kunaitwa kumtafuta bwana kwa sababu umeomba kulingana na ufunuo wake
Ni imani yangu kuwa baada ya kuwa umesoma ujumbe huu basi naamini umeshapata maarifa ya kukusaidia katika kumtafuta bwana na hivyo kwa jambo lolote utakalotaka kuomba siku zote utaomba kwanza ufunuo wa mungu juu ya hili jambo.

IMANI YAKO ITAKUPONYA, MWAMINI BWANA YESU LEO
Kila mwaka tarehe 1 / 12 ni siku ya kuadhimisha janga la ukimwi kwa kuwa na ujumbe mbalimbali jinsi ya kutokomeza na kuelemisha watu jinsi ya kujikinga na kuzuia maambukizo mapya ya virusi vya ukimwi na vile vile kuishi kwa matumaini kuhusiana na ugonjwa huu. Japo kuna baadhi ya maeneo elimu bado sijui niseme ni changa au haijawafikia walengwa vizuri, na  la kushangaza yakiwemo baadhi ya maeneo ya mijini yakiongoza kwa asilimia kubwa ya kuwa na maongezeko mapya ya mambukizi ya virusi vya ukimwi. Swali la kujiuliza ni kuwa watu hawataki kuelewa au ni elimu imezoeleka kiasi kwamba watu wanaona hakuna jipya au maisha ndio yanawalazimisha kutokuzingatia yanayosemwa. Au je waelemishaji nao pia hawana elimu ya kutosha ya kuwaelimisha watu / watoaji elimu ni wachache kuliko walengwa / walioathirika? Au wamekosa imani na asasi / ngo zinazotoa huduma hii? Ukiangalia kwa mtazamo wa kawaida tu kuna asasi/ngo mbalimbali zimeazishwa kwa ajili ya kusaidia na kuelimisha waathirika wa ukimwi / na ambao bado hawajapata maambukizi pamoja na watoto yatima na wajane. Je wanatoa elimu sahihi na yakutosha? Kama ndio kwa nini kuna ongezeko kubwa la watoto yatima na maabukizi mapya yanaibuka siku hadi siku? Au waanzilishi  wa hizi asasi / ngo wanatafuta maslahi yao wenyewe kwa kupitia mgongo wa walioathirika badala ya kutoa elimu ya sahihi na ya kutosha? Japo kwenye takwimu zinaonyesha kuwa tanzania imeshuka kwenye kiwango cha maambukizi ya ukimwi ukilinganisha na nchi nyingine za africa. Je hili nalo ni kweli yanaweza kuwa ongezeko la maambukizi mapya limepungua wakati bado tunashuhudia watoto yatima wakiongezeka kutokana na hili janga? (tutafakari hili) mimi sina jibu ila haya yote ni mtazamo wa kibinadamu tu. Hebu tungalie biblia inatuambia nini kwa habari ya magonjwa? Je kuna ambalo linashindikana kwa bwana? Kama yeye alitufinyanga kwa mikono yake si anajua kila sehemu ya viungo vyetu hivyo ni rahisi yeye kuturekebisha pale penye madhaifu na kupatia uzima. Hebu tuone biblia inasema nini basi kwa habari ya uponyaji....

Ukisoma kwenye biblia zetu utaona kwamba ukoma ndio uliokuwa ugonjwa mbaya sana na ulikuwa unatishia watu enzi hizo za kale pia ulikuwa ni ugonjwa usioponyeka lakini watumishi wa mungu walikuwa wanauwezo wa kuwaponya watu kutokana na ugonjwa huu kilichokuwa kinahitajika ni imani na kutii tu, kwa mfano naaman aliyekuwa unaukoma lakini alipokea uponyaji. Soma 2wafalme 5: 8-19 na pia soma mathayo 8:1-4 yesu anaponya ukoma.

Japo kwa jambo la kushangaza na la kuhuzunisha ni kuwa huu ugonjwa hadi sasa upo toka enzi za akina musa hadi leo lakini je ni kwamba dawa za kuuponya huu ugonjwa haijapatikana? Imepatikana na ipo sema watu hawatilii maanani. Wako wapakwa mafuta wa bwana ambao wamepewa karama ya kuponya wanaponyesha huu ugonjwa, kadhalika na ukiwmi pia wako watumishi wapakwa mafuta wa bwana waliopewe karama ya uponyaji wako kukusaidia leo. Kama huu ukoma ambao ulikuepo toka enzi hizo za akina musa unawezekana kuponyeka kwanini watu wasiamini kuwa hata ukimwi waweza kupona? Ukimwamini mungu na kuyashika maagizo yake na kutii hakika utapona.

Mfano wa mwanamke aliyetoka damu kwa miaka kumi na miwili biblia inatuambia kuwa yule mwanamke aliazimia kuwa akiweza kushika tu upindo wa vazi aliyovaa yesu hakika atapona na kweli alivyofanya hivyo kwa imani yake kuu aliyokuwa nayo alipokea uponyaji muda ule ule soma mathayo 9 : 20 - 22; pia kwenye marko 5: 25-34; sasa je wewe wawezaje kukata tamaa na kushindwa kumwammini yesu kuwa kwa jina lake tu magonjwa yanatoweka hayatakuwa na nafasi tena ndani ya maisha yako utapona na utakuwa na nguvu na mwenye afya tele. 

Kama bado haujaambukizwa acha njia zako mbaya mtafute yesu shika maagizo yake na kuyatenda hakika atakuponya na hili janga wewe na familia yako na watu wa nyumbani mwako. Ingawa unaweza kuwa mwaminifu, waweza kuwa unatenda yaliyo mema kwa mtazamo wa kibinadamu lakini bado ukaupata huu ugonjwa kwa njia nyingine kwa mfano katika ajali kama ya gari, pikipiki au njia yoyote ile nk. (unajua kuwa maambukizi waweza pata kwa njia nyingi si kwa kuzini tu japo kuzini ndio njia kubwa ya maambukizi haya ya virusi vya ukimwi). Lakini ukimtegemea mungu na kukubali kuwa yesu alikufa msalabani kwa ajili yako  na kuyatenda yote aliyokuamuru, hali hii haitakupata wewe na familia yako kwa ujumla na hata hutaacha wanao yatima bali utaishi hadi miaka mia na ishirini na utakufa ungali ukiwa na nguvu zako.

Yesu alifanya miujiza mingi ya uponyaji na hata sasa bado anafanya kwani anawatumia watumishi mbalimbali kufanya kazi aliyoianzisha kinachoturudisha nyuma ni kutokutilia maanani na imani kuwa haba kama nilivosema hapo juu. Watu tumekuwa na kiburi tukidhani kuwa wanayofanya watumishi wa mungu ni ya uongo lakini mimi nakusihi leo hebu mwamini yesu halafu utaona matunda yake na hakika hautajuta. Soma mistarii hii ikusaidie kwa habari ya imani katika uponyaji mathayo 8 : 5-13; mathayo 8 : 14-17;
Mathayo 9 : 27 - 31 n.k.

Mwamini yeye leo mtumainie bwana peleka haja zako kwake naye atatenda, atakushindia na pia atakuponya, usikate tamaa usihangaike ikuze imani yako kwa kusikiliza na kusoma neno la mungu mara kwa mara kwani biblia inasema hivi "imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la kristo"
Warumi 10 : 17 kisha mweleze shida yako peleka haja zako kwake naye atafanya. Pia yesu anasema hivi, hata ukiwa na imani kiasi cha punje ya haradali ukisema mlima huu ung'oke mahali hapa uende kule, nao utang'oka. Hivyo basi na uponyaji wako unahitaji imani yako kidogo tu kama punje ya haradali kwa yesu kuwa anaweza kukuponya nawe utapokea uponyaji. Tumwamini yeye tuuone mkono wa bwana ukitenda ndani ya maisha yetu.

 MAOMBI, UPONYAJI NA UREJESHAJI
(yakobo 5:13-20)
Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye >>pentecostalchurch2.blogspot.com>>kwa lugha ya kiswahili na kwa lugha ya kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile kifaransa, kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa roho mtakatifu unapojifunza.

UTANGULIZI: JE, umewahi kuwasikia watu wakisema kuwa wanaabudu kwa namna zao wenyewe? Wamechoshwa na “kanisa” na kwamba kukutanikia jangwani ni bora zaidi kwa sababu jangwa haliwaambii maneno yasiyo mazuri. Ingawa ni ukweli kwamba ni muhimu kutenga muda binafsi wa kuwa na mungu, katika somo letu juma hili yakobo anaelezea manufaa ya kushirikiana [kuchangamana] kiibada na wakristo wenzetu. Hebu tuzame kwenye somo letu la biblia ili tujifunze zaidi!


USHIRIKA NA MUNGU
A. SOMA YAKOBO 5:13. Maelezo ya fungu hili yanatuhusu watu wengi. Uwezekano mkubwa ni kwamba aidha tuna matatizo au hatuna furaha. Tunatakiwa kuitikiaje uzoefu huu wenye tofauti kubwa? (kwa kumgeukia mungu. Ama tunatakiwa kuomba kwa ajili ya kupata msaada au tunatakiwa kumsifu mungu kwa njia ya nyimbo.)
1.  Mwitikio wako kimaadili ni upi unapojikuta kwenye matatizo? (siku za nyuma, papo hapo nilifanya kile nilichoweza ili kutatua tatizo. Sasa nimejifunza kwamba hatua ya kwanza lazima iwe ni kumgeukia mungu.)
2.  Je, huwa unakasirika unapokabiliana na matatizo? (asili ya mwanadamu huwa ni kuwalaumu watu wengine, na kisha kukasirika kutokana na kile walichotutendea. Ikiwa, kwa uwezo wa roho mtakatifu, tutamgeukia mungu kwanza, itatuepusha kusema au kutenda jambo baya papo hapo kwa sababu ya hasira. Hii itaepusha kufanya tatizo kuwa gumu zaidi.)

B. Mtazamo wa namna gani unaakisiwa kwenye ushauri wa yakobo kwa ajili yetu kuomba au kusifu? (mungu ndiye anayeyashikilia maisha yetu. Yeye ndiye chanzo cha mibaraka yote. Tunamgeukia ili kupata msaada na tunamshukuru kwa kumpa sifa.)

   USHIRIKA NA WAUMINI
A.  Soma yakobo 5:14-15. Kuugua ni mfano mahsusi wa tatizo. Kwa nini usijiombee tu wewe mwenyewe – kama anavyobainisha yakobo katika mstari wa 13? Kwa nini kuwahusisha wazee katika jambo hili? (mungu hahitaji wazee kumshawishi ili afanye uponyaji, lakini wazo la kushirikiana na waumini wenzako linaelezewa hapa.)
1. Kuna nyakati kadhaa nilikuwa sehemu ya kundi la wazee waliomwombea na kumpaka mafuta mgonjwa. Nchini marekani, watengenezaji wa dawa wanaeleza bayana athari za dawa zao wakati ule ule wanapotangaza jinsi dawa zao zinavyoweza kutibu. Mke wangu alikuwa akiniambia kwamba nilitakiwa kubainisha jambo hili nilipokuwa sehemu ya wanaofanya maombi na kupaka mafuta katika kipindi cha nyuma ambapo wagonjwa hawakupona. Mke wangu alikuwa akitania, lakini hadi siku za hivi karibuni, jambo hilo lilibakia kuwa ukweli mtupu. Je, yakobo anatoa ahadi za uongo kuhusu uponyaji?
A.  Je, mimi ndiye niliyekuwa tatizo? Yakobo anapoandika “na kule kuomba kwa imani,” je, alikuwa akiandika kuhusu imani ya wazee? Kama sivyo, anaelezea imani ya watu gani, je, ni imani ya mgonjwa?
B. Soma marko 2:1-5. Je, hapa yesu anazungumzia imani ya nani? (haiko wazi. Yesu anaonekana kuzungumzia imani yao wote.)
C.  Soma mathayo 18:19. Vipi kama mgonjwa alikuwa na imani na mzee mmoja pekee ndiye alikuwa mwenye haki, je, imani hiyo ingetosha kuleta uponyaji? (utagundua kwamba yesu haonyeshi kiwango cha imani au haki inayotakiwa, anabainisha tu idadi ya waumini waliokubaliana. Wawili wanatosha.)
D. Hebu tuangalie tena yakobo 5:15. Je, yakobo anatoa muda wa kuinua na kuponya? (hapana. Nina uhakika kila mtu aliyekuwa kwenye huduma ya kupaka mafuta ambapo mimi pia nilihusika alikuwa mdhambi – kuanzia mgonjwa hadi kwa wazee wote. Yakobo hasemi kwamba hatutakiwi kuwa na dhambi, anasema kwamba tunatakiwa kuwa na imani. Kwa kuongezea, hatoi muda kwa ajili ya uponyaji. Ninaamini mungu atawafufua katika uzima wa milele wote waliolala wakimtumaini yeye.)
E.   Kipindi cha hivi karibuni kabisa ambapo nilikuwa sehemu ya kundi la wazee waliokwenda kufanya maombi, mgonjwa aliponywa. Mungu anatenda miujiza maishani mwangu, na kwenye maisha ya wale ninaowaombea, na ninaamini hili linahusiana zaidi na mapenzi ya mungu mwenye enzi, badala ya haki yangu. Je, wewe unadhanije?

UPONYAJI, IMANI NA DHAMBI
A. Angalia tena sehemu ya mwisho ya yakobo 5:15 na marko 2:5. Yesu anamwambia mwenye kupooza kwamba dhambi zake zimesamehewa. Yakobo anasema, dhambi zinaweza kusamehewa. Je, kuna uhusiano gani kati ya uponyaji na dhambi?
B.  Soma yohana 9:1-3. Kwa nini wanafunzi waliuliza kuhusu dhambi na upofu? (uelewa wa kipindi hicho ulikuwa ni kwamba dhambi ilisababisha magonjwa. Nadhani bado kuna ukweli mwingi kwenye uelewa wao.)

1.  Je, yesu alisema kuwa sababu ya upofu ni ipi? (ili mungu aweze kutukuzwa. Haikuwa suala la dhambi.)
2.  Dhambi inapoungamwa na kusamehewa, je, mungu anatukuzwa? (ndiyo! Angalao kauli za yakobo na yesu kuhusu ugonjwa na dhambi zina maelezo ya aina mbili. Kwanza, ni uelewa wa watu wa kipindi hicho. Lakini, jambo la muhimu zaidi ni kwamba, mungu anataka kutuponya dhambi. Lengo lake kuu kwetu ni kuwa na maisha yasiyo na dhambi na ugonjwa – na lengo hilo litatimia mbinguni.)
C. Siku chache zilizopita nilikuwa mapumzikoni kwa muda wa siku kadhaa eneo la “disney world,” ambapo watu wanene wanakusanyika na kuendesha vijigari. Kiukweli, watu wengi waliokuwepo mahali pale pia walikuwa wanene. (katika kuzungumzia suala la unene, niliweza kuongezeka uzito wa kilogramu 1.8 nilipokuwa likizo!) Wakati huo huo, sikumwona mtu hata mmoja akivuta sigara. Inaonekana kwamba hatari ya kiafya inayotokana na uvutaji wa sigara imebadilishwa na hatari ya kiafya inayosababishwa na unene mkubwa kupita kiasi. Swali gumu ni hili: je, dhambi inaweza kuingiliana na uponyaji?
1.  Kama utasita kumwombea mvuta sigara ili aweze kuponywa, vipi kuhusu mtu mnene kupita kiasi?
2.   Je, kiasili baadhi ya watu si ni wanene tu? Je, hilo linajalisha?
3.  Nimesoma sana kuhusu ubongo, na ninashawishika kwamba mazoezi ni tiba ya watu wote kwa magonjwa ya aina yote, yakiwemo masuala ya kiakili. Je, kushindwa kufanya mazoezi ni dhambi inayotuzuia tusiponywe?
4.  Je, nimemtukana takribani kila mtu? Ninachokimaanisha ni kwamba tunawaangalia wavuta sigara wanaougua saratani ya mapafu, na wasenge wanaougua ukimwi, na hatuwahurumii sana kutokana na matendo yao.

KUTUBU [KUUNGAMA] DHAMBI
A.   Soma tena yakobo 5:15. Muda wa msamaha ni upi? (baada ya mtu kuponywa. Hii inaashiria kwamba uponyaji upo kwa ajili ya watu wote.)
B.  Soma yakobo 5:16. Hebu subiri kidogo! Baada ya mjadala wetu juu ya dhambi, je, yakobo anasema kuwa tunatakiwa kutubu dhambi zetu ili tuweze kuponywa? Au, je, kuombeana sisi kwa sisi ndio kigezo pekee kinachohusiana na uponyaji?
C. Angalia tena yakobo 5:16. Unafikiria nini kuhusu kutubu dhambi kwa waumini wenzetu?
D. Soma zaburu 51:4, zaburi 32:5 na 1 yohana 1:9. Je, mafungu haya yanapendekeza kwamba tutubu dhambi zetu kwa nani? (tunatenda dhambi dhidi ya mungu, na mungu ndiye ana uwezo wa kusamehe dhambi. Hivyo, inaleta mantiki kutubu dhambi zetu kwa mungu.)
E.  Unapotafakari kuhusu jambo hili, je, kuna aina mbalimbali za kutubu? (ninadhani hivyo. Kwanza, kuna kutubu na msamaha wa dhambi, jambo ambalo ni suala kati yako na mungu. Pili, mathayo 18:15, luka 17:4 na mambo ya walawi 6:1-5, mafungu yote hayo yanaashiria kwamba kuna dhambi ambazo tunatakiwa kuombana msamaha sisi kwa sisi. Tatu, ni kile ninachodhani yakobo anakizungumzia; mantiki ya jumla kwamba tunatenda kazi na waumini wenzetu ili kuelekea kwenye haki. Tunaombeana sisi kwa sisi, tunajadiliana dhambi zetu sisi kwa sisi, tunajadiliana masuala ya kiroho sisi kwa sisi.)

NGUVU YA MAOMBI
A. Soma yakobo 5:17-18 kisha usome sehemu ya mwisho ya yakobo 5:16. Tumekuwa tukijadili juu ya dhambi, lakini nadhani yakobo amejikita kwenye maombi. Kwa nini yakobo anamtaja eliya kama mfano? (anasema alikuwa “mwanadamu mwenye tabia moja na sisi.” Sote tuna uwezekano wa kuwa na maombi yenye nguvu na ufanisi mkubwa.)
1. Soma 1 wafalme 19:3-4. Kwenye mjadala wetu hadi tulipofikia, nimelinganisha [nimehusianisha] masuala ya kiafya na dhambi. Katika mathayo 15:16-18 yesu anapendekeza kwamba mlingayo huu si sahihi. Kwa upande mwingine, kutokumtumaini mungu ni dhambi (ufunuo 21:8). Yakobo anapotuelekeza kwa eliya, je, anasema nini? (imani na udhati katika maombi ndio ufunguo wa uponyaji, sio kutokuwepo kwa dhambi.)
B. Soma yakobo 5:19-20. Haya yanaonekana kama madai ya mwisho ya “matendo” – ikiwa tutawaongoa upya “waliorudi nyuma” dhambi nyingi zitasamehewa. Je, muktadha huu unaashiria kuwa uelewa sahihi wa jambo hili ni upi? (unazungumzia juu ya uelewa wetu wa dhambi, badala ya asili ya wokovu. Sura hii ilikuwa inazungumzia juu ya kufanya ushirika [kuchangamana]. Ikiwa mtazamo wako ni kuwaunga mkono na kuwaokoa washiriki wenzako wa kanisa, basi kitendo hicho, badala ya kupoteza muda, ndicho kilicho cha muhimu machoni mwa mungu.)
C.Rafiki, je, wewe ni sehemu ya watu wanaofanya ushirika wa mara kwa mara? Kama wewe si sehemu ya kundi hilo, basi unakosa kipengele cha muhimu sana cha kuwa mkristo. Kwa nini usitubu juu ya jambo hili na kuungana na kundi linaloshikilia imani na utii?


MAOMBI YA KUSAMBARATISHA UCHAWI NA NGUVU ZA GIZA



Baba katika jina la yesu. Laana zote nilizo tupiwa na wabaya wangu zimeshindwa kwa jina la yesu na nazivunja na kuzisambaratisha kwa damu ya yesu. Mshindwe wote mnao tuma laana kwangu katika jina la la yesu.

Nawavunja na kuwaharibu na kuwakatakata wachawi wote kwa damu ya yesu.

Nasambaratisha kila neno la uovu lililosemwa juu yangu na famila yangu katika jina la yesu.

Naharibu na kuisambaratisha madhabahu yenu mliyo fanyia kafara kwa damu ya yesu.

Navunjavunja na kubomoa kila uovu na uchawi mnaonifanyia katika jina la yesu.

Nairudisha misukule yote na majini yote yawarudie nyie na kuwalipa dhambi zote mnazo fanya katika jina la yesu.

Naharibu kila uchawi, kila urogi, kila ndumba kila aina ya uovu ambao mnaufanya ili uniumize mimi na familia yangu katika jina la yesu.

nawateketeza kupitia damu ya yesu wachawi wote walio tumiwa kunitumia uchawi katika jina la yesu.

Nawateketeza na kuwaharibu majini yote yaliyo tumwa kuja kufanya kazi hiyo waliyo tumwa na wachawi katika jina la yesu.

Nawateketeza na kuwauwa makuhani wote ambao walienda kunishitaki kwa wachawi ili waniharibie maisha, nawateketeza kupitia damu ya yesu. Nawachoma kwa moto wa roho mtakatifu katika jina la yesu.

Nateketeza aina zote za vyombo vya kichawi vilivyo tumiwa kuja kunichunguza katika jina la yesu.

Naharibu fikra zao zote ambazo wanazitumia kufanya kazi zao za kichawi katika jina la yesu.

Nafuta kumbukumbu zoote zangu ambazo wamewapa mashetani, majini, roho chafu, nafuta hizo kumbukumbu kwa kutumia damu ya yesu, katika jina la yesu aliye hai.

Nawateketeza waweka kumbukumbu wa kimashetani kupitia damu ya yesu aliye hai. Naharaibu na kuchoma kupitia moto wa roho mtakatifu makabrasha yote yenye kumbukumbu zangu katika jina la yesu.

Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuharibu maisha yangu na ubomoa kupitia damu ya yesu.

Kila uchawi ulio fanywa ili uje kuniua nauvunja na kuuteketeza kupitia damu ya yesu.

Kila uchawi ulio fanywa ili kuja kuiba mali zangu, nauvunja na kuubomoa na kuuharibu kupitia damu ya yesu.

Kila uchawi ulio fanya kuja kuniharibia familia yangu, nausambaratisha na kuuvunja na kuubomoa katika jina la yesu.

Kila neno la kichawi lililo tumwa ili kuja kuniharibia, kunidhihaki, kunitendea mabaya nalirudisha kwa aliye lituma katika jina la yesu.

Kila uovu, uchawi, wanga, ndumba, ramli, yaliyo tumwa kuja kwangu navunja yote hayo kupitia damu ya yesu na katika jina la yesu.

Nyota yangu ambayo wanaita nairudisha kupitia damu ya yesu. Nyota yangu ya baraka nailinda na kuzungushia na kuizingira na damu ya mwana kondoo katika jina la yesu.

Namteketeza yule mtu aliye kuja kuiba nyota yangu katika jina la yesu.

Nateketeza mbinu zote wanazo tumia ili kuja kuiba nyota yangu katika jina la yesu.

Nateketeza wivu wao, chuki yao, laana zao, maovu yao na kila aina ya uchafu ambao wanao kwa ajili yangu katika jina la yesu.

Naizungushia na kuizingira nyumba yangu na damu ya yesu.

Naishungushia na kuizingira familia yangu na damu ya yesu.

Nashungushia na kuzingira maisha yangu yote na damu ya yesu.

Navunja laana zote zilizo semwa na mabau zangu katika jina la yesu.

Navunja laana zato ambazo zilisemwa bila ya mimi kufahamu, nazivunja na kuziharibu kupitia damu ya yesu na katika jina la yesu.

Narudisha kila mali walizo ziiba kutoka kwangu katika jina la yesu.

Narudisha kila baraka walizo ziiba kwangu katika jina la yesu.

Narudisha amani na upendo katika familia yangu.

Damu ya yesu ipo juu ya maisha yangu na inasafisha kila uovu, kila uchawi unaaribiwa na damu ya yesu katika jina la yesu.

Leo hii mtaiona nguvu iliyopo katika damu ya yesu.

Katika jina la yesu aliye hai ninaomba.

Amen


MUNGU AKUBARIKI SANA KWA KUPATA KITABU NINAMANI KITAKUSAIDIA / KIMEKUSAIDIA KATIKA KAISHA YAKO YOTE.

HII NI SEHEMU YA KWANZA YA KITABU JUU YA SOMO LA MAOMBI.



KIMEANDALIWA NA MWINJILIST LAURENT E. MPOMA.

KANISA LA PENTECOSTAL CHRISTIAN CENTER – MISUNA SINGIDA

KUJIPATIA VITABU VINGINE AU UNAHITAJI MAOMBI FIKA KANISANI PENTECOSTAL CHRISTIAN CENTER – MISUNA –SINGIDA

AU PIGA SIMU:+255763652896, 714890889.

MUNGU AKUBARIKI SANA>>>>>>AMINA.



Read More »